Kwa wale mnaokuja kula Christmas vijijini, zingatieni yafuatayo

Kwa wale mnaokuja kula Christmas vijijini, zingatieni yafuatayo

1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 12 jioni baada ya kutoka shamba, acheni shobo...
Huyu unayemzungumzia hapa ni mtu choka mbaya sana ambaye kiuhalisia hata nauli ya kuja huko kijijini hana hamtamuona.

Ukiwa na salio mambo yote unayosema hayawezekani kufanyiwa yatafanywa labda hicho kijiji kiwe cha wachawi wenye husda na maendeleo ya watu.

Wenzio tukienda kijijini tunapokewa kama wafalme ni mwendo wa vyuku mpaka tunaondoka. Na sababu kubwa ni kuwa tunawakumbuka kwa kugawa upendo hata kabla ya kwenda. Na siku tukienda tunahakikisha tumechenji 100K kwa ajili ya kugawa upendo buku mbilimbli kwa majirani na wanaukoo, kwa wanaukoo wa karibu pamoja na walio familia moja na wazazi wanakula 5k au 10K. Kjijini hawana baya wala makuu.

Kijijini siku hizi tunaenda tuko full ili watoto wetu wasielemee wazazi au ndugu. Ndugu wanafurahia uwepo wetu. Kila la heri mzee
 
Wapendwa waishio mijini, tunayo furaha kuwakaribisha nyumbani kwa ajili ya kusherehekea Krismasi. Lakini kabla hamjakanyaga ardhi ya kijiji, tafadhali zingatieni mambo haya muhimu ili kujiepusha na migogoro isiyohitajika:

1. TV ZA KIJIJINI:
Ndiyo, tuna TV. Lakini sahau kuhusu "Netflix and chill." Huku ni "TBC and patience." Na hata hiyo TV haijawashwa mchana, inangoja saa mbili usiku, baada ya mbuzi kurudi zizini na watoto kulala.

2. HATUNA WAFANYAKAZI WA NDANI:
Hii sio mjengo wa mtaa wa Mbezi. Kama umezoea kubebwa mabegi na kufanyiwa kila kitu, basi njoo na huyo dada wa kazi wako. Huku hakuna mtu wa kubeba watoto wako wala kukuambia, "Chai yako iko tayari."

3. MTONI NI GYM YA KILA MTU:
Kama unaogopa kuchota maji, ni bora ubaki mjini. Huku unachukua ndoo yako mwenyewe, unashuka mtoni, na unajifunza uzalendo wa kufua nguo ukitumia mawe.

4. VIFARANGA SIO MIDOLI:
Kama watoto wako hawana midoli, tafadhali wape. Huku vifaranga hawana nguvu za kujitetea. Tumeshaona vifaranga wakinyongwa kwa kamba za viatu wakibadilishwa kuwa "midoli."

5. KUKU WA KRISMASI:
Kuku wetu sio wa kuchinjwa kabla ya tarehe 25. Ukisikia harufu ya kuku mapema, basi jua ni ndoto yako tu. Tuna sheria za kidini kuhusu siku za kuchinja.

6. SABUNI ZA MULTIPURPOSE:
Usijali kuhusu "Omo" au "Sunlight." Sabuni ya kuogea ndiyo hiyo hiyo ya kufulia na kuoshea vyombo. Ukimaliza kuoga, acha sabuni ikauke vizuri kwa matumizi mengine.

7. MKE/MUME MSONYO:
Tafadhali mwambie mke/mume wako kuwa huku "Tumbo linauma" sio kisingizio. Ulivyokuwa mdogo ulikula hata maembe yenye ukungu na hukuwahi kulalamika. Kwa hiyo chochote kitakachopikwa, kinashuka tumboni bila mjadala.

8. WATOTO WAKATAA KULA:
Huku hakuna drama za kumbembeleza mtoto. Akikataa kula, basi chakula hakilali. Sisi tunakula hadi kisahani kinang'aa.

9. CHOO CHA USIKU:
Huku tunaitwa wapiga ramli wa kitaalamu. Tundu la choo halimulikiwi, unapapasa tu kwa mguu mpaka ulifikie. Hakuna "torch" wala "flashlight."

10. UGALI ULIOPUMZIKA:
Ugali wa jana sio chakula kilichoharibika. Ni "mkate wa kijiji." Usishangae tukiamka na kuunga chai na ugali uliolala. Ni utamaduni!

