Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

[emoji23] [emoji23] [emoji23]na kweli ukijifanya mtabiri aisee unaumbuka hivihivi umenikumbusha mimi pale niliwaza kwamba hapo hatadondoka atadakwa na katika hiyohiyo prosecution atamsaidia kushinda ile kesi mama weee kilichonipata siri yangu
Hahahahaaaaaaa hapa nilipo nimecheka mpaka majirani wametoka nje. hata mimi nilidhani atamsaidia kwenye kesi pale ambapo atakapo pona baada ya kujitupa.
tumeaibika
 
Khantwe Na Damushin Mnanichekesha Na Izi Comment Zenu Hahahaha Poleni Kwa Kuaibikaa Hahahahaha...Hii Drama Ni Inachanganya Kidogo Ndo Imenifanya Nivunje Mwiko Wa Kutoziangalia Izi Mambo..

Pale Restaurant Suzy Alikoenda Kuachana Na Lawyer (Lee Boo-Yeom) Alivyosimama Na Kuanza Kuongea Kwa Sautii Mpaka Watu Wakaawa Na Mshangaa, Umu Ndani Suzy Kauwa Vibaya Sana, Na Napenda Jinsi Chemistry Yake Na Mama Yake Ilivyo...

Kwaiyo Naombeni Tuchague Kati Ya The Good Guy,Bad Guy Na The Weird One.

Mi Naombeni Niwe The Weird One ( Suzy Anazimaliza Mbavu Zangu)...
 
Binaadamu Alonifanya Niwafatiliee Wakorea,Alonifanya Nipende kazi Na DRAMA Za Kikorea Alonifanya Kuwa Ni Sehemu Ambayo Natamani kwende Panapomajaaliwa InshaAllah, Alonifanya Nipate Mabae Wa Kikorea...

Mungu Amuwekee Na Kufanya Vingi Vizurii..Hongera Zake Kwa Kuongeza Mwaka Mwengine...

Saranghaee..
 
maneno (glossary) ambayo mara nyingi hutumika kwenye korean historical drama(sageuk)
  1. Aba mama : ni neno ambalo hutumiwa na mtoto anayetoka kwenye familia ya kifalme (royal child) kwa ajili ya kumuita baba yake
  2. Agasshi : halina tofauti na neno binti (young lady or miss) kwa lugha yetu,neno hili mara nyingi hutumiwa na mtumishi kwa ajili ya kumuita mtoto wa kike wa bosi wake ambaye hajaolewa
  3. Asshi : ni kifupi cha neno Agasshi
  4. Bin : hawara wa mfalme(Royal Concubine) mwenye cheo kikubwa (First Senior Rank).
  5. Bubuin : ni neno ambalo hutumika kwa ajili ya kumuita Grand Princess Consort (mke wa prince mkubwa)
  6. Buin: mke (Wife) lakini kwenye modern drama hutumia maneno tofauti kama vile yeobo.
  7. Cheoja/cheonyeo:msichana ambaye hamfahamu mwanamme (virgin).
  8. Cheop/b: masuria (Concubine).
  9. Chonggak : kijana ambaye hamfahamu mwanamke (Bachelor).
  10. Daebi :mke wa mfalme aliyeondoka madarakani (Queen Dowager) na mara nyingi kwenye drama tunawasikia watumishi wanasema daebi mama.
  11. Daegam : ni neno ambalo mara nyingi hutumiwa kwa ajili ya kumuita kiongozi mwenye cheo kikubwa
  12. Dae-janggun : Great General.
  13. Daewang :Great King
  14. Doryeon-nim :Young Master.
  15. Eolja :mtoto wa tajiri (nobleman) aliyezaliwa na mtumwa
  16. Eoma mama:ni neno lenye maana ya mama ambalo hutumiwa zaidi na mtoto anayetokea kwenye familia ya kifalme
  17. Ginyeo/ gisaeng : msichana ambaye ni kahaba(hutumika zaidi kwenye drama zinazozungumzia taifa la joseon)
  18. Gunbuin 😛rincess Consort( mke wa prince)
  19. Halba mama/Harabanim: ni neno lenye maana ya babu na hutumiwa zaidi na mwana wa mfalme
  20. Halma mama: bibi
  21. Hwangje : Emperor.
  22. Imgeum:mfalme (King).
  23. Janggeun :General.
  24. Jeoha: Crown Prince.
  25. Jeonha: mfalme ila mara nyingi hucheka sana wakisema chona tafadhali niue
  26. Jumo : mmiliki wa mgahawa na mara nyingi utasikia chumo niletee pombe
  27. Ma-nim : ni neno ambalo mara nyingi hutumiwa na mtumishi kwa ajili ya kumuita mke wa bosi
  28. Mudang :Shaman(mganga)
  29. Naeuri/nari :mtu mwenye cheo kikubwa kama kijana au kama tajiri, ni neno ambalo mara nyingi hutumiwa na masikini
  30. naegeumwi:walinzi wa mfalme
  31. naegeumwijang:mlinzi mkuu wa mfalme
  32. Orabeoni/orabi :kaka ila kwenye modern drama wanatumia oppa
  33. Pyeha:mfalme na mara nyingi korean drama zinazozungumzia taifa la goguryeo hutumia neno hili.
  34. Seobang-nim :mume (Husband).
  35. Seonbi :msomi (Scholar)
  36. Soja:ni neno ambalo mara nyingi hutumiwa na kijana kwa ajili ya kujitambulisha kwa wazazi au mtu mkubwa
  37. Sonyeo:ni neno ambalo hutumiwa na mtoto wa kike anapojitambulisha kwa mkubwa wake
  38. Soin:ni neno ambalo hutumiwa na mwanamme anapozungumza na kujitambulisha kwa mfalme
  39. Wang :mfalme (King).
  40. Wangja: prince
 
