talnam
Picha: General Yi Songgye Vs General Choi Young
View attachment 2725445
Kuna hii kazi inaitwa Jeong do Jeon,. Ni drama ambayo infanana na hiyo six flying dragon zote zinaelezea jinsi Joseon ilianzishwa. Six flying dragon imeandaliwa na SBS na ilitoka mwaka 2015. Wakati Jeong Do Jeon ilitoka mwaka 2014 na imeandaliwa na KBS.
JEONG DO JEON
Hiii drama inamuelezea zaidi Jeong do Jeon a.k.a Sambong ambaye ni moja ya wasomi wakubwa katika historia ya Korea, pia alikuwa Neo Confuciunist Philosopher, waziri mkuu wa kwanza wa Joseon. Pia Lee Songgye( King Taejo) mfalme wa kwanza wa Joseon. Naweza kusema kwenye hii drama General Choi Young uhusika wake umeoneshwa zaidi kuliko hata Yi Bang Won.
Kwa sababu hao watubwa 3 ndio walikuwa na funguo za Goryeo ibaki na iangushwe. Ingawa hatuwezi kumbeza Yi Bang Won( King Taejong) mfalme wa 3 wa Joseon, kwa maana yeye ndiye aliyetuma wapambe wakamuue Joeng Mong Ju a.k.a Peoun ambaye alionekana kama kikwazo kwq mapinduzi ambayo Sambong pamoja na Lee Songgye( King Taejo) alikuwa ameyapanga.
Joeng Mong Ju ( Peoun) Huyu ni moja ya wasomi wakubwa kwenye hisoria ya Korea na alikuwa ndiye Waziri mkuu wa mwisho wa Koryeo. licha ya kuwa alikuwa mpinzani mkubwa wa Joeng Do Jeon ( Sambong) hawa walikuwa ni marafiki wakubwa toka utotoni mwao na ndoto yao ilikuwa ni kuleta mapinduzi kwenye Taifa lao lilikuwa linanuka rushwa na ufisadi. Kwahiyo Peoun na Sambong hawa wamesoma shule moja na wote walikuwa ni Confuciunist Philosophers. Baada ya mtihani wa Taifa Peoun aliongoza kisha Sambong akishika nafasi ya 3. Uadui wao wakisiasa ulikuja pale ambapo wawili hao walitofautiana kiitikadi kwa maana
View attachment 2725733
SAMBONG aliamini kuwa Goryeo ilipofika haiwezi kurudishwa nyuma Kwahiyo inapswa kuzamishwa kisha ianzishwe Dynasty nyingine ambayo itakuwa na mifumo bora ya utoaji huduma kwa watu na kiutawala mpaka sera za kijeshi mpya.
PEOUN aliamini kuwa kubadilisha Taifa jina sio suluu kwa matatizo yaliyopo kwenye Nchi yao bali wale viongozi wabadhilifu ambao wanafanya maisha ya watu kua magumu wachukuliwe hatua kaili za kuajibishwaji.
Kwahiyo pamoja na tofauti zao bado Sambong pamoja na Lee Songgye walikuwa bado wanamuheshimu sana Peoun kwa maana ndiye aliyekuwa kiongozi( Waziri)mwadilifu kupita hata Nyumba ya kifalme( Ukoo wa Wang) pia kiongozi mkuu wa Majeshi Choi Young alikuwa na heshima kubwa sana kwa wadilifu wake.
