Toofast
JF-Expert Member
- Dec 23, 2015
- 522
- 942
Noma sanaNDIYO HUYO HUYO HANA MAKUU HUYO NINJA NI MPORE MWAMBA MIMI NILISOMA NAE O LEVEL NA ADVANCE ALIRUDI PALE TUKAGONGA NAE.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Noma sanaNDIYO HUYO HUYO HANA MAKUU HUYO NINJA NI MPORE MWAMBA MIMI NILISOMA NAE O LEVEL NA ADVANCE ALIRUDI PALE TUKAGONGA NAE.
Nimemkamata mwanangu aliyekula hela ya ticha alipoagizwa voucherDunia kijiji wakuu [emoji3]
Dada Nakubusu sio kuwa hawatakiwi kuzalishwa ila hata ungekuwa wewe ukimzalisha ukweli ni kuwa utakuwa umeingia cha kike .[emoji849][emoji20][emoji20]Kwahio hawapaswi kuwa na familia?,nani wa kuwazalisha kwama sio nyie wanaume?
Aki andika kitabu Cha misuko suko yake, na Hilo jina basi ata uza Sana🤣😄Linachekesha sana 😀
Kuna vitabu vya Pure Maths 1 na 2.Vijana wa siku hizi!!! "Eti pure mathematics"..... ni Advanced mathematics. Hakuna somo la mathematics A level katika combinations za PCM, PGM na EGM linaloitwa pure mathematics. Hiyo pure maths ni hesabu tu katika Advanced maths. NB: mimi nimesoma PCM miaka kadhaa ya nyuma.
Nakumbuka rafiki yangu mmoja yeye alipangiwa mzumbe alisoma mwezi mmoja tu akarudi Dsm akamalizia azania, nilipo muuliza vipi mbona umekimbia akasema wewe wacha tu ile siyo shule ni kufuru.Hizi shule(mzumbe,pugu,kisimiri,ilboru,kibaha and the likes) japokua siku izi nyingi zimepoteza sifa zake aisee kama una moyo mwepesi usiende huko unaweza kupata depression au pressure ukashindwa kusoma
Miaka Hio mwisho wa miaka ya 2000 niliripoti Moja ya shule tajwa hapo combination ya pcm... Kipindi hicho special school wamejaa watoto wa dar kutoka (kibaha, Azania, pugu) aisee Hawa madogo wana sifa kishenzi.... Mtu anakuja kuripoti form 5 ameshamaliza topic zote za form 5 anakaribia kumaliza za form 6
Sasa si matozi tulivyomaliza form 4 vitabu tukatupa Kule mpaka siku ya kuripoti hujawahi kupiga pindi lolote... Unakutana na vitoto vimesoma sijui mchikichini huko aisee wamefuta topic zote, aisee nilipata presha sana mpaka kuzoea ile Hali.... Nakuta madogo wanapiga integration kama hawana akili, ukikaa bwenini wanaulizana kwa nguvu reaction za organic. Chemistry huko....
Dah yaani mwezi wa kwanza form 5 watu wanasolve necta review nikasema hapa nimeyatimba... Aisee ile presha ya ku catch up nilipata shida Sana sio Siri... Ukiwa na roho nyepesi unaweza kukata tamaa Moja kwa Moja
Kuna dogo tumeingia form 5 alikua anaitwa T.O (Tanzania one) alitukimbiza wote form 4 aisee huyu Jamaa mpaka Leo hua namuogopa. Hua namwambia hata hii kazi ya u engineer unayofanya unastahili kua somewhere else una potential kubwa sana, picha linaanza tumeingia form 5 hapo.... Sasa form 6 walikua wanafanya fitness tests (hii anatokea mwanafunzi mmoja au wawili wanatunga mtihani alafu wengine wanafanya japo sio lazima)
Ujinga wa hii mitihani wanafunzi wanajua kukomoana yaani maswali yote unakuta ya kibabe... Kuzungusha 0 huku ni kawaida tu ndo maana wengi walikua hawataki huu ujinga, dogo bana tunafika form 5 kaskia form 6 wanafanya fitness test ya physics dogo akazamia akapiga Pepa... Matokeo yanatoka form 6 karibu wote wamefeli dogo kawakimbiza.... Wote wanaulizana hili jina nani mbona hatumjui... Kuja kuulizia wakaja kugundua ni dogo wa form 5 aisee jamaa walimind kinoma akapigwa marufuku kabisa kusogeza pua kwenye fitness tests za form 6
Huyu dogo tulipofika form 6 sidhani kama aliwahi kukaa akasoma, jamaa alikua anakaa zake class watu wamepanga foleni na maswali Yao yaliowashinda dogo anapiga yote tu hajali kama ni ya physics, chemistry, pure au bam ye anasolve tu. Alikuja kua Tanzania one tena form 6 jamaa walimtangaza hesabu paper 1 na 2 zote alipiga 100%.