Pale Restaurant Suzy Alikoenda Kuachana Na Lawyer (Lee Boo-Yeom) Alivyosimama Na Kuanza Kuongea Kwa Sautii Mpaka Watu Wakaawa Na Mshangaa, Umu Ndani Suzy Kauwa Vibaya Sana, Na Napenda Jinsi Chemistry Yake Na Mama Yake Ilivyo...
hahahaaaa umenikumbusha basi nilifikiri pale ndio wanaamua kuachana, hatari sana huyu director na muandishi watatuua kwa michomo
 
Yaani Hii Ost Ni Hatari..

Awards Za Mwakaa Huu Sijuh Yaani Maana Kazi Zote Ni kari, Kutakuwa Na Mpambano Wa Kukata Na Msumenoo
naona SBS tv drama awards zitakua ngumu sana jaribu kufikiria mafanikio ya
  • suspicious partner
  • my sassy girl
  • defendant
  • reunited world
  • saimdang lights diary
  • whisper
  • while you were sleeping
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] umenikumbusha nilicheka balaa et the more anafeel apologetic ndo ndo sauti inazidi kupanda
 
Khantwe na aminas bado najiuliza kuhusiana na mwanajeshi
  1. kama yeye ndio ni muuaji wa police sasa kwa nini alishindwa kubadilisha nguo na akaingia kwenye basi na form zake au ndani ya begi alikuwa hana nguo?
  2. kwa nini alikuwa ana khofu kubwa sana na anaonekana kama ni mtu muoga ambaye hajawahi kufanya tukio la hatari na kwa nini amekimbia jeshini na anakwenda wapi?
  3. je yule mwana jeshi alijiua au aliripua bomu?
  4. na je nini kitatokea kwa yule mdogo wake lee jong suk na je kim so hyun atachukua hatua gani dhidi ya baba yake ambaye anamtesa mama yake.kwa jinsi inavyooneka lee jong suk atashindwa kesi mahakamani akiwa kama wakili na ndipo mdogo wake atachukua maamuzi ya kumuua yule mzee anayemtesa mama wa kim so hyun
  5. hahahaaaaaaaaaa robo ya watu duniani wanaisubiri siku ya jumatano na alhamisi naona kila mtu ana speculate kitachotokea.
  6. inawezekana muandishi anajaribu kutufundisha ya kwamba hatupaswi kufuata majaliwa yetu(fate), kwa sababu majaliwa yana njia tofauti nzuri na mbaya hivyo basi ni jukumu letu kufuata njia iliyosahihi,jaribu kuangalia jinsi gani jae chun alivyoiamini ndoto yake na akaamua kufanya maamuzi ya kumsaidia suzy na mama yake na yule kijana aliyopata ajali na kufa kama angeliachia ndoto yake iwe vile vile alivyoota basi ndio lingetokezea tatizo kubwa alilotuonesha muandishi na director wa drama.vile vile alituonesha kosa la kuamini majaliwa