Kwa wale tunaofuatilia Masuala ya Kijeshi kimataifa naomba ufafanuzi wa hili

Kwa wale tunaofuatilia Masuala ya Kijeshi kimataifa naomba ufafanuzi wa hili

Jeshi la Marekani lina branch kuu sita, ya mwisho ilianzishwa kipindi cha Trump kama sikosei.
1. US Army
2. Marine Corps
3. Navy
4. Air Force
5. Coast Guard
6. Space Force

Kuna branches zinafanana kidogo mfano US Navy na US Coast Guard zinaelekeana ila hazifanyi kazi sawa. Ingawa ukiivamia Marekani zitashirikiana, ila mfano kupigana vita mbali sijui Yemen na Taiwan hutowaona Coast Guard. Na kwenye kupambana na narcos pwani zile sijui Miami hutowaona US Navy bali DCEA wataomba assist kwa Coast Guard. Hata silaha zao ni tofauti, Coast Guard wana meli zina rangi nyeupe na nyekundu, ni meli nyepesi.

Space Force ni ndogo sana. Hizo nne za mwanzo zina uwezo wa kujitegemea kivyake kwa kiasi fulani kwenye silaha, special forces na misheni.
US Army ina jeshi lake lenyewe la anga (USAAF) hivyo haihitaji kuwaita Airforce (USAF) kwenye mission yake.
Wakati huo jeshi la maji (US Navy) lina jeshi lake la anga (Naval Air Force) ambalo hili lina idadi kubwa ya ndege kuliko ndege zote za Urusi. Ndege kama F/A-18 Super Hornet ni fightet ila inatumiwa na Navy tu, Airforce haitumii. US Navy ina jeshi lake la ardhini, US Marine Corps
Marekani inaifanya Marine Corps ni branch ya jeshi iliyo independent (kati ya 6), ila iliyo tawi la branch nyingine (Navy). Na huwa wana silaha tofauti kama bunduki, armour na weapons systems. Mfano F-35 kuna A ya Airforce, B ya Marines na C ya Navy.

Marine Corps wanaendesha zile amphibious landing crafts na hovercrafts. **** Wana missions ngumu na ndio hufa sana vitani, alafu ndio wa kwanza kutangulia kufungua njia kwenye battlefield ya mbali. Na wana mafunzo makubwa zaidi na uzoefu mzuri. Na huwa wanachukuliwa kwingineko hawaanzii Marine Corps.
*** Ndio maana wanapewa kazi za haraka zenye ugumu. Wako easily deployable na hawatumii muda mrefu kufundishwa mazingira ya ugeni.
Mwanzoni nilisema kila branch kati ya zile nne inaweza jitegemea kiasi, sasa kila branch ina special force yake. Special forces wa Navy ni SEALs (hawa wanapiga popote), wa Marines wanaitwa Raiders (hawa sanasana wanapiga Pwani kwenye mwambao tu).
Hivyo badala watumie Raiders, wanatumia SEALs. Kwanini hawatumii soecial forces za Army kama Green Berets?
Sababu Green Berets wao huwa ni special force ya muda mrefu na malengo mengi. Ukisikia jeshi la Marekani limewafundisha XXX ujue waliofundisha ni Green Berets. SEALs ni kufanya kazi ya malengo ya muda mfupi kama kuua Osama bin Laden.

Kwenye vita Raiders watavia fukwe wafe sana wafungue beachheads, SEALs watafuata wafe kwa wingi muda mfupi wamsome adui waondoke, Green Berets waje baadae ila wakae muda mrefu wakipiga misheni ngumu za rasharasha. Troops wa kawaida wapigane kila siku wao wafe mamilioni.
Isee
 
Jibu lako linatengeneza swali:

Kwani vifaa vilivyotumika kwenda kumkamata si ni ndege aina ya helcopter, sasa hapo helicopter na jeshi la majini inakuwaje, unganisha dot vizuri ili jibu lipate mantiki.
Marekani hata Marine wana helicopter. Helicopter anayotumia rais wa Marekani ni ya Marine, inaitwa Marine One, kama ndege ya rais wa Marekani ilivyo ya Air Force na kuitwa Air Force One.

US Marine wanatumia helicopters. Wana kitengo chao cha aviation United States Marine Corps Aviation Unit.


The United States Marine Corps (USMC) uses helicopters for a variety of missions, including:

Transport: Helicopters transport ground forces and equipment.

