Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Mkuu,
Anza kwa kupekua posts za nyuma maana tushajadili sana.
Unaweza kuanzia hapo link ya chini.

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako! - Page 73
Si kazi ndogo kuanza ku review page ya 73 to 224 tena kwa umakini wa hali ya juu kusoma kila neno tatizo huo muda na inachosha mkuu ndo maana nikaomba anayefahamu ni vizuri angenitajia maana hazitozidi hata dk 3 katika kunitajia kwa mtu ambaye ni mzoefu.anyway thanks!
 
Seoul 1945 (서을 1945) ni series moja yenye story na matukio mazuri yakusisimua. Ni historia ya ukweli ambayo ilitokea korea miaka ya 1940s' mpaka miaka ya 1950s, ambapo mwanzo walikuwa wakitawaliea na japan empire. Vta vya pili vya dunia vilivyoisha mfalme wa japan akasalenda na kuiacha korea kama marrkani na urusi walivyotaka. Baadae (baada ya uhuru kulitokea mtafaruku mkuwa wa kiitikadi kati ya ujamaa na ubepari na hapo wakapigana vita wenyewe kwa wenyewe ba kupelekea korea kugawanyika kuwa mbili
 
namshukuru Mungu kwa kunijaalia kutimiza miaka 2 tokea nilipofanikiwa kujiunga JF.
kiukweli sikupaswa kuziweka pongezi zangu kwenye thread hii kupitia jukwaa la entertainment ila imenibidi nifanye hivyo kwa sababu ujumbe wangu wa kwanza kuandika ndani ya JF niliuandika humu, hahahaaaaa hata kama itatokezea siku moja nimejaaliwa kuwa trillionair basi sadaka yangu pia itanibidi niianze humu.

kupitia JF nimejifunza mambo mengi mno na bado naendelea kujifunza mambo mbali mbali yanayoihusu dunia yetu tunayoishi.
kiukweli member wa mwanzo kumzoea ndani ya JF ni mwanadada Prishaz, simfahamu wala hanifahamu na japo kuwa sijachunguza background yake kupitia content thread zake ila namuona ni mwanadada mwenye hekima na maarifa makubwa sana, heshima kwako nuna.
nauanza mwaka wa 3 ndani ya JF hivyo basi kama kuna member yeyote niliwahi kumkasirisha kupitia maandishi yangu ambayo 80% nimeyaandika kupitia thread hii basi namuomba anisamehe kwa sababu mimi sijakamilika.

korean drama forever
 
Hahhhahhhhahhhhaaaaaaaa!

Sunbae, Damushin
Nilikuwa najikumbusha posts za nyuma nikakutana na hii basi nimechekaje!

Halafu hizo pesa bado unazo au ndio ushakunywa urojo? Hahhahahahaaa!
aigooooo pesa zangu nilizihifadhi bandari ya dar, sasa bahati mbaya huyu mwenye nchi ameziona na nikimpigia simu hapokei.
kiukweli nipo frustrated
 
Hongera sana Damushin kwa kutimiza miaka mitatu ndani ya hii miaka wengi tumenufaika na uwepo wako na tunatarijia kunufaika zaidi Mungu jalia. Noona anasema asante sana kwa sifa kem kem ulizommwagia, nimefurahi kumuona huyo dogo hapo nilimpenda sana kwenye Dr stranger.
 
Nini kinakufanya useme wakorea wambea wakat wapo so talented katka ku catch feelings na kwa style yao ya uigizaji....Mzungu haeki mkono....Nakushauri tafuta Jumong tu....utaelewa zaid.....
BAABA,MKUUBWA ILE KITU JUMONG NI SHHIDA.
 
december 14 mwanadada song hye kyo alipata nafasi ya kuhudhuria sherehe maalum zilizofanyika nchini china za ufunguzi wa maadhimisho ya mashirikiano ya kiuchumi (Korea-China Economic Partnership). ni mara ya kwanza baada ya kufunga ndoa kwa song hye kyo kushiriki kwenye shughuli za kijamii ambapo alibahatika kukutana na raisi Moon Jae In wa taifa la korea ya kusini.
Song Hye Kyo amenukuliwa akisema: "Iam thankful to be invited to such an honorable event. It is truly an honor to meet with President Moon in this wonderful setting."