kwa tukio la yule jamaa aliyeungua moto kwa kuwasha kibiriti inamaana bae suzy kwa kuwa lile tukio aliliota ndotoni basi alikuwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya kulibadilisha lile tukio la kinyume, lakini kinyume chake muandishi anajaribu kutufundisha ya kwamba tunapaswa kukubaliana na majaliwa yetu baadhi ya wakati liwe jambo zuri au baya litakalokukuta
 
Hahahahahahahah, Aya Bana Kwaiyo Mimi Ndo Nipo Kati Yenu Siyo Hahahahaha Aya Tuone Nani Mbabee Apo (Like This)

Mmenifanya Nacheka Mwenyewe Kila Nikimuangalia Uyo Weird Hahahahahah Suzy Ni Ndeee Kwelii Kwelii
mwambie Khantwe tukutane mahakamani na ajiandae kisaikolojia kwa kitakachomkuta mdogo wake
[HASHTAG]#logOut[/HASHTAG]
 
hahahaaaa umenikumbusha basi nilifikiri pale ndio wanaamua kuachana, hatari sana huyu director na muandishi watatuua kwa michomo
Yah Si Wameachana Baada Ya Kujua Kuwa Ni Bad Guy So Akaamua Kutokuwa Nae Kwenye Mahusiano...

Kama Unakumbuka Wakati Episode Ya Kwanza Inaanza Kuna Ile Part Suzy Alikuwa Anaongea Na Mama Yake Uku Akimuhadisia Ndoto Aliyeiota Kuwa Kuna Kijana Kamuota Anamkumbatia Na Yeye Wala Si Mtu Wa Kuanza Kumtokea Mtu Ila Anashangaa Kwenye Iyo Ndoto Kamkumbatia Uyo Mwanaume Lol!! Apa Aliniacha Hoi

"Maa You Know that I'm Not The Type To Hit on Guys First"

Maa Wake Akamjibu, ''of Course I know,How Can You Hit on Guys Looking Like that, If You Have any Conscience,That Is"

Suzy Akamuuliza,"Maa,Are You Really My Mom?''

Yaani Apa Maongezi Yao,

Na Kuna Pale Wakati Ameenda Kuchukua Chakula Kwenye Friji,

Mama Yake Anamuuliza''Is He Handsome?'' Anamjibu''Why Does That Even Matter? I have a Boyfriend, You Know"

Mama Yake Anamjibu''Hey,You've Only Seen Him Twice since the Blind Date,Will you marry Him The Next Time You see Him?''
Nilikipenda Sana Ichi Kipande Mpaka Pale Wanamchungulia Jong Suk Anavyoamia Laahh!!!
 
mwambie Khantwe tukutane mahakamani na ajiandae kisaikolojia kwa kitakachomkuta mdogo wake
[HASHTAG]#logOut[/HASHTAG]
Hahaha Wewe Tunakujua Michezo Siyo, Unacheza Sana Rough Kwaiyo Hatuna Jinsi Japo Tunajitahidi Mi Na Khantwe Wangu Apa Kulistopisha Ilo Tukio...

Ila Khantwe Ujuee Tayari Nishakuzimikia (In Suzy Voice) Kwa IYO Usifanye Kama Ahuoni...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…