Kwa wale wenye "MAJINI" vichwani au pembeni yao

Mzee ni add kweny hilo group namba zang hizo 0768174787
Mkuu kwa kukusaidia tu usiwe unafuata watu usio wajua ,na acha tabia za kuweka namba yako online wazi kama hapa,kwa hiyo namba yako information zako kibao umeziweka wazi pasipokujua the same kwa kumfuata huyu jamaa utaingia kwenye matatizo.Si kila kitu kinafaa epuka sana hawa watu wa kwenye mitandao jamaa yuko ki busijness zaidi,utaumia mkuu.Mtegemee Mungu wa kweli achana na elimu hizi za siku za mwisho.
 
Biashara gani ninayoifanya mkuu, ya kununua namba za whatsapp au?
 
Elimu hii unaoitoa wap
 
Wewe NI mpumbavu na mjinga kwa wakati mmoja...kwani ruhusa ya KULA wali na chapati umeitoa wapi?mi toka Niko tumboni mwa mama yangu nakula kitimoto....na nitaendelea KULA kitimoto mpaka MBINGUNI....NYANI WEEE
 
Wewe NI mpumbavu na mjinga kwa wakati mmoja...kwani ruhusa ya KULA wali na chapati umeitoa wapi?mi toka Niko tumboni mwa mama yangu nakula kitimoto....na nitaendelea KULA kitimoto mpaka MBINGUNI....NYANI WEEE
povu la nini mkuu!
 
Japo uzi ni wa muda kidogo ila nimeona nichangie ni kwamba , hakuna jini mwema anayeingilia mambo ya binadamu yeye kaumbwa ni kiumbe na sisi ni viumbe nia ni moja tu kumuabudu mwenyezi mungu.

Nina wasi wasi wewe jamaa ni mganga wa kutumia majini , na kaa ukijua kuyatumia majini kwa kutaka yenyewe au kwa kuyalazimisha ni moja ya shirki na shirki huwa haisamehewi.

Na mwenyezi mungu anajua zaidi.
 
Unaelewa nini unaposkia au kusoma neno shikri?
Tuanzie hapo

Rakims
 
Unaelewa nini unaposkia au kusoma neno shikri?
Tuanzie hapo

Rakims
Mkuu na swali langu out of topic lkn nahisi apa Ni mahali panapofaa Kuna jamaa yangu mmoja alienda kwa mtaalam akaambiwa ameibiwa kivuli Cha kwa nguvu za Giza Swali je kivuli kp alichokuwa anazungumzia na kina kazi gn kwa mtu na je kama hakipo hasara zake Ni Nini...nitashukuru Kama utanijibu
 
Haina tofauti na mtu aliyetolewa msukule lakini lengo la hawa waliosema hapo walilenga kivuli ni nyota yake na kwa maneno mengine nyota kwa hawa waswahili wanaita bahati hivyo bahati yake inakuwa inatumika na mtu mwingine hali ya kuwa yeye anabaki kuhangaika na maisha ya kila siku

Rakims
 
Lakini Kuna uwezo wa kurudisha hiyo nyota yake mtaalam?
 
Unaelewa nini unaposkia au kusoma neno shikri?
Tuanzie hapo

Rakims
Niende moja kwa moja

shirki ni kufanya kitu katika aina za ´ibaadah kumfanyia asiyekuwa Allaah .

Ibada zipo za aina nyingi zinazochukuliwa kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Hivyo basi, yule mwenye kufanya kitu katika aina ya ´ibaadah hizi kwa asiye Allah, basi huyo ni mshirikina ambaye kafanya shirki kubwa inayomtoa katika Uislamu.

Mwenye kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah, akaweka nadhiri kwa asiyekuwa Allaah, akasujudu kwa asiyekuwa Allaah, akamuomba asiyekuwa Allaah,akamtegemea asiyekuwa allah katika wafu na viumbe vilivyoko mbali, akawataka uokozi wafu,majini n.k., huyu kamshirikisha Allaah (´Azza wa Jall). Kwa sababu ´ibaadah kwa aina zake zote ni haki ya Allaah (Azza wa jall).

Jua kuwa hakuna jini mzuri anayeingilia maisha ya binadamu jini ni kiumbe kama mimi na wewe na ameumbwa kwa dhumuni moja na sisi ambali ni kumuabudu Allah pekee .

Unapotaka muongozo kutoka kwa majini either elimu au chochote hauwezi kufanya hivyo bila kuyaita au yenyewe yawe yamekukalia hii inamaanisha umemuona allah hana msaada kwako umeshindwa kutumia alivyokubariki navyo sasa unayafuata majini yakupe muongozo?

Kuna watu mnachafua dini kwa makusudi hakuna sehemu kwenye uislamu umeabiwa utegemee asiye allah.
 
Nimekusoma na kukupata vizuri sana, lakini maana yako ya shirki na hoja uliyochangia mwanzo ni vitu viwili haviendani japo vinafanana kwa kidogo

Rakims
 
Nimekusoma na kukupata vizuri sana, lakini maana yako ya shirki na hoja uliyochangia mwanzo ni vitu viwili haviendani japo vinafanana kwa kidogo

Rakims
Wewe unaelewa nini kuhusu shirki? Tuanzie kwanza hapo.
 
Wewe unaelewa nini kuhusu shirki? Tuanzie kwanza hapo.
Shirki ni kuabudu chochote kisichokuwa mwenyezi Mungu kukitegemea kama muumba.

Kukiri kuwa hakuna Mungu isipokuwa chenyewe na kuomba au kusali kwa imani kama sanamu, mizimu, majini, jua n.k

Lakini kuwa karibu au kuzungumza na hivyo shirki yake inakuja kwenye kukiabudu.

Pia neno shikri sio uchawi.
Uchawi ni kitu kingine na shirki ni kitu kingine na pia shirki sio miujiza. Miujiza ni jambo lingine na shirki ni jambo lingine,


Achilia mbali Shirki na Ushirikina kwa waswahili wenyewe hawawezi kukupa maana ya utofauti wa maneno haya shirki ikisema maana yake ni kuabudu asiye kuwa Mungu na USHIRIKINA wanakwambia ni uchawi.

Hali ya kuwa ni neno moja likiwa na mitajo tofauti lakini linalazimishwa kuwa na maana mbili tofauti.


Rakims
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…