Kwa wale mnaokuja kula Christmas vijijini, zingatieni yafuatayo

Kwa wale mnaokuja kula Christmas vijijini, zingatieni yafuatayo

Nelson Kileo

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2011
Posts
3,053
Reaction score
3,259
1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 12 jioni baada ya kutoka shamba, acheni shobo.

2. Mje na dada wa kazi huku hakuna mtu wa kubeba mtoto wako anaye deka-deka.

3. Hakuna kuchotewa maji ya kuoga, ndoo ya maji kutoka Bomba la nje mtabeba wenyewe.

4. Mje na midoli ya kuchezea watoto wenu wasije kutunyongea vifaranga.

5. Hakuna kuchinjiwa kuku hadi siku ya christmas.

6. Ukimaliza kuoga toka na sabuni kwa sababu hiyo hiyo ndiyo tunaoshea vyombo.

7. Ukija na mke au mume wako asianze kusema mboga hii akila anaumwa tumbo sisi tunakujua tangu ulivyokuwa mdogo ulikuwa unakula makande au viazi chukuchuku na haukuwahi kuumwa tumbo kwa hiyo mtakula chochote kitakachopikwa.

8. Huku hakuna kumbembeleza mtoto wakati wa kula akikataa kula sisi tunakula na tunamaliza.

9. Usiku hakuna kumulikiwa tundu la choo unapapasa na mguu tu.

10. Hakuna Kutupa ugali au wali uliolala huo ni mkate wetu asubuhi.

11. Hakuna mto wa kulalia huku unalalia mikono kwa kukunja ngumi.

12. La mwisho wale mliopo kwenye ajira zaidi ya miaka 10 na huku nyumbani hamjajenga mtakuwa mnalala kwa mwenyekiti wa Kitongoji/Kijiji.

Ahsanteni na karibuni sana 🙏🙏
 
1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 12 jioni baada ya kutoka shamba, acheni shobo.

2. Mje na dada wa kazi huku hakuna mtu wa kubeba mtoto wako anaye deka-deka.

3. Hakuna kuchotewa maji ya kuoga, ndoo ya maji kutoka Bomba la nje mtabeba wenyewe.

4. Mje na midoli ya kuchezea watoto wenu wasije kutunyongea vifaranga.

5. Hakuna kuchinjiwa kuku hadi siku ya christmas.

6. Ukimaliza kuoga toka na sabuni kwa sababu hiyo hiyo ndiyo tunaoshea vyombo.

7. Ukija na mke au mume wako asianze kusema mboga hii akila anaumwa tumbo sisi tunakujua tangu ulivyokuwa mdogo ulikuwa unakula makande au viazi chukuchuku na haukuwahi kuumwa tumbo kwa hiyo mtakula chochote kitakachopikwa.

8. Huku hakuna kumbembeleza mtoto wakati wa kula akikataa kula sisi tunakula na tunamaliza.

9. Usiku hakuna kumulikiwa tundu la choo unapapasa na mguu tu.

10. Hakuna Kutupa ugali au wali uliolala huo ni mkate wetu asubuhi.

11. Hakuna mto wa kulalia huku unalalia mikono kwa kukunja ngumi.

12. La mwisho wale mliopo kwenye ajira zaidi ya miaka 10 na huku nyumbani hamjajenga mtakuwa mnalala kwa mwenyekiti wa Kitongoji/Kijiji.

Ahsanteni na karibuni sana 🙏🙏
Wakumbuke kununua helmet za kutosha hukohuko mjini
 
Sasa kijijini tv ya nini wameangalia sana
Hao wapeni baiskeli wakazunguke nazo tu au wakawinde
Kijijini raha yake unajizima kila kitu na unaenda na maisha ya huko
Kijijini raha sana
 
Ila hili la sabuni moja kuogea na kuoshea vyombo limekaaje mkuu, maana hata ukitoka msalani unanawia mikono hiyohiyo, ila sio mbaya mi nadhani bana sabuni haitunzi bakteria 😅
 
Vijiji miaka ya 1980s na 1990s kurudi nyuma ndio ilikuwa vijiji, watu wanafua toni na kuanika nguo juu ya mawe kula wali hadi sikukuu, vijiji vya sasa vingi vimeendelea kuna huduma kama mijini tu,
 
Kijiji gani hicho bado wanaishi maisha ya kizamani mpaka sasa, mbona maisha ni changanyikeni mijini na vijijini? Kuna nyumba kali vijijini, maji ya bomba, umeme, misosi kama ya mijini tu. Bushi kwetu niliondoka niliacha chaka lakini leo hii ni kama mjini nilienda nikashindwa kuishi maisha ya kizamani, kula misosi ya kizamani, kulalia ngozi za ngombe/mbuzi, hakuna tofauti na mjini labda majengo mengi tu
 
13. Huku tunalalia vilago , so hakuna kulalamika asubh mbavu zinakuuma, kama mnataka mtununulie godoro mkija mtumie
 
Pia huku kijijini ndipo yupo jamaa aliyemtoa bikra mkeo kwahy usijichoreshe kwa wanakijiji wakati mbabe wako yupo.
 
Back
Top Bottom