Huku kama una roho ndogo sio pa kwenda mi nusura panishinde nilitaka nirudishe mpira kwa kipa(kuhamia private)
Mkuu kwani watu wanakukimbiza mwanzo mwisho hawapoiNilifika shule ya namna hii nimeripoti tuu nikakutana na haya mambo watu wametokea shule kali huko aisee mimi nimetokea shule ya kata duh hakuna walimu hata akija anafundisha kama watu waliokwisha kusoma tayari akiuliza swali watu wanajibu nabaki peke yangu ambae sijajibu. Watu form five anasolve chand, tom duncan.Basi bwana kuna jamaa mmoja alikua anasema physics rahisi sana kwake kwahiyo wale ambao hatujui lolote jamaa akaanza kutufundisha kuanzia topic za mwanzo kabisa. Cha kushangaza ukaja mtihani wa phyisics jamaa nikamkimbiza yeye na majamaa wengi tuu waliokua manakua na kujionesha aisee hahaha sitasahau mimi naenda kwa mwana tuendelee kupiga pindi jamaa akanichana "Sina muda nina mambo mengi" baadae shule ilivokuja kuchanganya hakuna cha aliesoma tuition au umetoka sijui st nani mziki ulikua mzito kwa wote zile mbwembwe huwaga za mwanzoni tuu.
Hakuna elimu rahisi kama ya chuo mkuu, mtu aliyepiga 1 kipindi chetu hawezi kushindwa na viswali vya MT hapo chuoMkuu hongera kwa kupitia shule hizo za vipaji. Maana inasemekana kule ndipo panatoka bongo za kuendesha nchi ( Sina hakika ukizingatia wenye vipaji wanawindwa na wenye wivu ovu). Panatamanisha asikwambie mtu! .
====
Sasa baada ya 4 na 6 linaanzia picha!!!!
Yaani Kasheshe inaanza pale Ukiingia Chuo Kikuu na mihemko ya wani ya Tatu na wani ya saba Hasa shahada za "sayansi asilia au sayansi gumu". Nyote mnakuwa sawa sawa... Divijheni zenu mnaziacha getini!!
Na huyo wa wani kama alikuwa ana meza Maswali na majibu huko A levo na O levo...anaweza kukimbizwa Chuo kwa muhula wa kwanza tu . Maana kule naambiwa ni mwendo wa kosepti na apulikeisheni mbinu katika kukabili changamoto halisi!!!
Kwa maneno mengine vijana mkipata furusa kwenda huko nendeni mkapambane. Maana Kipimo halisi ni huko kwenye Shahada!!!
Haha ndo huyo nimesoma nae mkuu, alikua na jamaa yake anaitwa shaka wanafatana muda wote, japo shaka hakuingia top 10 ila alipiga one ya tatu safi kabisa.... Japhet ni shida sana.... Jamaa hajawahi kukaa kusoma yeye alikua analetewa maswali tu anasolveAcha uongo mkuu, kuna mwamba anaitwa JAPHET.
Alikua T.O ACSEE 2010 Ilboru, na T.O CSEE 2007 Arusha day.
Nafikiri wamenye au Arusha Day au mtoa mada anaweza thibitisha hili.
fundi sanifu siyo lazima awe form 6. Ukiona fundi sanifu ana form six basi huyo alifeli form six. Best Engineers and Technicians ni wale waliopitia Technical Colleges like DIT, Arusha tech, MUST etc.Kwa masomo ya arts ni kupoteza muda Ila sayansi hasa PCM siyo level ya kuiruka.
Muhimu sana mbele ya safari huko elimu ya juu. Pia katika maisha ya kawaida ya fundi sanifu au mhandisi.
Tena sana mkuu washafanya physics hesab kemia bios kama kiswahili miaka yetu physics kupata A unajulikana wilaya nzimaSa ivi Kuna shule nilikuta karibia darasa zima Lina 1.3 pcm na pcb .. nikasema hii sasa ishakua dharau
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Nilienda nimechelewa nikakuta hao mabongoland wamesharipoti wameshamaliza topic zote
Nikataniwa niandike electronic configuration Mimi akili yangu nikawa natumia zile za o level 2:8:8 walicheka balaa mambo ya orbitals ,Wala vi theory vya aufbau , Pauling exclusion sijui kama zipo
Majamaa yakawa yanadhusha ma theory ya electro chemistry na ma reaction ya delocalization za benzene na Ortho and para kwenye organic nilitaka kulala mbele nimwbie mshua anipeleke shule za arts
Alianza kuwa T.O tangu shule ya msingi.Mtanzania pekee aliyekuwa T.O O-level na Advanced level ni Martin Chegere,Akaenda mlimani akawa best student,masters akaongoza,PhD Sweeden pia akaongoza!
now yuko Udm anapiga madogo pindi.
Hapa uongo tupo live udsm coict hapa telecom hata wenye 1-8 tunasoma naoSa ivi ukipiga 1.5 pcb muhimbili huwezi pata intake, kwa ufaulu huu nadhani muhimbili wanachota 1 za tatu tu...
Au pale udsm pcm hata 1.4 tele communication eng wanaweza wakakutema maana 1.3 ni za kumwaga.... Kuna mwaka T.0 mwenyewe alikua na 1.4 enzi zile Kuna somo Tanzania nzima hakuna aliyenusa A dadeki