Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Kwa Tanzania/Dunia ya leo Katiba kuruhusu Darasa la Saba kuwa Mbunge ni aibu kwa Taifa

Let's face it!
Yaani badala ya kususia uchaguzi na kusisitiza Tume Huru mnakuja kujificha huku na haya matumaini hewa!!??
 
Ni jambo jema kuwekwe ombwe la mtu wa kuteuliwa na chama flani ili awe mgombea wa ubunge kama wa kwanza kichukua fomu ni saba akija wa pili na form six huyu wa saba anakua ametoka na akija mwengine mwenye digree huyu wa form six nae atoke ili tupate mwenye elimu ya juu zaid kwenye jamii hii itasaidia watu wasome zaidi
 
Babu yangu amestaafu ualimu kwa miaka 30 anakula vumbi la chaki lakin amelipwa million 64,..

Lakin mbunge wa leo anaingia bungeni kulala kama akina wasila anaamka anakunywa maji hana mchango na bunge wala jimbo lake lakin kwa miaka mitano anapewa million 240, akitoboa miaka yote kumi bas atakuwa na million 480..

Tunawavunja moyo sana waalimu, ualimu sio wito tena.

[emoji25][emoji21][emoji29] REST IN PEACE BABU
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Hao darasa la saba ni CCM wote hivyo ni ngumu kubadili kitu chochote.
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Siyo hayo tu,mbunge ndo mtunga sheria,mpitia mikataba ya ndani na ya kimataifa,kusimamia serikali kupitia kamati za kibunge ,sasa fikiria darasa la saba ndo anapewa kazi hiyo si kituko
 
Iko hivi swala lakuchambua hoja linaweza mshinda hata wa chuo kikuu mwenye ma PhD, linapokuja swala la kitaalamu tunawaachia wataalam,kuwa darasa la Sana sio kukosa akili najuwa na elimu ya juu sio ndokuwa na akili, kwani machifu walioongoza jamii wakusoma wapi? Tunafeli tunapoamini wasomi ndowanauwezo wakutuongoza, angalia mfano hapa kwetu wanaeongoza kusaini mikataba yakuinyonya nchi ni wasomi,wanaeongoza kusema uongo niwasomi,,wlietunga Sheria ya kuwa mbunge nilijua kusoma nakuandika tusiwabeze walikuwa namtazamo chanya,,
Notice kwamba mimi hoja yangu haikua kusema hawa wagombea wawe wamesoma.

Umeniquote kunifafanulia kitu ambacho sijakisema.

Wasomi wametuingiza chaka na wasomi pia wametutoa kwenye chaka. Machifu walituongoza bila kusoma lakini ni wakina Chifu Mangungo ndiyo walisaini mikataba kituko.

Hoja nilizomaanisha hapo ni zile za mgombea mbele ya wapiga kura. Unadhani hilo linahitaji utaalamu? Mgombea akikuambia anakuhakikishia lishe bora huku kakuletea ubwabwa na kuku utamuita mtaalamu gani akuchambulie hilo?
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Hilo ni kweli kabisa; mbunge ni mtu anayetunga sheria za nchi ambazo zinaweza kufanya kazi kwa muda mrefu sana nchini, kwa hiyo anatakiwa awe na uelewa wa kusoma miswada na kuihoji. Mwaka jana tumewahi kujadiliana hapa kuhusu ujenzi wa uwanja wa ndege Chato, lakini ujenzi wa uwanja ule ulipitishwa kihalali na wabunge ambao hawakuweza kuhoji wakati bajeti inaletwa. Kwa kweli ni lazima sana kuhitaji kila mbinge awe na ama dipolma au digrii ya kwanza, yaani awe ni zaidi ya high School. Dunia ya sasa ina mambo mengi sana yanayohitajiwa kuchambuliwa kabla ya kuyatolea uamuzi, na uwezo wa wabunge wetu wengi katika uchambuzi ni mdogo sana. Kuna mbunge anaitwa Musukuma huwa anasimama bungeni kutoa pumba mara nyingi tu; lakini angalau yeye huwa annsimama na kuongea, na wakati mwingine hutoa michango mizuri. Ila kuna wabunge ambao kazi yao ni NDIYO na kupiga makofi tu wala hawachangii lolote bungeni kwa sababu hawajui linaloongelewa.
 
