Kwa wale waliosoma Seminari za Katoliki

Ukimuangalia John Mnyika anavyo behave ni mfano bora wa product za Seminary.

Zamani hata TISS walikuwa wanakwenda kubeba vijana kule.
 
Last edited by a moderator:

NAAMINI:
Waliosoma seminary kwa uzoefu mdogo nilionao ni watu fulani wenye mwelekeo chanya katika nyanja zote za maisha. Katika uongozi wapo sawa lakini pia katika mambo mengine ya ajira (ufanisi kazini), biashara, uanzishaji na uongozi wa makampuni binafsi.

Nimesoma seminari, ninawenzangu niliosoma nao seminari moja (walionitangulia, niliokuwa nao mwaka mmoja na hata niliowatangulia). Nipo jijini Dar es Salaam, nakutana nao baadhi tunawasiliana, tunafahamiana tunafanya nini katika swala zima la maisha....... ipo wazi wote tunaona kila mmoja yupo VIZURI pale alipo (ajira, uongozi biashara, familia, etc).

Kama binadamu hatuwezi kuwa sawa wote kwa kila kitu hilo lipo wazi. wapo baadhi ambao kwa bahati mbaya mambo hayakwenda vizuri kutokana na sababu tusizozifahamu... NI MAISHA.

Haimaanishi kuwa kusoma seminari ndio kufanikiwa maishani, HAPANA!!! unaweza soma popote au hata usisome ukafanikiwa. Ila kwa kiasi kikubwa SEMINARI zinamjenga kijana/mwanafunzi kujitambua na kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha. Maadili mema yafundishwayo huko ni msingi mkubwa wa matokeo katika maisha.

Natamani kuendelea ila kwa sasa muda......
 
Dah..!! Maisha ya seminary matamu sana st.pius x seminary au makoko seminary Musoma R.I.P fr.Fmakure
 

nyie mlikuwa wazee wa "ORA ET LABORA"
 

mkuu umenena vyema sana.....natamani siku moja waseminary waseminary zote Tanzania tukutane mana naamini sisi sote tu watoto wa mama mmoja yani kanisa
 
Dah..!! Maisha ya seminary matamu sana st.pius x seminary au makoko seminary Musoma R.I.P fr.Fmakure

nasikia makoko palikuwa sio jamaa yangu kapata upadre mwaka huu hapa jimboni Dar anaitwa Gasper basilidi walikimbia hapo wakaenda sps
 

Duu kwa miaka niliyosama mimi kulikuwa hakuna swala la tuition kwa mseminary na bado uhakika wa kupiga pepa ulikuwa mkubwa. I remember Likonde seminary
 
Kuna vitu common kwa shule za seminary, Majina ya wapishi mara nyingi yanakuwa ya utani au kuchekesha, waseminari wengi wakiwa shule wanakuwa ni wezi wa vyakula/matunda/mifugo na wanaletea hasara shule kuliko unavowafikiria, Kufukuzwa shule ni kitu rahisi sana hasa kukatwa maksi ili mradi uwe below fifty, form one/preform one (nguruwe) hawana haki kabisa na kazima kuna na siku maalum ya kuwakata mikia mara baada au karibia napepa ya mwisho wa mwaka, lazima katika kila darsa kutakuwa na watoto wa mababa(puppets au wanoko) wa kupeleka umbea kwa mapadiri, kati ya masista wanaohudumia mafadha lazima mmoja atakuwa chakula ya mseminary, kulima ni kitu cha kawaida na miraba yao wanachongea sifa yaani mirefu balaa na waseminari huwa wanapendwa sana na watoto wa kike wa kijijini (sehemu ilipo shule). SIJASAHAU MASIFU HASA YALE YA JUMAMOSI USKU KUAMKIA JPILI AMBAYO NI SIKU YA WALI MDUDU.
 
Maisha seminari ni mazuri sana mimi niliyafurahia sana hasa kuimba nyimbo za kiingereza na mafundisho mbalimbali yanayomhusu Mungu na pia maadili, yote hayo yanapatikana semenari.Niifukuzwa O level nikiwa form three nikarudi advance kusoma seminary tena. watu walio soma seminari hutumia zaid yale mafundisho kwenye maisha yao
 
Ha ha ha nakumbuka mbali st Pius makoko seminary rector fumakule aka pumbu ..full sala masifu plus poor diet

R.I.P Fumakule alivyotoka Makoko akaelekea Peramiho amefariki akiwa Peramiho
 

We utakuwa ulimazia Ujiji semanary...!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Huyu c akaanzishe uzi wa waliosomea St. Kayumba au st. Mwajuma? Msuli niliopiga mtu akinikashifu this way ananikeraje mie...!


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Duu kwa miaka niliyosama mimi kulikuwa hakuna swala la tuition kwa mseminary na bado uhakika wa kupiga pepa ulikuwa mkubwa. I remember Likonde seminary

ila kwasasa likonde imepotea mkuu...ebu kawatieni vijana
 
Seminari ni kama jkt ukijituma utafanikiwa maishani.
 
Nimesoma posts zooote sijawaona wadau wa St. Joseph's seminary Ujiji- UJISEMI, mko wapi?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 

Jamani umenipeleks mbali sana mkuu...! Atakumbukwa fr. Duba(baba gambera) na fr.Wabanhu spritual directory sengerema seminary. Hawa mapadri walinifukuza 2002, nikiwa form two walinivurugia future yangu. Ila Mungu awasamehe. Maana mpaka sasa bado nasuffer of their impact to my education career.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…