Kwa wanaoifahamu Zambia; Msaada tafadhali nahitaji kwenda kufanya biashara huko

Mkuu unataka kwenda mji gani huko zambia hilo nivizur ukapanga maana kuna miji mikubwa yakibishara kama kitwe, lusaka nk
 
Mkuu unataka kwenda mji gani huko zambia hilo nivizur ukapanga maana kuna miji mikubwa yakibishara kama kitwe, lusaka nk
Kwa kuanzia nataka nifikie lusaka baada ya hapo ntafanya utafiti zaidi sehem gan biashara yangu itatoka zaidi
 
Chukua mzigo kidogo for research purpose, misha yako gharama kidogo ukilinganisha na Tanzania(chakula&accommodation).Umepewa ushauri wa kustamp visit trip make sure you do that,ukisema unaenda kibiashara utakutana na vikwazo na gharama ambozo si za lazima.Ni Watanzania wengi wanaofanya biadhara hiyo kwa kutembeza(vending) ambao hujulikana kama ego ego au kabaza lakini kama unataka kufungua duka dogo kuna sehemu kama COMESA kwa Lusaka na masoko ya Copper belt (Ndola&Kitwe) kuna Wabongo wengi mengine watakufungua mkikutana hukohuko kwenye kazi.Good spirit,nenda ukaangalie na kwa jicho la tatu unaweza kuona fursa zaidi ambazo wengine hawazioni.
 
Tazama hii kuna rafiki yangu mzambia amekuja kunitembelea tangu tarehe 27/Nov.Katika mizinguko yetu tukafika Segera (Tanga) tukastop kidogo kupata matunda,tukanununua machungwa.Mm nikamsogelea kijana mkata madafu anikatie dafu moja la nazi,nikaanza kunywa yale maji.Mzambia akaniuliza hii nini?Nikamweleza,akasema ooh haya maji tunauziwa kwenye chupa Zambia kwa bei mbaya na yanatoka Uingereza.Nina bahati kuyaona live yanakotoka.Akaniomba nimpige picha akiwa anakunywa dafu.Nikampiga kwa simu.Akatuma picha ile kwenye 'wasap' kwao Zambia.Watu wakaanza kumuuliza nini hicho unakunywa?Akawapa jibu.Mm nikabaki nashangaa kumbe kuna watu hawafahamu madafu.Anaondoka leo,amebeba dafu kwenye begi kwenda kuwaonyesha kwao.Wanaita Coconut water.Naona hiyo ni fursa mojawapo.
 
Asante sna mkuu kwa taarifa
 
Daah! Very interested mkuu asante kwa kunipa moyo,najua safari moja hufungua nyingine
 
Mr Mimi mwaka Jana nilienda Zambia kupeleka viatu vya culture lkn nikakuta bei yao ni ndogo na nikaona haina maslahi..nikaamua kupitiliza hadi Namibia ndipo nikakuta soko lipo vizuri..
Lakini wakati naenda Namibia sikuwa na ndugu wala jamaa Ila nilikomaa kiubishi na MUNGU akanikutanisha na watu..
 
Bei yao ilikua kiasi gani na ww ulikua unauza kwa kiasi mkuu ili na mm kidogo nipate abc
 
Aisee mkuu, viatu vya wamasai utauza lakini inabidi ukifika umtafute mzambia akuuzie usionekane wewe ndo unauza. Wazambia hawaoni shida kutumia pesa nyingi kwa mambo ya starehe na urembo.
 
nicheki pm kuna mwl wangu yupo huko, anapiga ujasiria mali!!!
 
Aisee mkuu, viatu vya wamasai utauza lakini inabidi ukifika umtafute mzambia akuuzie usionekane wewe ndo unauza. Wazambia hawaoni shida kutumia pesa nyingi kwa mambo ya starehe na urembo.
Kwann mkuu isionekane mm nauza...lengo la mm kwenda kule ni ku expand soko langu baada ya hapo narud huku kisha ntakua naenda na mzigo ambao ntakua najua ntausambaza kwa wateja wapi
 
Kwann mkuu isionekane mm nauza...lengo la mm kwenda kule ni ku expand soko langu baada ya hapo narud huku kisha ntakua naenda na mzigo ambao ntakua najua ntausambaza kwa wateja wapi
Wana ubaguzi, wanaona wageni wanamaliza fursa zao
 
Ngoja nimuulize hapa dereva mwenzangu wa Lori yy anaendaga Zambia Mara kwa Mara anauzoefu wa kutosha na huko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…