Kwa vile Israel imekubali yaishe; je, kuna umuhimu kuonewa huruma ili dunia ipate nafuu?

Kwa vile Israel imekubali yaishe; je, kuna umuhimu kuonewa huruma ili dunia ipate nafuu?

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Matukio ya jana jimboni Gaza na kauli kutoka Marekani na Israel ni wazi kuwa mbabe mkubwa amekubali kistaarabu ili yaishe.

Shinikizo la kuondoa askari Gaza si la Benjamin Netanyahu kwa ridhaa yake bali limetokana na ukweli aina tofauti katika uwanja wa vita.

Ukweli wa mwanzo ni kuwa hali ya uchumi wa Israel imekuwa mbaya na tishio la Marekani kuzuia misaada liko wazi sana kutokana na majukumu yaliyolielemea taifa hilo,ikichangiwa na jeuri ya Netanyahu kupingana na kujibizana na raisi Biden.

Ukweli wa pili ni kuwa Israel imeona kuwa malengo yake hayana dalili ya kutimia, ambayo yalikuwa ni kuokoa mateka na kuwasambaratisha Hamas na wenzao ili wasiweze tena kutawala jimboni humo.

Na mwisho kama ilivyoelezwa na washirika hao ni kuwa wanajeshi wamechoka kupigana bila kuona matokeo mbali na kuua watu ovyo na wengi kutaka wapumzike.Katika hali kama hiyo kuwalazimisha kupigana na kuendelea kubaki mbali na familia zao ni hatari zaidi na mwishowe wanaweza kuasi kwa mpigo jambo ambalo limeshaanza kwa hatua za awali.

Kauli kwamba brigedia moja imeachwa kuangalia watu wasirudi kaskazini ni kauli ya kujitoa kimaso maso kwani hiyo hiyo jana mamia ya watu wamerudi makwao na bila vikwazo.Kwa upande mwengine si rahisi kwa askari waliobaki kumudu wimbi la watu kutaka kurudi majumbani mwao wakati ambapo waliweza kupenya hata kabla ya tukio hili la kuondoshwa brigedia zilizokuwa zikipiga kwa nguvu.

Baada ya yote hayo suala muhimu, ni je kuna umuhimu wa Israel baada ya uovu wao huo ihurumiwe na wapinzao wao kama vile Houth na Hezbollah.

Je, Hamas wawaachie mateka warudi makwao na Hizbullah iache kurusha makombora kaskazini ya Israel ili waisrael wanaoishi kwenye mahoteli ya kulipiwa nao warudi makwao.

Na je, Houth waache kushambulia meli na kurusha maroketi kusini ya Israel. Mara baada ya tangazo la Israel kurudisha nyuma askari tayari bei ya mafuta duniani imeshuka kidogo.
 
Akili huna, unaongea kishabiki ukiwa Matumbi, ungekuwa Gaza ndio ungejua uhalisia, hali ni mbaya kuliko unayoandika, magaidi yameteketezwa hadi ardhini, wewe akili huna
 
  • Thanks
Reactions: 511
Akili huna, unaongea kishabiki ukiwa Matumbi, ungekuwa Gaza ndio ungejua uhalisia, hali ni mbaya kuliko unayoandika, magaidi yameteketezwa hadi ardhini, wewe akili huna
Najua sana hali ilivyo huko.Watu wameuliwa sana na hata aliyeuwa amechoka kuua bila kutimiza hata lengo moja.
Muhimu wamechoka na wameamua kurudi nyumbani hatua kwa hatua.Huo ni ushindi mkubwa kwa Hamas na watu wote wapenda haki duniani.
 
Matukio ya jana jimboni Gaza na kauli kutoka Marekani na Israel ni wazi kuwa mbabe mkubwa amekubali kistaarabu ili yaishe.

Shinikizo la kuondoa askari Gaza si la Benjamin Netanyahu kwa ridhaa yake bali limetokana na ukweli aina tofauti katika uwanja wa vita.

Ukweli wa mwanzo ni kuwa hali ya uchumi wa Israel imekuwa mbaya na tishio la Marekani kuzuia misaada liko wazi sana kutokana na majukumu yaliyolielemea taifa hilo,ikichangiwa na jeuri ya Netanyahu kupingana na kujibizana na raisi Biden.