11. MITO YA ASILI:
Sahau kuhusu mito ya masponji yenye 'memory foam.' Huku mikono yako ndio mto wa kitaifa. Tunaita "biceps comfort."

12. WAJENZI WA NDOTO:
Ukiwa na zaidi ya miaka 10 kwenye ajira na bado hujajenga kijijini, nafasi yako ni kwa mwenyekiti. Hatuwezi kukuandalia malazi huku hata tembe moja hujajenga.

Tunaomba mzingatie haya yote. Siku ya Krismasi siyo tu sherehe, bali ni mafunzo ya kurudi kwenye asili! Karibuni sana, lakini mjue, vijijini ni shule ya maisha.

AHASANTENI NA HERI YA KRISMASI!
 
Wapendwa waishio mijini, tunayo furaha kuwakaribisha nyumbani kwa ajili ya kusherehekea Krismasi. Lakini kabla hamjakanyaga ardhi ya kijiji, tafadhali zingatieni mambo haya muhimu ili kujiepusha na migogoro isiyohitajika...
Dah mleta mada huu Uzi umesimama kucha😂😂😂umewapania
 
1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 12 jioni baada ya kutoka shamba, acheni shobo.

2. Mje na dada wa kazi huku hakuna mtu wa kubeba mtoto wako anaye deka-deka.

3. Hakuna kuchotewa maji ya kuoga, ndoo ya maji kutoka Bomba la nje mtabeba wenyewe.

4. Mje na midoli ya kuchezea watoto wenu wasije kutunyongea vifaranga.

5. Hakuna kuchinjiwa kuku hadi siku ya christmas.

6. Ukimaliza kuoga toka na sabuni kwa sababu hiyo hiyo ndiyo tunaoshea vyombo.

7. Ukija na mke au mume wako asianze kusema mboga hii akila anaumwa tumbo sisi tunakujua tangu ulivyokuwa mdogo ulikuwa unakula makande au viazi chukuchuku na haukuwahi kuumwa tumbo kwa hiyo mtakula chochote kitakachopikwa.

8. Huku hakuna kumbembeleza mtoto wakati wa kula akikataa kula sisi tunakula na tunamaliza.

9. Usiku hakuna kumulikiwa tundu la choo unapapasa na mguu tu.

10. Hakuna Kutupa ugali au wali uliolala huo ni mkate wetu asubuhi.

11. Hakuna mto wa kulalia huku unalalia mikono kwa kukunja ngumi.

12. La mwisho wale mliopo kwenye ajira zaidi ya miaka 10 na huku nyumbani hamjajenga mtakuwa mnalala kwa mwenyekiti wa Kitongoji/Kijiji.

Ahsanteni na karibuni sana 🙏🙏
Tuambie hapo wapi penye watu wakarimu viwango hivyo tujisogeze kula krismass.
 
1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 12 jioni baada ya kutoka shamba, acheni shobo.

2. Mje na dada wa kazi huku hakuna mtu wa kubeba mtoto wako anaye deka-deka.

3. Hakuna kuchotewa maji ya kuoga, ndoo ya maji kutoka Bomba la nje mtabeba wenyewe.

4. Mje na midoli ya kuchezea watoto wenu wasije kutunyongea vifaranga.

5. Hakuna kuchinjiwa kuku hadi siku ya christmas.

6. Ukimaliza kuoga toka na sabuni kwa sababu hiyo hiyo ndiyo tunaoshea vyombo.

7. Ukija na mke au mume wako asianze kusema mboga hii akila anaumwa tumbo sisi tunakujua tangu ulivyokuwa mdogo ulikuwa unakula makande au viazi chukuchuku na haukuwahi kuumwa tumbo kwa hiyo mtakula chochote kitakachopikwa.

8. Huku hakuna kumbembeleza mtoto wakati wa kula akikataa kula sisi tunakula na tunamaliza.

9. Usiku hakuna kumulikiwa tundu la choo unapapasa na mguu tu.

10. Hakuna Kutupa ugali au wali uliolala huo ni mkate wetu asubuhi.

11. Hakuna mto wa kulalia huku unalalia mikono kwa kukunja ngumi.

12. La mwisho wale mliopo kwenye ajira zaidi ya miaka 10 na huku nyumbani hamjajenga mtakuwa mnalala kwa mwenyekiti wa Kitongoji/Kijiji.

Ahsanteni na karibuni sana 🙏🙏
6,7 na 12 wasome na wakuelewee sanaaaa
 
Back
Top Bottom