DAEMUSHIN
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 22,428
- 120,464
Korea Broadcasting Actors Union Rep Provides Deeper Insight Into Drama Payment Controversy
taarifa zinazohusu kutokulipwa fedha zao kwa baadhi ya waigizaji zimezidi kuongezeka jambo ambalo limepelekea chama cha waigizaji nchini korea kulitolea ufafanuzi suala hilo.
wiki iliopita baadhi ya waigizaji kama rain, lee na young,jung yoo mi na kim min jung kwa nyakati tofauti walizungumzia mkasa huo wa kutokulipwa fedha zao baada ya kuigiza drama.
siku ya jana (17/01/2018) bwana Song chang gon ambaye ni mkuu wa korean brodcasting actors external relations alipata nafasi ya kulizungumzia suala hilo kwenye mahojiano aliyoyafanya kupitia vyombo vya habari.
kwanza aliyelezea jinsi mfumo wa malipo unavyofanyika kwa waigizaji ambapo song chang gon alisema ili kuelewa sababu ya waigizaji kutokulipwa fedha zao baada ya kushiriki kwenye drama ni lazima tufahamu ya kwamba;
kwenye film waigizaji wanalipwa baada ya film kukamilika na kwenye drama waigizaji wanalipwa baada ya drama kuanza kuonekana kwenye televisheni, kwa mfano kama zoezi la kuigiza drama litaanza december na baadae drama ikaanza kuonyeshwa mwezi january kwenye televisheni basi muigizaji hulipwa fedha zake mwishoni mwa mwezi february kwa sababu mashirika ya habari nchini korea hulipa mishahara mwishoni mwa mwezi.
mfumo huu ndio husababisha makampuni kushindwa kuwalipa waigizaji fedha zao kwa kusubiri mpaka drama itakapomaliza kuonyeshwa na hapo ndipo tatizo linapotokezea, alisema song chang gon.
alipoulizwa ni kiasi gani cha fedha ambacho waigizaji hawajalipwa song alisema siwezi kuzungumzia deni la kila muigizaji analodai kwa sababu hiyo ni ishu binafsi ila kwa waigizaji waliojiunga kwenye chama wanadai jumla ya won billion 3.2 (usd 2.98 million) kupitia mashirika ya KBS,MBC na SBS, lakini hayo ni madeni ya zamani kwa sababu kwa sasa hakuna muigizaji ambaye amewahi kulalamika kutokulipwa fedha zake.
pia amezungumzia sababu inayopelekea kuwa na ugumu wa kutatua tatizo hilo ambapo aliendelea kusema wakati wa utawala wa lee myung bak haki yetu ya kukaa na kuzungumzia suala hili liliathiriwa zaidi na kanuni za serikali.
lakini suala hili lipo mahakamani na tunategemea mwezi machi au april hukumu ya kesi hii itatolewa.baada ya hapo tutakaa na mashirika ya habari, production company na serikali kwa niaba ya waigizaji ili kuweza kulitatua suala hili.
Wawakilishi pia wamebainisha ya kwamba wizara ya utamaduni,michezo utalii na fair trade commission waliiingia makubaliano waigizaji ila kwa jinsi inavyoonekana makubaliano haya hayafuatwi ipasavyo, makubaliano hayo yanasema kama kutatokezea tatizo la malipo basi shirika ndilo litakalohusika na suala hilo.
taarifa zinazohusu kutokulipwa fedha zao kwa baadhi ya waigizaji zimezidi kuongezeka jambo ambalo limepelekea chama cha waigizaji nchini korea kulitolea ufafanuzi suala hilo.
wiki iliopita baadhi ya waigizaji kama rain, lee na young,jung yoo mi na kim min jung kwa nyakati tofauti walizungumzia mkasa huo wa kutokulipwa fedha zao baada ya kuigiza drama.
siku ya jana (17/01/2018) bwana Song chang gon ambaye ni mkuu wa korean brodcasting actors external relations alipata nafasi ya kulizungumzia suala hilo kwenye mahojiano aliyoyafanya kupitia vyombo vya habari.
kwanza aliyelezea jinsi mfumo wa malipo unavyofanyika kwa waigizaji ambapo song chang gon alisema ili kuelewa sababu ya waigizaji kutokulipwa fedha zao baada ya kushiriki kwenye drama ni lazima tufahamu ya kwamba;
kwenye film waigizaji wanalipwa baada ya film kukamilika na kwenye drama waigizaji wanalipwa baada ya drama kuanza kuonekana kwenye televisheni, kwa mfano kama zoezi la kuigiza drama litaanza december na baadae drama ikaanza kuonyeshwa mwezi january kwenye televisheni basi muigizaji hulipwa fedha zake mwishoni mwa mwezi february kwa sababu mashirika ya habari nchini korea hulipa mishahara mwishoni mwa mwezi.
mfumo huu ndio husababisha makampuni kushindwa kuwalipa waigizaji fedha zao kwa kusubiri mpaka drama itakapomaliza kuonyeshwa na hapo ndipo tatizo linapotokezea, alisema song chang gon.
alipoulizwa ni kiasi gani cha fedha ambacho waigizaji hawajalipwa song alisema siwezi kuzungumzia deni la kila muigizaji analodai kwa sababu hiyo ni ishu binafsi ila kwa waigizaji waliojiunga kwenye chama wanadai jumla ya won billion 3.2 (usd 2.98 million) kupitia mashirika ya KBS,MBC na SBS, lakini hayo ni madeni ya zamani kwa sababu kwa sasa hakuna muigizaji ambaye amewahi kulalamika kutokulipwa fedha zake.
pia amezungumzia sababu inayopelekea kuwa na ugumu wa kutatua tatizo hilo ambapo aliendelea kusema wakati wa utawala wa lee myung bak haki yetu ya kukaa na kuzungumzia suala hili liliathiriwa zaidi na kanuni za serikali.
lakini suala hili lipo mahakamani na tunategemea mwezi machi au april hukumu ya kesi hii itatolewa.baada ya hapo tutakaa na mashirika ya habari, production company na serikali kwa niaba ya waigizaji ili kuweza kulitatua suala hili.
Wawakilishi pia wamebainisha ya kwamba wizara ya utamaduni,michezo utalii na fair trade commission waliiingia makubaliano waigizaji ila kwa jinsi inavyoonekana makubaliano haya hayafuatwi ipasavyo, makubaliano hayo yanasema kama kutatokezea tatizo la malipo basi shirika ndilo litakalohusika na suala hilo.