Kwa Utashi wangu binafsi, baada ya kuona Chuki zinazidi Kwake na Wahusika wamenyamaza namuombea Msamaha Hayati Rais Magufuli kwa Mapungufu yake

Kwa Utashi wangu binafsi, baada ya kuona Chuki zinazidi Kwake na Wahusika wamenyamaza namuombea Msamaha Hayati Rais Magufuli kwa Mapungufu yake

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kama Binadamu (Mwanadamu) tulivyo Mimi na Wewe hatujakamilika kama walivyo Watakatifu na Malaika wa Mbinguni.

Tokea Kifo chake GENTAMYCINE nimekuwa nikiona Lawama nyingi Kwake (Hayati Rais Dkt. Magufuli) kutokea humu Mitandaoni na hata katika Vichochoro (Vijiwe) ambavyo huwa najivinjari navyo 24/7.

Baada ya kuona Lawama, Chuki dhidi yake huku hata Wengine wakionyesha Furaha zao kwa Kifo chake nilidhani Kibusara tu basi Rais wa sasa Mama Samia au Chama Tawala chake (CCM) kingejitokeza Kwanza Kukiri Mapungufu yake au Matatizo aliyatengeneza ndani ya Tanzania yetu hii na Kiungwana kabisa Kuwaomba Radhi (Msamaha) wale Watanzania wote waliojeruhiwa au kuwa Wahanga wa Utawala wake.

Hivyo basi leo GENTAMYCINE kwa Utashi wangu binafsi (na hapa simlazimishi Mtu yoyote yule) nipo chini ya Miguu yenu nawaombeni TUMSAMEHE Hayati Rais Dkt. Magufuli kwa yale Mapungufu yake yote au kama aliwakwaza na kuwaumiza Watu kwa namna yoyote ile.

Kikubwa nawaombeni tu tumuombee Malazi mema ya Milele aliyonayo na Mwenyezi Mungu pia amsamehe Makosa yake ila liwe ni Fundisho kwa Viongozi (Watawala) Wengine waliobaki kuwa wasije Kuyarudia yale yale na kwa nimuonavyo Rais wa sasa Mama Samia sioni hata hiyo Chembe ya ama Kuumiza au Kuwakomoa Watu katika Uso wake na hata Moyoni mwake ( japo sina Darubini ) ya Kuuona upoje au unasemaje.

Naamini kabisa kuwa Marafiki wangu (JamiiForums Members) wote mtanielewa GENTAMYCINE na sasa mtashusha Jazba zenu Kwake na Kumsamehe kidhati kabisa Baba (Mzee) wa Watu kama hata Mimi pia nimemsamehe kwani kuna mahala alinivuruga (alinikera) kwa Utawala wake kwa mambo kadha wa kadha (hasa ya Kiutendaji) japo huko nyuma nilimpigania, nilimkubali na hata Kumtetea kwa kila aina hasa alopokuwa akipopolewa (akikosolewa) kila Kona nchini.

Tumsamehe, Tumsamehe na yaishe pia!
 
Hawezi kusamehewa kirahisi namna hiyo, tunahitaji mjadala wa kitaifa na utashi wa serikali kuwaomba watu radhi kwa maovu mengi yaliyofanywa na huyu mtu.

Kweli ameumiza wengi mno na kuna laana kubwa kwa nchi inatakiwa kufutwa kwa ridhaa ya wote walioumizwa na pia kwa ridhaa ya watanzania wote! Tuliumizwa!
 
Namna pekee ya kutufanya tumsamehe ni kuacha kumsifia kinafiki. Kwa vyovyote vile mtu akileta uzi wa kumpaka mafuta lazima tutamwagika kuzuia upotoshaji wowote.
 
Marehemu asemwi vibaya ila jiwe alipokufa watu mioyo yao ilishangilia.

Kufa wote tutakufa ila insue nani anatangulia?

Jiwe kanitesa binafsi ila nishamsamehe muda sana.

