Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Duh haya bwana sijui kwa nini moyo wangu bado hautaki kuamini
 
Mara Ya Mwisho Kuangalia Kdrama Ilikuwa 2015, Naomba Kuuliza Hivi Wakorea Wamefanikiwa Kutengeneza Historical KDrama Kali Kuliko JUMONG?? Sijafanikiwa kuiona SIX FLYING DRAGONS ila sidhani kama ni kali kuliko JUMONG
Six flying dragon ni kali balaa kila nikitafuta korean drama nkajua itafanana na Jumong au six flying dragon siiendelezi.
 
Hivi hii IRIS huwa inaonyeshwa siku gani hadi siku gani? Maana hadi sahv nimeganda tu hawajaonyesha
ITV mnatakiwa muheshimu matakwa ya Wateja wenu.Sasa hivi mlitakiwa muonyeshe IRIS lakini sijui mnarusha kipindi gani.Hebu acheni uswahili basi!
 
Uandishi mkuu unashabihiana sana
Uliposema kuwa kuna mshabihiano wa kiuandishi nikasema 'isiwe tabu' ngoja niurudishe huu uzi nyuma ili kupata kuyashuhudia mwenyewe hayo unayoyasema mkuu maana kuna msemo unasema; "Lisemwalo lipo na kama halipo, linakuja na kama bado halijafika basi huenda limepotea njia".

Baada ya kurudi nyuma na kuzisoma vyema taarifa na mabandiko kadhaa ya ndugu Daemusin na aina ya uwasilishaji wake, naweza kusema kwamba; You have a point! na huenda kweli kuna mshabihiano wa kiuandishi kutokana na matumizi ya aina fulani hivi ya uwasilishaji taarifa yenye burudani ndani yake.

Lakini hii nadhani ni aina fulani ya uwasilishaji wa taarifa utakaomvutia msomaji kukifuatila na kukielewa kile kilichoandikwa bila kujali msomaji yuko katika hali gani; hasira, furaha, huzuni, msongo wa mawazo, kukosa fedha, kukosa chakula, kukosa mke au mume, kukosa usingizi n.k.

Katika maisha sikuzote ni jambo jema sana mtu kuwa ni mwenye furaha wakati wote na moja ya kazi kubwa za Tasnia ya Burudani ni kuhakikisha kwamba watu wanaburudika ikiwemo pia kuwafanya wawe na furaha ili waishi maisha marefu (kwa mujibu wa tafiti za kisayansi) na ndio dhumuni pia la kuitumia aina hii ya uandishi katika jukwaa hili la Burudani ama Entertainment.

Nimezipitia taarifa na mabandiko yaliyopita hivi karibuni katika kipindi ambacho sikuingia katika huu uzi hususan mabandiko ya ndugu Daemusin bin Koroshow bin Makinikiyya (bin ziko kama mia hivi) na nimpongeze kwa aina yake ya uwasilishaji taarifa na jinsi gani unavyoweza kumfanya msomaji akaifuatilia taarifa na kuielewa huku akibaki kucheka mwenyewe kama 'chizi'.

Nimalizie hivi;
Maisha yamebadilika sana na ukitaka kuamini hilo, hapo kabla kulikuwa na kamsemo 'wahenga wa kisasa' walioko humu wanakakumbuka kanasema "Hata uoge vipi, mjini huendi". Ila siku hizi kuna mpya; "Kama hujaoga, usije mjini". Kweli maisha yamebadilika sana.

Nimemaliza.
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Siku yangu imeanza vizuri barikiwa
 
Flower in prison ni kali balaa nimeifatilia had episode ya 10 youtube duh!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…