Tofauti ya Jeong Do Jeon (Sambong) na Lee Bang Won ilianzia hapo baada ya Yi Bang Won kumuua Joeng Mong Ju ( Peoun) baada ya hili tukio Sambong alimkataa kabisa Lee Bang Won ingawa mwanzoni Sambong alionekana kumpenda Bang Won sababu ndiye alikuwa brightest kati ya watoto wote wa Yi Songgye. Hata Yi Songgye alimkataa Bang Won baada ya Jambo hili la kumuua Peoun ambaye alionekana mwiba mkali kwa kina Lee Songgye na Sambong Ingawa tukio hili liliwapoa kina Sambong kufanya mapinduzi so Sambong akamwbia Chukua jEshi ukakamilishe kazi mie huku kwenye siasa tayari.
kifupi moja kati ya sababu ya Sambong kuuliwa na Lee Bang Won ilianziapo baada ya Sambong kumkataa na ikumbukwe Lee Songgye alikuwa anamsikiliza sana Sambong hata katika utawala wake mambo mengi alikuwa anapanga Sambong. Sambong hakutaka yaliyotokea Goryeo yajirudie tena Joseon hivyo alitaka kuanzisha mfumo wa Constitutional Monarch ambapo Waziri mkuu ndiye kiongozi wa mambo ya serikali na atachaguliwa na watu, hivyo familia ya kifalme kwakua wao wanarithi madaraka hivyo watakuwa tu kama Wakuu wa Nchi. Yi Songgye ( King Taejo) hakuwa na shida alikubali, baada ya Lee bang won kusikia hayo akafanya njama akamuua Sambong kisha Akachukua Nchi maana aliona kama mzee wake kila kitu anachoambiwa na Sambong anafuata na aliona kama Sambong anaidhalilisha nyumba ya kifalme. Kifupi Lee Bang Won alikuwa ni moja ya Viongozi bora wa Joseon licha ya kuwa aliichukua Nchi kwa njia mbaya na aliongoza kwa sheria kali mno. Pia Lee Bang Won alikuwa akiwapenda watu wa Joseon ingawa alikuwa akijuta sana kwa namna ambavyo alimwaga damu za watu ndio maana drama nyingi zina muhusisha na neno 'TEARS'
Hii drama utajifunza siasa, Falsafa pia vita zimo. pia imejikita zaidi katika historia kama unataka kuelewa kwa undani jinsi Joseon ilivyoanzishwa hii ndio first recommendation then ufanye revision na Six flying dragon.
View attachment 2725732
SIX FLYING DRAGON
Hii drama imejikita zaidi kuelezea maisha ya Yi Bang Won jinsi alivyopambana na Sambong mpaka Joseon ikaanzishwa, cha kushangaza humu ndani Lee Songgye hakupewa attention kubwa kiiivyo.
Kwenye hii drama ya six flying dragon kuna baadhi ya washiriki katika historia hawapo au visa katika historia havipo ila directors walijiongeza hivyo ilikuleta utofauti na ile drama ya Jeong do Jeon.
Ndani ya Six flying dragon utajifunza Siasa, Falsafa pia utaenjoy Action humu ndani, kuna mdada anaitwa sijui Chuksangwa anagawa dozi huyo!!!..
Kifupi drama zote ni nzuri, na kila moja inaupekee wake. Na zote ni fupi tu zina episode 50 kwa 50
NOTE: SAMBONG anahesabika kama msomi wa Joseon na msaliti wa Koryeo while PEOUN anahesabika kama msomi wa Goryeo na mwaminifu wa Goryeo
General Choi Young anahesabika kama Shujaa wa Goryeo wakati Lee Songgye anahesabika kama shujaa wa Joseon.
Recommendation
Drama yenye Story mwendelezo wa hizo mbili ni
THE GREAT KING SEJONG inamuelezea mtoto wa Lee Bang Won aitwaye Lee Do au Yi Do( Sejong the Great), ingawa Tree with Deep root nayo inaelezea japo nayo wamejiongeza director, Jang young sil pia
zote hizo zinamgusa Sejong na utawala wake.
Hawa ndio Wafalme 5 bora wa Joseon
1. Sejong the Great( mtoto wa Yi Bang Won)
2. Jeong Jo( mtoto wa Prince Sado na Mjukuu wa Yeong Jo)
3. Yeong Jo( mtoto wa Dong yi na Sukjong)
4. Taejong ( Lee Bang Won)
5.... utajaza hapa.
TAHADHALI: Chunga ulevi wa Historical drama usije ukakuathiri bure.
Alamsiki.