Ukweli wa pili ni kuwa Israel imeona kuwa malengo yake hayana dalili ya kutimia, ambayo yalikuwa ni kuokoa mateka na kuwasambaratisha Hamas na wenzao ili wasiweze tena kutawala jimboni humo.

Na mwisho kama ilivyoelezwa na washirika hao ni kuwa wanajeshi wamechoka kupigana bila kuona matokeo mbali na kuua watu ovyo na wengi kutaka wapumzike.Katika hali kama hiyo kuwalazimisha kupigana na kuendelea kubaki mbali na familia zao ni hatari zaidi na mwishowe wanaweza kuasi kwa mpigo jambo ambalo limeshaanza kwa hatua za awali.

Kauli kwamba brigedia moja imeachwa kuangalia watu wasirudi kaskazini ni kauli ya kujitoa kimaso maso kwani hiyo hiyo jana mamia ya watu wamerudi makwao na bila vikwazo.Kwa upande mwengine si rahisi kwa askari waliobaki kumudu wimbi la watu kutaka kurudi majumbani mwao wakati ambapo waliweza kupenya hata kabla ya tukio hili la kuondoshwa brigedia zilizokuwa zikipiga kwa nguvu.

Baada ya yote hayo suala muhimu,Ni jee kuna umuhimu wa Israel baada ya uovu wao huo ihurumiwe na wapinzao wao kama vile Houth na Hezbollah.

Jee Hamas wawaachie mateka warudi makwao na Hizbullah iache kurusha makombora kaskazini ya Israel ili waisrael wanaoishi kwenye mahoteli ya kulipiwa nao warudi makwao.

Na jee Houth waache kushambulia meli na kurusha maroketi kusini ya Israel.Mara baada ya tangazo la Israel kurudisha nyuma askari tayari bei ya mafuta duniani imeshuka kidogo
Umepofushwa na udini hadi unashabikia upuuzi. Israel wakiwachapa unapiga kelele eti ooh wanauwa watoto na akina mama. Wakipozi kidogo utasikia ooh wamewaogopa Hamas. Hovyo sana wewe mujahidina.
 
Umepofushwa na udini hadi unashabikia upuuzi. Israel wakiwachapa unapiga kelele eti ooh wanauwa watoto na akina mama. Wakipozi kidogo utasikia ooh wamewaogopa Hamas. Hovyo sana wewe mujahidina.
Wala hakuna udini hapo.Kule Marekani wanaoimba kifo kwa Marekani na Israel na wanaimba hivyo wala si mujahidina.
Hao ni watu wenye akili na wapenda haki.
 
Upuuzi kwa vile nimesema Israel imerudisha majeshi nyuma.
Mimi sihusiki na maamuzi hayo japo nayafurahia sana.
Nyinyi mlioshitushwa nayo ndio mumekasirika sana.
Pumba zako zinakera
 
Najua sana hali ilivyo huko.Watu wameuliwa sana na hata aliyeuwa amechoka kuua bila kutimiza hata lengo moja.
Muhimu wamechoka na wameamua kurudi nyumbani hatua kwa hatua.Huo ni ushindi mkubwa kwa Hamas na watu wote wapenda haki duniani.


Hivi kichwa umebeba tu, kumbe empty brain unaongea, huna kitu ndani, hadi vita vinaanza nani alianza kuua mwenzake? Nani alianza kuvamia na kuua raia wa Israel na mataifa mengi wakiwa katika sherehe yao? Nani? Hadi mtanzania kauawa na Hamas, tena vita ilikuwa hakuna, hivi umejitoa akili kabisa wewe? Hamas ni magaidi pumbaf sana, inafaa waangamizwe kabisa hata mmoja asibaki, ni kuwa hujui kabisa hata chanzo za vita hivi wewe, uko kama kichaa tu unaandika, of course you have mental disorder, but huponi hata kujua ukweli, vita havianzi tu kuna sababu, hata sababu hujui, wewe kichaa kabisa.
 
  • Kicheko
Reactions: 511
Back
Top Bottom