Kama Msukuma Kuna mda anakuwa na logic kuliko Kabudi, Lipumba na huyu utopolo Dr Abbas Kwa nini tusichague darasa la saba?????

Mleta mada!! Kwa taarifa yako Darasa la saba wengi ndo werevu kuliko hao wenye madegree! Hili ndo ajabu kuu la Tanzania!

Hivi wewe kati ya Mfanyabiashara wa madini Laizer na Mwakyembe wakiongea, Nani unamuelewa kwa haraka na vizuri????
Nonsense
 
Sina nia ya kuwadharau wale wenye elimu ya Darasa la Saba ila ninaandika haya kwa kuzingatia nafasi ya uwakilishi wa Jimbo na unyeti wa nafasi hii. Dunia/Tanzania ya leo siyo ile ya miaka ya 60s. Tunahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja zote ikiwemo katika nafasi za ubunge.

Mbunge ni mtu muhimu sana katika eneo analoliwakilisha na ndiyo maana anaheshimika na kulipwa mamilioni ya pesa kutoka na unyeti wa kazi anayoifanya au nafasi aliyonayo.

Mbunge anayeongoza Jimbo lenye kata 30 anakuwa na elimu ya Darasa la Saba, ila afisa mtendaji wa kata anayeongoza kata moja anatakiwa angalau awe na Diploma/shahada. Hiki Ni kichekesho sana na Tanzania inatakiwa tubadilike ili kuendana na uhalisia wa sasa. Tumebaki nyuma sana katika mambo mbalimbali likiwemo hili la kuwa na wawakilishi ambao uwezo wao na nafasi zao haviendani.
Darasa la 7 la miaka ya 60 lilikuwa la juu Middle School na lilikuwa pia Sekondari siyo Shule ya Msingi. Wanafunzi wa Chekechea mwaka 2020 anajua kusoma na kuandika na wanasema Kingereza au na Kifaransa lakini wa Darasa la Saba hajui kusoma wala kuandika kwa Kiswahili lughà yetu adhimu wala Kisukuma. Wabunge wa Darasa la 7 ni wa CCM tu wa ndiyoooo ndio maana Sheria zetu ni sheria za CCM.
 
T
Sasa kama la Saba ana logic kuliko graduate kwanini tusiseme sasa hao lasaba wanaweza kuwa walimu, au Afisa rasilimali watu au hata mgavi au mtakwimu?

Hoja ya kiwango fulani cha Elimu ndio inatakiwa itangulie hizo hekima na busara zako. Ukiona zina umuhimu basi zipeleka kwenye familia yako au biashara zako

Ubunge ni kitu cha kushindania miongoni mwa watu wengi mambeleko haya hayasaiidii.
Na hivi kweli std VII anaweza kuchambua taarifa za kitaalamu za CAG, fiscal arenas kwa muono mpana kwani critical and analysis yake ni ndogo ukilinganisha na nafasi anayoitaka.

Kama form four tu kwenye uaskali wanaanza kuonekana wanapwaya ile mbaya ije kuwa std VII tena ile kazi wanatumwa tu lakini uwezo hata wa kuitekeleza maamuzi unaanza kuwa mgumu kwasababu ya shule aliyosoma.

Hawa ilitakiwa waondolewe hata kwenye udiwani sema Chama chenye hakipo serious
tatizo ni mgombea darasa la saba au ni wapiga kura kuchagua darasa la saba?
 
Hivi hizo Sheria zinatungwa kwa lugha ya malkia alafu mbunge darasa la Saba hajui ht kutamka 1100 kwa kiswahili... Je hiyo Sheria ataijuaje zaidi tu ya kupitisha pasipo kupinga ili asiulizwe kasoro zilizomo...
Kama ni Tatizo naona lipo kwa waliomchagua!!
 
Hii ishu yaweza sound rahisi ila ni complicated kidogo. Demokrasia inasema kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Binafsi naona hata kuweka standards za elimu ni kumnyima mtu haki yake ya kidemokrasia.

Kama unaweka standards za mpigiwa kura tufanye ya kwamba na mtu yeyote aliyeishia la saba asipige kura pia. Maembe alisema "Pakiliwa kwa mwali na pa kungwi paliwe"
Sawa Sawa kwel ni complicated sio kidogo

NA kama kwel kila mtu Ana Haki ya kuchagua na kuchaguliwa kwann kwenye uraisi haiwezekani?

