Mkulima na Mfugaji
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,047
- 1,832
Habari wakulima na wafugaji,
Kuna watu ambao wanataka kujiingiza kwenye kilimo cha michungwa muda ni huu wa kuandaa shamba,
1. Lima shamba
2. Ng'oa visiki
3. Fanya layout
4. Piga mashimo
5. Weka mbolea ya samadi
6. Subiri mvua hasa zile za masika
Mimi nipo Muheza Tanga na mkulima
mdogo wa machungwa. Mbegu zipo
nyingi ila zinazotumika kwa sasa ni
msasa na valencia. Tofauti yake ni
kwamba msasa unakomaa mapema
na unakulazimisha kuuza mapema.
Mbegu hii hulimwa na wakulima
wenye kipato cha chini ambao
hawawezi kuvumilia njaa. Bei yake
shambani huanzia Tsh 20 mpaka Tsh
50.
Valencia ndio mbegu
inayopendwa na wakulima wengi
kwani inaweza kukaa muda mrefu
shambani. Pia chungwa linaweza
kuuzwa mpaka Tsh 100 au zaidi ya
hapo.
UNAPATAJE FAIDA?
Ukiwa na shamba ekari moja inaweza
kuingia michungwa 80 ambao
utakapokomaa vizuri unaweza kuzaa
hata machungwa 1000.
Wekea umezaa machungwa 800
zidisha mara michumgwa 80 unapata
64000 zidisha mara 100 kama ni
valencia unapata Tsh 6400000/=
GHARAMA ZA KUHUDUMIA
Shamba la michungwa litahitaji
huduma za ukaribu katika miaka
mitatu ya mwanzo baada ya hapo
itakuwa ni kulimia tu na kufanya
usafi Mwingine kama prunning
ambazo hazifiki hata laki tano kwa
mwaka. Kumbuka hapo nimepiga
hesabu ya ekari moja tu.
CHANGAMOTO
Machungwa hasa valencia
uwezekano wa kushambuliwa na
magonjwa ni mdogo sana
changamoto kubwa ni wezi na
machungwa kuanguka kama utakuwa
unasubiri bei kubwa.
SOKO
Zamani soko la machungwa lilikuwa
ni changamoto kubwa kwani mikoa
iliyokuwa inapokea machungwa
ilikuwa ni Dar na Arusha tu ila kwa
sasa soko ni kubwa mpaka Nairobi
na Mombasa kwa mfano inafikia
kipindi ukiwa na machungwa
shambani wateja wanakusumbua
wewe.
UPATIKANAJI WA MASHAMBA
Mashamba yanapatikana ila kwa tabu
na bei yake iko juu kidogo.
KUHUSU WAFANYAKAZI
Wafanyakazi wanapatikana pia
unaweza kujenga nyumba ya kawaida
shambani na Mtu akakaa huko huko
kwa Ulinzi.
Nafikiri nimekujibu japo kidogo.
Pia nimepiga hesabu ya ekari moja
na pia mchungwa unaweza kuzaa
mara mbili kwa mwaka.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna watu ambao wanataka kujiingiza kwenye kilimo cha michungwa muda ni huu wa kuandaa shamba,
1. Lima shamba
2. Ng'oa visiki
3. Fanya layout
4. Piga mashimo
5. Weka mbolea ya samadi
6. Subiri mvua hasa zile za masika
Mimi nipo Muheza Tanga na mkulima
mdogo wa machungwa. Mbegu zipo
nyingi ila zinazotumika kwa sasa ni
msasa na valencia. Tofauti yake ni
kwamba msasa unakomaa mapema
na unakulazimisha kuuza mapema.
Mbegu hii hulimwa na wakulima
wenye kipato cha chini ambao
hawawezi kuvumilia njaa. Bei yake
shambani huanzia Tsh 20 mpaka Tsh
50.
Valencia ndio mbegu
inayopendwa na wakulima wengi
kwani inaweza kukaa muda mrefu
shambani. Pia chungwa linaweza
kuuzwa mpaka Tsh 100 au zaidi ya
hapo.
UNAPATAJE FAIDA?
Ukiwa na shamba ekari moja inaweza
kuingia michungwa 80 ambao
utakapokomaa vizuri unaweza kuzaa
hata machungwa 1000.
Wekea umezaa machungwa 800
zidisha mara michumgwa 80 unapata
64000 zidisha mara 100 kama ni
valencia unapata Tsh 6400000/=
GHARAMA ZA KUHUDUMIA
Shamba la michungwa litahitaji
huduma za ukaribu katika miaka
mitatu ya mwanzo baada ya hapo
itakuwa ni kulimia tu na kufanya
usafi Mwingine kama prunning
ambazo hazifiki hata laki tano kwa
mwaka. Kumbuka hapo nimepiga
hesabu ya ekari moja tu.
CHANGAMOTO
Machungwa hasa valencia
uwezekano wa kushambuliwa na
magonjwa ni mdogo sana
changamoto kubwa ni wezi na
machungwa kuanguka kama utakuwa
unasubiri bei kubwa.
SOKO
Zamani soko la machungwa lilikuwa
ni changamoto kubwa kwani mikoa
iliyokuwa inapokea machungwa
ilikuwa ni Dar na Arusha tu ila kwa
sasa soko ni kubwa mpaka Nairobi
na Mombasa kwa mfano inafikia
kipindi ukiwa na machungwa
shambani wateja wanakusumbua
wewe.
UPATIKANAJI WA MASHAMBA
Mashamba yanapatikana ila kwa tabu
na bei yake iko juu kidogo.
KUHUSU WAFANYAKAZI
Wafanyakazi wanapatikana pia
unaweza kujenga nyumba ya kawaida
shambani na Mtu akakaa huko huko
kwa Ulinzi.
Nafikiri nimekujibu japo kidogo.
Pia nimepiga hesabu ya ekari moja
na pia mchungwa unaweza kuzaa
mara mbili kwa mwaka.
Sent using Jamii Forums mobile app