Kwa wapenda mageuzi wote inahitajika nguvu na akili kidogo tu tuweze kushinda, tumuunge mkono Lissu

Kwa wapenda mageuzi wote inahitajika nguvu na akili kidogo tu tuweze kushinda, tumuunge mkono Lissu

Memento

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2021
Posts
4,423
Reaction score
9,986
Baada ya jana Rais kuulizwa maswali ya kimtego na kuyajibu kiholela, ni dhahiri inahitajika nguvu kidogo tu kupata yale tuliyoyapigania kwa miaka mingi.

Hadi sasa raisi kishaonyesha hana nguvu ya kuzuia wananchi wanachodai na tayari kishaanza kuchoka. Tusipotumia nguvu na akili kidogo kwa huyu basi itatuchukia miaka mingi kuja kuchukua hii nchi.

Hadi sasa tayari kishaanza kujichanganya na ameshaona kazi ya Urais ni ngumu, na kwa jinsi alivyo huyu hachelewi kususa na kutuachia nchi na hatimaye mageuzi rasmi yatapatikana Tanzania.

Nilimsikiliza kwa makini sana Mh. Lissu, Lissu anapaswa kuungwa mkono na kila mwenye akili timamu. Lissu anakwambia wakati ni Sasa
Naungana na Lissu, wakati ni sasa.

Huyu mama muda si mrefu ata-surrender, tuendelee ku-push kwa nguvu sana kwa akili na hatimaye tutapata katiba mpya na tume huru.

Tusichoke, tusichoke huyu wa sasa kishaonyesha hana pumzi ndefu za kuhimili mikiki mikiki.

KATIBA MPYA, MIKUTANO YA SIASA NA TUME HURU NI LAZIMA, NI LAZIMA
 
Baada ya jana rais kuulizwa maswali ya kimtego na kuyajibu kiholela
 
Uingereza haina katiba lakini mambo yao yako vizuri tu. Kenya walibadilisha katiba hivi karibuni lakini mambo bado yako hovyo.
 
Back
Top Bottom