Tuseme Amina!!! wengine tuseme Inshaallah!!
Pole sana mkuu,,yule kiumbe hakuna ambae hajapitia madhila yake, nahisi yule hakuwa binadamu
 
Mwendazake safari yetu ya maisha aliifanya kuwa ni ya taabu Sana na mateso Tena KWA kipindi kifupi,alipotufikisha kimasafa palikuwa ni mbali ikatuchosha kufikiria kurudi,na tulivyovipoteza ni vingi hatuwez kuvihesabu,bora tuhesabu tulivyovibakiza
 
Kama Binadamu ( Mwanadamu ) tulivyo Mimi na Wewe hatujakamilika kama walivyo Watakatifu na Malaika wa Mbinguni.

Tokea Kifo chake GENTAMYCINE nimekuwa nikiona Lawama nyingi Kwake ( Hayati Rais Dkt. Magufuli ) kutokea humu Mitandaoni na hata katika Vichochoro ( Vijiwe ) ambavyo huwa najivinjari navyo 24/7.

Baada ya kuona Lawama, Chuki dhidi yake huku hata Wengine wakionyesha Furaha zao kwa Kifo chake nilidhani Kibusara tu basi Rais wa sasa Mama Samia au Chama Tawala chake ( CCM ) kingejitokeza Kwanza Kukiri Mapungufu yake au Matatizo aliyatengeneza ndani ya Tanzania yetu hii na Kiungwana kabisa Kuwaomba Radhi ( Msamaha ) wale Watanzania wote waliojeruhiwa au kuwa Wahanga wa Utawala wake.

Hivyo basi leo GENTAMYCINE kwa Utashi wangu binafsi ( na hapa simlazimishi Mtu yoyote yule ) nipo chini ya Miguu yenu nawaombeni TUMSAMEHE Hayati Rais Dkt. Magufuli kwa yale Mapungufu yake yote au kama aliwakwaza na kuwaumiza Watu kwa namna yoyote ile.

Kikubwa nawaombeni tu tumuombee Malazi mema ya Milele aliyonayo na Mwenyezi Mungu pia amsamehe Makosa yake ila liwe ni Fundisho kwa Viongozi ( Watawala ) Wengine waliobaki kuwa wasije Kuyarudia yale yale na kwa nimuonavyo Rais wa sasa Mama Samia sioni hata hiyo Chembe ya ama Kuumiza au Kuwakomoa Watu katika Uso wake na hata Moyoni mwake ( japo sina Darubini ) ya Kuuona upoje au unasemaje.

Naamini kabisa kuwa Marafiki wangu ( JamiiForums Members ) wote mtanielewa GENTAMYCINE na sasa mtashusha Jazba zenu Kwake na Kumsamehe kidhati kabisa Baba ( Mzee ) wa Watu kama hata Mimi pia nimemsamehe kwani kuna mahala alinivuruga ( alinikera ) kwa Utawala wake kwa mambo kadha wa kadha ( hasa ya Kiutendaji ) japo huko nyuma nilimpigania, nilimkubali na hata Kumtetea kwa kila aina hasa alopokuwa akipopolewa ( akikosolewa ) kila Kona nchini.

Tumsamehe, Tumsamehe na yaishe pia!!
Kama ulikuwa haujamsamehe ni shida yako tuu. Tangu day one mpaka 21, watanzania tulimlilia kwa kujipiga vifuani kwa kumuomba mwenyezi mungu amasamehe yale yote ambayo alitenda kwa bahati mbaya au makusudi ila kwa lengo la kuinyosha nchi. Kati ya watanzania mil60 na hao wa vijiweni kwako wasiozidi watu50 haina athari hata kwa mwenyezi mungu. Mwenyezi mungu mwenyewe ni Baba wa Vita ana wapigania watu wake, na hata aliruhusu watu wauwawe kwa sababu ya kukiuka matakwa yeke. So, HAYATI JEMEDARI JPM pumzika kwa amani, watz tutazidi kukuombea hadi mwisho wa dahali.
 
Back
Top Bottom