Close air support: Helicopters support ground forces in combat.

Special-purpose roles: Helicopters can be used for amphibious assault and raid operations, fire support, interdiction operations, air-to-air operations, and more.
 
Marines ni kitengo maalumu cha jeshi la marekani cha makomandoo waliofunzwa mafunzo yote kwa mpigo wamefunzwa vita ya majini,nchi kavu na angani

Kwa hiyo kukiwa na operation ambayo yaweza hitaji combination ya kupigana hutuma Marines

Askari wengine wako wa ardhini tu wengine wa majini tu na wengine wa angani tu
Marines ni tofauti .Wanaweza yote hayo na mafunzo yao ni ya kufa mtu
Hayo mafunzo yao ni kwa ajili ya kupiga waarabu na waafrika tu.Na sio Russia,China,Iran wala North Korea.
 
Tofautisha kati ya Marine na Navy Mkuu
Marine ni habari nyingine na wanaamini kwa kutatua matatizo mengi
Marines wana mafunzo yote sio ya maji tu hata ardhini
 
Nitajibu kwa mtazamo wangu while opening a room to be challenged. Marine army is easy to operate in terms of costs of operations while the results is higher than infantry and air forces; nitafafanua hapa
1. Meli ya kivita inaweza kupiga doria baharini kwa kutumia askari wachache na vifaa wakati bei ya kuiendesha meli ni ndogo as well, askari wanaweza hata kufanya zamu ya kupumzika/kulala while wengine wakawq alert tofauti na askari wa miguu, hawa wote wanatakiwa kua alert na isadi yao inakua kubwa. Halafu angani, ni gharama zaidi but again huwezi kua na askari wengi kwa wakati mmoja but also huwezi kuiweka ndege just for doria kwa masaa mengi angani tofauti na meli inaweza kukaa baharini zaidi ya mwaka.
Masahihisho kigodo; Osama hawakutumia wana maji, as fast I know, walitumika askari wa anga wenye mchanganyiko wa kimafunzo na askari wa ardhini; zilitumika chopper special ambazo were made special for that operation; hazikua na mlio na kikosi kilocho tumika kwenda kumkamata Osama kilikua kile kilichokua Afghanistan. Vijana wachache makomandoo na operation ilitumia almost 32 minutes; askari wa maji walihusika only kwenye kuuzika mwili wa Osama Bin Laden.
 
Habari ya wakati huu nawasalimu kwa jina la jamuhuri ya muungano🖐️🖐️🖐️,

Isee kwa wale mnaofuatilia au kufahamu maswala ya kijeshi kuna jambo huwa naliona ama kulisikia linanichanganya nisijue why.

Ipo hivi ni kwanini jeshi la ulinzi la Marekani hupenda kutumia kamandi ya wanamaji (MARINE FORCE) katika utekelezaji wa operation zake nyingi nowdayz tofauti na kipindi cha nyuma. Tumezoea nchi nyingi duniani kunapotokea operation mbalimbali wanatumia kamandi husika kutokana na mazingira wanayokwenda. Mfano katika opresheni ya kumkamata osama na kikundi chake ilitakiwa waende ARMY (kamandi ya ardhini) ila wakaenda Wanamaji.

Vipi huwa kuna ajenda ya siri au ni kuwachanganya maboya manaake ninachoamini marine wapo specialized zaidi baharini kuliko infantry ambao medani za nchi kavu ndo pao Japo sikatai huwa wanafanya poa tu.

KARIBUNI TUPEANE UMBEA

Pichani ni mfano wa sare za askari wa marine na nchi kavu kwa wasiojua tofauti ya sare zao.

View attachment 3039495View attachment 3039496
Marine sio kamandi ya maji.
Marine kwa marekani, sio jeshi la maji,

Marine Ni jeshi la wanajeshi makomando Maalum (elite forces) waloiva wenye mafunzo ya ziada.

Ni Kama ilivyo seal team, Delta force, SWAT n.k

Jeshi la marekani la majini linaitwa NAVY
Nope. Marine sio special force kama hizo ulizotaja. Ni branch ya jeshi la US ambayo ni versatille, yaani wana uwezo wa ku-operate majini na nchi kavu. Halafu SWAT ni kitengo cha polisi na sio jeshi. Special forces nyingine ukiacha Navy Seals na Delta Force ni Army Rangers, Green Berets, MARSOC, Air force Special tactics n.k.
 
Back
Top Bottom