Kwa vijana ni wachache sana, ila wazee wetu wengi waliweza

Kwa vijana ni wachache sana, ila wazee wetu wengi waliweza

Wazee zamani walioa wanawake hata 6, na bado mtaani ana vibinti kadhaa, lakini wake zake hakuna aliyefungua mdomo kusema chochote walimtunzia "siri" mume wao japo watu wa nje wanajua lkn sio kwa kusikia kutoka kwa wake zake....tofauti ya sasa ni kwamba Wanawake wengi sio wavumilivu na wengi huongea wazi mambo ya ndani ya mume/mpenzi kitu ambacho sio sawa...
 
Mi naweza afiki siamini kama tabia asili za mwanaume zimebadilika sana ila kilichopo sasa na kufanya mambo yawe hadharani sana ni teknolojia.

Huwezi kwepa matumizi ya simu maana ndio njia nyepesi ya kuwasiliana na hawara wako, mbaya zaidi mfumo jike ndio umetawala sana zama hizi mambo ya haki sawa hivyo mkeo akijua unachepuka aidha kakuta unaongea na simu na malaya wako au chats ili muende sawa nae anatafuta kolo yoyote anaruka nae!

Shida ukijua nae kakulipizia unaumia kufa, girls weren't meant to overpower us!

What you are saying so true aisee. Haki sawa na technology hasa simu nilitoa moja ya sababu kubwa kwa sasa kufanya watu wengi wachepuke mkuu.

Nakubaliana nawe.
 
Wazee zamani walioa wanawake hata 6, na bado mtaani ana vibinti kadhaa, lakini wake zake hakuna aliyefungua mdomo kusema chochote walimtunzia "siri" mume wao japo watu wa nje wanajua lkn sio kwa kusikia kutoka kwa wake zake....tofauti ya sasa ni kwamba Wanawake wengi sio wavumilivu na wengi huongea wazi mambo ya ndani ya mume/mpenzi kitu ambacho sio sawa...

Ni kweli mkuu uvumilivu walikuwa nao sana wazee wetu ukilinganisha na sasa. Na hata ukiangalia zamani ilikuwa kama mzee ana wake hata kama ni wawili au watatujulisha waliweza kuishi kama ndugu kwa upendo, furaha na amani ya hali ya juu tofauti na sasa hivi.

Walivumiliana kwa kila hali mkuu. True talk.
 
zamani sio ya kuiongelea hata, kidogo, tena uchepukaji wake ulikuwa wa kibabe, mtemi anakuja we unatoka unamuacha ndani na mkeo, anafanya anachojua yeye huko ndani we unakaa nje unaskilizia, akitoka hapo anaingia nyumba inayofuata, yaani kijiji kizima wake zenu ni wake zake akiwahitaji...mambo gani sasa ukizingatia zawani chupi ilikuwa hamna watu walimalizana sana kwenye makorongo, visimani, shamba huko, kwanza mnazungumzia zamani gani maana labda sijaelewa vizuri, kama ni zamani ile mgeni wa kimasai akija kwako achomeka mkuki nje ili mwenye nyumba ukija uje kuna njemba ipo ndani, aisee zamani ile wachepukaji walikuwa wababe kuliko sasa

Hahahaha, ila unajua mkuu wazee wetu hawakuwa Kama kuku coz kuku hata umuwekee gunia zima hapo chini still atapekua pekua chini zaidi kuona kuna nini.

Tofauti na wazee wetu hata kama ilikuwa ameshaaga na akakosa gari kwa bahati mbaya atamtuma hata mtoto apeleke begi yee anaenda kwenye kijiwe cha kahawa, karata, draft, bao etc

Walijua jinsi ya ku-treat wake zao kuepusha kila kitu ambacho kingekwaza mapenzi yao ila kwa sasa watu wanatafuta kabisa makosa that's why uvumilivu unakuwa mdogo hatimaye wengi wanaharibu mahusiano.
 
Ningepata mwanamke wa dizain iyo ningemshkilia maisha yangu yote
 
Sisi tulioa kwa kuangalia tabia, wajukuu wanaoa kwa kuangalia sura na chura.... na wale wa jinsia ya pili wanaangalia maslahi

Hekima na Busara za babu hutazamwa kwa mawazo yake tu.

Asante Babu. 100%T.
 
Ningepata mwanamke wa dizain iyo ningemshkilia maisha yangu yote

Mbona wapo mkuu. Fuata busara za Babu hapo juu kiongozi.

You will never go wrong.
 
Kuna vijana huwa wanajipa moyo... Anajua kabisa anaoa/olewa na kimeo... ila utasikia "nitajitahidi kumbadilisha" ... Akisahau kuwa binadamu hafugwi kama mifugo.

Ukitaka starehe tafuta malaya, ukitaka kuoa tafuta mke.

100%T.
 
Kuna vijana huwa wanajipa moyo... Anajua kabisa anaoa/olewa na kimeo... ila utasikia "nitajitahidi kumbadilisha" ... Akisahau kuwa binadamu hafugwi kama mifugo.

Ukitaka starehe tafuta malaya, ukitaka kuoa tafuta mke.
Mmmh
 
Zamani walikuwa wakichepuka sana na mume akitaka kukuolea mke wa pili we ndo unatandika kitanda na kumuhudumia huyo bi mdogo sema ss kina mama tumejua haki zetu hatuambiwi kitu. Na wamama walikuwa wakichepuka ndo maana walikuwa wakizaa watoto wengi kumbe kati ya wale 2 ni wa familia anayodhani huwa wana akili za darasani, 2 wa mzee mwenye hela mtaani (kwamba kuna mkondo wa utajiri) 1 wa mwenyekiti (anafata mkondo wa uongozi) na wengine wa mzee rafiki na mumewe aliyeonyesha kuwajali wakati baba kaenda kutumika shamba la mkonge. Na maradhi kulikuwa hamna sasa hivi chepuka uone maradhi yatavyokuumbua!!! Gono, HIV, UTI
 
Back
Top Bottom