Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote lakini nafikiri hilo lingewezekana tu kama tungekuwa na bunge huru ambayo sio muhuri kama hili la siku zote.

Lakini kwa bunge hili la sasa ambapo wabunge wa ccm wanatakiwa kuunga juhudi bila kuhoji hamna kabisa ulazima wa kuwa na wabunge wasomi kwa upande wa ccm ila kwa upande wa upinzani sawa kuna ulazima.

Ndio maana tunahitaji katiba mpya ili bunge, mahakama na taasisi zingine zimalize vifungo vyao kutoka kwa rais ambaye hii katiba imemuacha awe dikteta.
 
Kama Msukuma Kuna mda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?????

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri????
Laizer
 
Kuna elimu na akili,wapo wenye elimu lakini hawana akili nawapo wenye akili hawana elimu,kusoma sio kuelimika na uongozi ni akili na karama,,ndomana unaweza kuwa msomi ukaajiliwa na asiye msomi, naunaweza kuwa msomi ukawa masikini wa Mali ha akili,,
 
Kama Msukuma Kuna mda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?????

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri????
Naunga mkono hoja yako.Na niseme jambo moja Mfumo wa elimu yetu unatakiwa kubadilika.leo vijana wetu wanaenda kukaririshwa tu na ndio kufaulu kwao. Hakuna wanachoengeza .ndio sbb mtu wa darasa la saba anaweza kuwa na hoja kuliko wenye digrii.
 
Kuna elimu na akili,wapo wenye elimu lakini hawana akili nawapo wenye akili hawana elimu,kusoma sio kuelimika na uongozi ni akili na karama,,ndomana unaweza kuwa msomi ukaajiliwa na asiye msomi, naunaweza kuwa msomi ukawa masikini wa Mali ha akili,,
Kweli mkuu wapo watu hawana elimu au wana elimu ndogo sana lakini watu mbali mbali wanawakimbilia kwa maswala ya kijamii kutafuta ushauri.
Ajabu yake wanajua kujenga hoja zenye mpangilio na mtiliko ulio rahisi na sahihi kuelewa.
 
Naunga mkono hoja yako.Na niseme jambo moja Mfumo wa elimu yetu unatakiwa kubadilika.leo vijana wetu wanaenda kukaririshwa tu na ndio kufaulu kwao. Hakuna wanachoengeza .ndio sbb mtu wa darasa la saba anaweza kuwa na hoja kuliko wenye digrii.
Kati ya mambo yanayonifanya nisiichague tena CCM kwenye uchaguzi huu

1. Ni kuharibu mfumo wetu wa Elimu na kuzalisha watu wa hovyo wasio na chochote

2. Ni kushindwa kupanga makazi na mipango miji

Kwa hizi sababu kuu mbili hakuna anayeweza kunishawishi lolote juu ya CCM
 
Sina Nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya Leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muimu Sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho Sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa Sasa. Tumebaki nyuma Sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Katiba mbovu kabisa
 
Kazi ya mpiga kura ni kuchagua tu, na wagombea wanapewa siku 60 kuongea na wapiga kura kuwaeleza ni kwa nini wawachague. Haihitaji elimu kubwa sana kujua huyu ataniwakilisha vyema kama mambo mengine ya rushwa nk yakidhibitiwa.

Kinyume chake, mbunge anatunga sheria, anaishauri serikali, anajadili na kupitisha miradi mbalimbali, anajadili taarifa za kifedha na kuwasilisha kero za wananchi wake. Haya yote yanahitaji mtu makini na mwenye elimu na maarifa ya kiwango fulani.
Mh kwahiyo mtu wa la saba ana uwezo wa kuchambua atakachoambiwa sawasawa na mtu wa form four?
 
Ule ni uchaguzi tatizo mtu akimaliza chuo anajiona nafasi zote za kwake kuanzia kuajiliwa hadi kuchaguliwa .
Jiulizeni kwanini darasa la saba anamzidi kura msomi hayo ndio mambo ya kina Mwakyembe kujidai wana digrii nne lakini uwezo ni sifuri kwa kifupi hoja yako haina mashiko
 
Mh kwahiyo mtu wa la saba ana uwezo wa kuchambua atakachoambiwa sawasawa na mtu wa form four?
Nadhani ndiyo, kwa sababu sera binafsi za wagombea na za vyama katika ngazi ya jimbo zinajielekeza kwenye kutatua kero zinazowazunguka na kuwawezesha kunufaika na fursa zilizopo hivyo haihitaji kuwa na elimu kubwa kuyajua hayo kwa mwananchi sababu ni kitu anakiishi daily.

Kwa upande mwingine kama kwa wagombea tutaweka vigezo vya elimu, itarahisisha kuondoa 'vilaza' kwenye mchakato. Hivyo tutakuwa tunachagua 'safi' miongoni mwa 'safi' kuliko ilivyo sasa.
 
kama ni logic basi wote wenye logic tuwe wabunge,au sio. tatizo mmewabinya watu kutoa maoni yao tofauti na kuwa mbunge. kina msukuma wangeweza kutoa maoni yao kwenye media mikutano nk..lakini sio kuwa wabunge. mbunge ni lazima awe msomi. kingine hao kina Kabudi sio kwamba hawana uwezo bali wanaangalia chama hakitaki nini kwa hiyo na wao wanaonekana hawana tofauti na wasiosoma
Hivi ni uhutu gani wa habari umebinywa? Lissu kutafuta wadhamini tu anakusanya na kuhutubia mikutano ya hadhari na inaoneshwa na vyombo vya habari. Mnataka uhuru gani?
 