NB:

umefika wakati wa china na korea kusini kumaliza mgogoro wao uliopelekea China kupiga marufuku masuala yote yanayohusu utamaduni wa korea kusini jambo ambalo limepelekea athari kubwa sana ya kimapato kwa tasnia ya sanaa nchini korea kwa sababu soko kubwa la hallyu lipo china.
usishangae sana hata sisi tunapotaka biashara hata za kuuza dawa za miti shamba tunakimbilia china kwa sababu ndiko liliko soko.
wenzetu kila wanapokumbana na changamoto ndio wanazidi kuja na mbinu za kumaliza tatizo ila huku kwetu kila tunapokumbana na matatizo ndio tunazidi kuja na mbinu za kuongeza tatizo, sijui waafrika ameturoga nani.
ukiangalia drama nyingi za mwaka huu zinazoonyeshwa na Televisheni za bure nchini korea wanaweka matangazo ya biashara kila baada ya nusu saa tofauti na zamani ambapo walikuwa wanaweka matangazo kila baada ya saa moja.
sheria za korea kusini haziruhusu kuweka matangazo katikati ya show ila unapaswa kuweka matangazo mwishoni mwa show au mwanzo.

Broadcasting Stations Struggle To Survive From China’s Ban On Korean Cultural Content
 
EMPTY dongsaeng, aminas noona
hawa watu wawili nikiwaona najisikia raha sana na hunifanya nisahau dhiki zote zinazoniandama katika maisha yangu ya kila siku.
imefika wakati natamani wiki iwe na siku moja tu nayo ni jumamosi ili nipate kuona performance ya hali ya juu kutoka kwa waigizaji wanaofahamu kazi yao.
si mshabiki mkubwa sana wa Jang hyuk ila namuombea ashinde tunzo ya daesang mwaka huu.


nimefurahi sana kiupande fulani baada ya kugundua ya kwamba jang bo cheon ni mtoto wa nje ya ndoa hivyo basi hastahiki kurithi mali za Cheong A.
Hahahaaaaa huku kwetu waigizaji wazee wenye viwango ni wa kuhesabu.
 
aminas huyu kim rae won uzungumzaji wake wa taratibu unaweza ukaenda kisimani kuchota maji na ukarudi bado hajamaliza kuzungumza.
black knight drama nayo inanifanya nitamani siku za wiki zipungue ziwe angalau 3.hivi hawa bongo movies wanashindwa kuja hata huku zanzibar kwa ajili ya kuomba film location kwenye mahoteli.kama wanaweza kupeana zawadi ya gari za millioni 50 kwa ajili ya birthday wanashindwa kuwekeza kwenye kazi zao zinazowafanya wanunue gari za gharama.
jana nimeota nipo slovenia nakunywa chai na shin se kyung hahahaaaaaa ndio maana huwa sipendi mtu aniulize una ndoto gani kwenye maisha yako, kwa sababu ndoto inakuja na kuondoka lakini malengo hayaondoki.


kabla ya kuangalia black knight nilikuwa naangalia bride of the water god lakini nilipofika episode ya 5 niliamua kuifuta yote kwenye computer yangu, kiukweli haikunivutia kabisa hususan uhusika wa shin se kyung.
 
Hahahahhahahah,Rae won ni bae kabisaaa

Khabari za Siku nyingi kwanza na pole na Kutingwa.

Sijawahi ona Iyo Bride ila Watu wengi sana Wanailalamikia aikuwa nzuri..
Ila humu ndani lazima Rae won bae Amn'garishe Uyu Binti ...Won yupo Vizuri wanamuita King of Romance akifatiwa na Min Ho
 
Uyu Mzee napenda tuh Ukorofi wake na kupenda Zake Ela...Uyu Bibi ndo kabisaaa..

Ila Nimependa Sana Akili za hyuk Oppa Umu ndani Etiii...Na Mo Hyun Nae nimependa Sana Swala La Kukubali Mtoto Wa Mme wake kwa Ujasiri Mkubwa Sana Yaani...Ningetamani Nasisi watz tuige Huu mfano Unamkubari Tuuh na Kumlea ndo damu ya Mume iyo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…