aminas nimeamua nikuite huku kijiweni kwetu kama una nafasi au nawewe umebanwa na ratiba kiasi ambacho unashindwa hata kutembelea facebukiiiiii na twitteriiiii.
hivi ile amri niliokupa umeshaifanyia kazi?
lazima unapaswa ufahamu ya kwamba damushin huyu ni tofauti na yule aliyekuwa akivaa bendera ya nchi shingoni kwake.
damushin huyu wa sasa hivi bendera ya taifa ameishonea kwenye shati lake hivyo basi ndio ufahamu jinsi gani nilivyo mzalendo wa taifa hili la.
kwenye maisha hutakiwi kupangiwa unachokifanya, fanya maamuzi kutokana na moyo wako kama anavyofanya mpenzi wangu mtarajiwa bong sera. Anavaa anachokipenda iwe miwani, bangili.
nakukumbusha tena nimekupa amri uniletee namba ya simu ya huyu mdada kabla episode ya 16 haijaonyeshwa siku ya leo.
episode ya 14 ilikuwa ndio episode zaidi ya drama hii.
hii drama natamani iongezwe episode 10 zaidi ili nipate kufaidi uhondo wa team work.
sielewi kwanini huyu bonge hana mchumba humu ndani.