Ukimuangalia Mbunge kama Msukuma anawashinda wenzake wengi tu kuwawakilisha watanzani. Waulize wafanyabiashara na wachimbaji madini wadogo.

Yuko waziri mkuu mmoja alishawahi iongoza uingereza vizuri akiwa na vyeti mchundo.
 
Hahaha iko hivi, wasomi wanaogopa kujidhalilisha, wasiosoma hawana cha kupoteza.

Kama umesoma na unaogopa kushindwa kwanini usiongozwa na wasiosoma wasio ogopa kushindwa?!
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Siyo la saba tuu, Kuna kibajaji na Jah people hawakufika hata darasa la tatu lakini ni wabunge.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
N
Demokrasia Ni kuheshimu maamuzi ya wali wengi

Tanzania darasa la saba ndio walio wengi Huwezi wanyima haki Yao ya wao kuchagua mbunge miongoni mwao
Hatuangalii dunia tunaangalia walio wengi
Ndio maana Siasa Ni mchezo mchafu,na maamuzi mengi ya kisiasa ukiyaangalia Sana Ni maamuzi ya kijinga na machafu..Hebu wee fikiria(1)Wanasiasa/au Mbunge(hata Kama Ni STD 7),analipwa mishahara kwa Mwezi ambao Ni mkubwa mara dufu kuliko Daktari,mwalimu hata Kama Ni wa chuo kikuu.(2)Na Huyo mwanasiasa akimaliza miaka mi-5,pension yake Ni milioni 240 au zaidi.Mfanyakazi wa serikali atatumika zaidi ya 35 yrs kwenye utumishi LAKINI akistaafu,Pension take Ni kiduchu.(3)Viongozi WENGI wa kisiasa Ni wale ambao wameshachoka akili.maana WENGi wao utakuta Ni wastaafu sehemu mbalimbali(Wana umri zaidi ya 60yrs,Akili zimeshachoka Hiko walikotumika kwa miaka yoyote under 60yrs..Halafu huku kwenye Siasa ndo hao WENYE final say kwenye maisha yetU.KAMA SIO UJINGA NI NINI..Kuna haja ya kuangalia upya hizo sera na taratibu za kizamani ambazo Ni za kipuuzi.
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Kitu ambacho hakipo sawa ni mfumo wa elimu. Tofauti ya Form na Darasa la Saba ni lugha tuu
 
Sina Nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya Leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu mhimu Sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.
Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho Sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa Sasa. Tumebaki nyuma Sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Ukitoa vyote ulivyofundishwa darasani utabakiwa na akili, sasa wasomi wengi hasa wa sasa akili zao hazina effect kubwa katika jamii wao wanaishia tu kukwambia mwana filosofia mmoja wa Marekani alisema hivi,basi ni maneno maneno mengi mengi lakini c
Kwa maana ya usomi ni nini????? Mbona watanzania tunataka kuhalalisha ujinga kwa kiasi hiki?????

Usomi wa mtu unatakiwa kuwa nyakati zote na kwenye mazingira yote anayokuwa. Kusema nimuangalie akiwa nje ya siasa hapo sikubaliani na wewe!!! Ifike kipindi watanzania tuwe wakweli ili tuisadie kweli nchi yetu. Haiwezekani mtu akawa msomi wa madegree mengi alafu akawa haonyeshi huo usomi wake kwenye nafasi anazopata alafu tunachukulia poa tu!

Amini maneno yangu, class ya wasomi ya Tanzania ndo watu wajinga zaidi kuliko class ya watu ambao hawajasoma sana
Wengi wamekariri tu profesa fulani aliwahi kusema hivi! Huku wao wenyewe effect zao kwenye jamii hazionekani.
Ukitoa vyote ulivyofundishwa darasani utachobaki nacho ni akili na akili ndio were mwenyewe.



MAGUFULI4LIFE.
 
Mh kwahiyo mtu wa la saba ana uwezo wa kuchambua atakachoambiwa sawasawa na mtu wa form four?
Iko hivi swala lakuchambua hoja linaweza mshinda hata wa chuo kikuu mwenye ma PhD, linapokuja swala la kitaalamu tunawaachia wataalam,kuwa darasa la Sana sio kukosa akili najuwa na elimu ya juu sio ndokuwa na akili, kwani machifu walioongoza jamii wakusoma wapi? Tunafeli tunapoamini wasomi ndowanauwezo wakutuongoza, angalia mfano hapa kwetu wanaeongoza kusaini mikataba yakuinyonya nchi ni wasomi,wanaeongoza kusema uongo niwasomi,,wlietunga Sheria ya kuwa mbunge nilijua kusoma nakuandika tusiwabeze walikuwa namtazamo chanya,,
 
Basi ingekuwa wasomi Ni wajinga kuliko wasiosoma Hakuna nchi ingekuwa inahangaika na Elimu bali wangejikita na mambo mengine tu. Ki ufupi wewe Ni mjinga ambaye haupaswi hata kujibiwa.
Hivi elimu ni Nini?
 
Back
Top Bottom