Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Wakorea ni noma wapo fasta hasa kwenye company dinner,wananishangaza wanaokataa kuhudhuria kwenye mnuso kwa sababu binafsi ukiangalia sababu zenyewe hazina umuhimu kama utamu wa msosi husika. Bongo movie wanaishia kunywa juisi na wali nyama napo kwa wanaoigiza kitajiri tu ila ugali ni kwa maskini tu wa bongo movie tena anakula huku kakunja uso kama kanyeshwa kwinini bila kupenda
Bila kusahau zile skonzi za subway. Khaa mtu ana njaa kali eti lunch skonzi na juisi wakorea bana wanajua kujipigia promo
 
hahahahahahahahahaa ina maana bongo movies ni mwendo wa kuigiza hata kama anakunywa juicy ya embe.
ndani ya episode moja wakorea wanakula mara tatu tena vyakula vyao vya asili. drama yoyote ambayo miongoni mwa wadhamini ni subway basi lazima kinukishwe.
ahjumaaaaaaaa nilietee chupa moja ya soju.
neeeeeee
 
Labda Tuseme Wenzetu Wanajitahidi Kuelezea Maisha Yao Kiuhalisia Zaidi, Japo Wanaigiza Lakini Wanayaonyesha Maisha Yao Kupitia Sanaa Yao, Leo Hii Wengine Tumeifahamu Korea Kupitia Sanaa/kazi Zao, Tumeanza Ata Kufahamu Baadhi ya Maneno Yao Wanayotumia Kila Siku Kupitia Sanaa Yao, Vinywaji Wanavyotumia,Vyakula Vyao, Mavazi Yao Na Historia Yao,

Yote Haya Tumeyafahamu Kupitia Maigizo Yao, Sisi Ni Kipi Tunakitangaza Chakwetu Kupitia Maigizo Yetu!?
 
Teena bongo movie juisi moja (glass) watakunywa siku mbili hata wiki nzima.wakinywa kidogo na maongezi,director anasema cut,wanaenda badili nguo hapo tunaonyeshwa baada ya wiki wapo hapo hapo wakinywa juisi na maongezi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]na pombe wakorea wanakunywa za kikweli kweli ila kwetu mwendo wa kujaza maji chupa za bia
 
Hahahahahhaha Daah!
 
nimechelewa kumtakia heri ya kuzaliwa kaka yangu ambaye hatuna uhusiano wowote wa kindugu na hata kibahati mbaya Ahn Jae-Hyeon.
1/07 ametimiza miaka 31.
May 20, 2018. ametimiza miaka miwili ya ndoa pamoja na mke wake kuh ye sun (geum jan di wa boys over flower.)
mahusiano yao ya kimapenzi yalizaliwa rasmi walipokutana kwenye drama ya BLOOD mnamo mwaka 2015.
waliamua kutoa sadaka fedha zao ambazo walikusudia kuzitumia kwa ajili ya honeymoon.
mungu azidi kuwajaalia baraka na furaha kwenye ndoa yao.
kuh ye sun anamzidi mume wake kwa miaka 3.
 
Wale wazalendo naona pia hata lugha yao wanaijali mno hadi makazin wanatumia vikorea na mitandao yao ya kijamii ila kwetu ndo kwanzaa wababa na wamama wanashindana kujipodoa,kuweka dawa nywele,kuvaa ndivyo sivyo.

Honesty kiss scene za wakorea zinadatisha zaidi kuliko za wabongo. Wakwetu wapo busy kuandaa skendo na kiki za kuuzia movies zao,majungu wazi wazi na maringo tele,acha tu wakorea watutawale
 

ni mwendo wa kunywa na kula mwanzo mwisho hamuna kuoneana aibu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hii blood nikiikumbuka najicheka maana nilivuta episode mbili tu kilichonivutia kuendelea na zingine mpaka mwisho ni lips za ahn jae
 
pengine tatizo ni bajeti hairuhusu dada yangu ndio maana glassi moja masaa 4
 
Bajeti si tatizo,tatizo ni wao sio wabunifu mpaka kuvutia wawekezaji. Khaa movie haina hata mdhamini mmoja. Wawe wajanja badala ya kutegemea kiki kuwapa umaarufu bila pesa
pengine tatizo ni bajeti hairuhusu dada yangu ndio maana glassi moja masaa 4
 

ni mwendo wa kunywa na kula mwanzo mwisho hamuna kuoneana aibu.
Ivyi Kwa Chakula Unaanzaje Kuona Aibu!

Sema Siye Pesa Zetu Ni Ndogo, We 1M Unataka Utoe Movie Kweli,

Wenzetu Wanaweka Ela Sababu Wanajua Inarudi, Ndomana Ata Waigizaji Wao Wanalipwa Vizuri, We Muigizaji Unampa Kidogo Ndomana Ata Uhusika Hana, Script Inamwambie Atabasamu Ye Anacheka.
 
hahahahahaaaaaaaaa jamani munanifanya nacheka peke yangu kwa hizi comment zenu.
 
Lee Si Un ndio kichaa kuliko wote
 
hahahahahaaaaaaaaa jamani munanifanya nacheka peke yangu kwa hizi comment zenu.
Hahahaha Waigizaji Watanzania Wanafanya Maigizo Ndani Ya Maigizo, Tuseme Sijuhi Wanaionaje Hii Kazi, Nani Atataka Kuweka Ela Zake Kwenye Undezi Wanaoufanya! Si Bora Ata Tuburudike Na Maigizo Ya Viongozi Kuliko Wao.
 
Hiyo Drama ya Mr Sunshine nilikuwa naisubiri kwa hamu kubwa mno. Nili tamani kuona Lee Byung Hun amekuja kiaje baada ya miaka 9 mara ya mwisho nilimuona kwenye IRIS 1. Ngoja nikae mkao wa kula na vile ni drama yenye bajeti kubwa kuwahi kutokea kwa South Korea $27.8 million najua itakuwa nzuri katika ubora unao stahiki.
 
Dharau ni mbaya sana, ogopa hii tabia. Ni bora kama hupendi ukae kimya tu kuliko kuwadharau namna hii. Hii tabia ya kudharau ndio ilifanya......... Basi tu ngoja nikae kimya nisije andika visivyo takiwa.
Hahahaha Waigizaji Watanzania Wanafanya Maigizo Ndani Ya Maigizo, Tuseme Sijuhi Wanaionaje Hii Kazi, Nani Atataka Kuweka Ela Zake Kwenye Undezi Wanaoufanya! Si Bora Ata Tuburudike Na Magizo Ya Viongozi Kuliko Wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…