Kwa uzalendo alionao, James Mbatia anastahili kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungebi

Kwa uzalendo alionao, James Mbatia anastahili kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungebi

Kwa uzalendo alionao kiongozi wa NCCR Mageuzi ni dhahiri kuwa anastahili kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.
Huyu jamaa kwenye masuala yanayohusu manufaa ya taifa letu hana utengano kama wale jamaa wanaotumiwa na mabeberu. Maana duniani pote nchi inapokuwa kwenye vita lazima raia wote muwe na umoja na kushirikiana.

Kama sasa taifa letu lipo kwenye majanga alafu wafuasi na Wanachama wa Chadema pamoja na viongozi wao ni kuhamasisha watu wasiwe na umoja na kuongeza hofu kwa wananchi,hii inaonyesha ni namna gani hiki chama hakifai kabisa hata kuwepo.

Wanachama na viongozi wa Chadema muda wote wamekuwa wakitaka mifarakano tu hata kama taifa lipo katika janga ambalo linahitaji umoja ili kulidhibiti. Wanasambaza habari ambazo zinatia hofu wananchi na kuleta hali ya taharuki.

Lakini James Mbatia na chama chake chenye slogan nzuri ya Udugu hana mambo kama haya ambayo hayastahili kabisa kufanywa na watu wenye akili timamu hasa kwenye kipindi kama hichi. Na kwa mantiki hii huyu jamaa huu ndio muda muafaka kujipanga ili aje kuchukua hii nafasi maana uzalendo kipimo kikubwa cha kuweza kumwamini mwanasiasa makini.
Asikanyage maeneo yoyote ya Moshi kuanzia leo msaliti mkubwa.
 
Back
Top Bottom