Au kwenye uraisi Kuna nini??
 
Hii ishu yaweza sound rahisi ila ni complicated kidogo. Demokrasia inasema kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Binafsi naona hata kuweka standards za elimu ni kumnyima mtu haki yake ya kidemokrasia.

Kama unaweka standards za mpigiwa kura tufanye ya kwamba na mtu yeyote aliyeishia la saba asipige kura pia. Maembe alisema "Pakiliwa kwa mwali na pa kungwi paliwe"

Mkuu huko ilikoanza demokrasia na waasisi wake lazima mtu na elimu ya juu ndiyo awe kiongozi, Kwahiyo sisi tunaoiga tumeboresha?
 
Sawa Sawa kwel ni complicated sio kidogo

NA kama kwel kila mtu Ana Haki ya kuchagua na kuchaguliwa kwann kwenye uraisi haiwezekani?

Au kwenye uraisi Kuna nini??
Hapa ndiyo hizo complications na kitu kinaitwa claw back clause kinapojitokeza.
 
Kwa maana ya usomi ni nini????? Mbona watanzania tunataka kuhalalisha ujinga kwa kiasi hiki?????

Usomi wa mtu unatakiwa kuwa nyakati zote na kwenye mazingira yote anayokuwa. Kusema nimuangalie akiwa nje ya siasa hapo sikubaliani na wewe!!! Ifike kipindi watanzania tuwe wakweli ili tuisadie kweli nchi yetu. Haiwezekani mtu akawa msomi wa madegree mengi alafu akawa haonyeshi huo usomi wake kwenye nafasi anazopata alafu tunachukulia poa tu!

Amini maneno yangu, class ya wasomi ya Tanzania ndo watu wajinga zaidi kuliko class ya watu ambao hawajasoma sana

Unaonaje huo mlinganisho wa mwajiriwa wa kata moja kitakiwa kuwa na kigezo cha juu cha elimu kuliko mbunge?

Je kwako nafasi ya ubunge na kuongoza kata ipi inahitaji vigezo vya elimu?
 
Mtendaji ameajiriwa na halmashauri,mbunge anachaguliwa na wananchi
Hujalazimishwa kumchagua wa Darasa la 7,pigia kura tu mwenye PhD
Kumbuka Mbunge ana uwezo wa kuajiri karibu mwenye Masters akawa na jukumu la kuchambua na kushauri juu ya nyaraka na Mambo mbali mbali
Mwakyembe amenisikitisha sana!

Basi ili lifanyike kisheria kwamba huyo mbunge wa darasa la saba lazima awe na wataalamu wenye ubobezi na elimu zaidi yake ili wamsaidie

Je hao wabunge wanafanya hivyo?
 
Kuelezea matatizo ya watu wako haihitaji degree. Kuna watu wanaitwa profesa na wamekuwa wanafanya ujinga. Vyeti sio kila kitu.
 
Hahaha jamani ubunge ni uwakilishi, makundi yote kwenye jamii yanahitaji kuwakilishwa.

Waacheni waende bungeni watuwakilishe.
 
Na hivi kweli std VII anaweza kuchambua taarifa za kitaalamu za CAG, fiscal arenas kwa muono mpana kwani critical and analysis yake ni ndogo ukilinganisha na nafasi anayoitaka.
Kipi cha kuchambua na unaletewa tu ripoti kuoneshwa mapesa yalotumika? Uchambuzi utafanywa na wenyewe wahasibu na wakaguzi kwenda kukagua marisiti. Mimi ukiniletea ripoti nikiona umetumia milioni 500 kwenye kutoa copy ndani ya mwezi nahitaji Elimu ya degree kujua kama hapo kuna ubadhirifu wa hela?

Sasa mwenye degree ya course tofauti na uhasibu ataweza kuchambua ripoti ya CAG? Au na yeye asigombee ubunge?
 
Mkuu huko ilikoanza demokrasia na waasisi wake lazima mtu na elimu ya juu ndiyo awe kiongozi, Kwahiyo sisi tunaoiga tumeboresha?
Elimu ya wapiga kura wao unaionaje? Tia maji tia maji kama hapa kwetu?
 
Back
Top Bottom