Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Rookie Historian Goo Hae Ryung Daemusin Ost Zake Ni Balaa Hasa My Dream By Yoonmirae..
Bogoshipo Chingu Sana Sana.
Uje Basi Twende Busan.
jewel in the palace, dong yi, jang hee bin, jang ok jung drama.
zote hizi zilikuwa zinaelezea historia za wanawake ikiwemo mafanikio yao pamoja na changamoto walizokutana nazo ambazo baadae walizigeuza kuwa ni fursa, lakini ukiziangalia drama zote hizo kwa umakini simulizi zake utagundua ya kwamba kwa kiasi kikubwa sana watengenezaji wa project hizi waliendelea kumfanya mwanamke awe chini ya kivuli cha mwanamme kiutegemezi.

inanilazimu nikiri ya kwamba hizo project zote nilizozitaja hapo juu hakuna hata moja niliowahi kuiangalia hivyo basi kama nitakuwa nimeteleza kifikra na mtazamo basi nipo tayari kusahihishwa kwa lugha safi isiokera na mdau yeyote.

Rookie Historian Goo Hae Ryung drama nayo pia sijawahi kuifuatilia hata episode moja lakini baada ya kusoma maoni ya wadau mbali mbali kupitia vyanzo tofauti na kuangalia short videos nimejifunza ya kwamba hii ndio drama pekee ambayo imemuandika mwanamke kama ndiye muhusika mkuu halisi wa hadithi ukilinganisha na drama hizo hapo juu nilizozitaja ambazo kwa kiasi kikubwa mission nyingi zilikuwa zinafanywa zaidi na mwanamme.

  • goo hae ryung ndiye wa kwanza kuziweka wazi hisia zake za kimapenzi kwa mwanamme ambaye ni mtoto kutoka royal family,​
  • si hilo tu pia mwanadada ndiye wa kwanza aliyeanza kuonyesha uthubutu wa kutamani kumbusu (kiss) mwanamme, cha ajabu unapozifuatilia hizo drama nyengine zenye kutuonyesha ushujaa wa mwanamke zimejaribu kutuwekea ukomo wa matendo ya mwanamke anayopaswa kuyatenda kana kwamba ni dhambi kwa mwanamke kuyatenda matendo hayo jambo ambalo linamfanya mwanamke abebe sifa za parasite wa hisia (amsubiri mwanamme adhihirishe hisia zake ndipo naye afuate mkondo kama maji ya mto ruvuma)​
  • nyakati ambazo bwana mdogo anatengeneza mipango ya kumtokea hae ryung na bidada pia naye amekuwa akisuka mipango yake ya kutamani kuwa na mwana wa mfalme, ni nadra sana kuona mwanamke anaziweka wazi hisia zake za kimapenzi kwa mwanamme kuanzia kwenye maisha ya maigizo hadi kwenye maisha halisi labda kwa kuhofia jamii itamchukulia kama ni mwanamke asiyeiheshimu thamani yake.​
chingu, bado nipo kwenye mgomo wa kuingiza project mpya kwa sasa hivyo basi hii drama acha kwanza iende pengine huko mbeleni naweza kubadili msimamo.
 
Juzi Wakati Naiangalia, Nikakumbuka Ule Usemi Wako Na Hiki Ulichoandika Apa.

Naona Hadithi Za Maigizo Zinaenda Kasi na Dunia Inavyoenda.... Kuwapa Ujasiri Zaidi Wanawake.

Ila ni Drama yenye Stori Nzuri..
 
Wakuu dramania yng inafanya ivi nikitaka ku donwload ni zote au yng tu haliti chochote na hata uki lazimisha ina feli tu ni week ya 3 sasa
 
Kapo yenu iko lit mno.. Mwaendana!! Hope hayataishia humu
teh teh teh nimeona leo ndio siku nzuri kujibu hizi comment.
bwana davinci kwa mara nyengine tena umekalia ukuwadi juu yangu na aminas.

sidhani kama tunaendana kitabia kati yangu mimi babu mtarajiwa na huyu ahjumma mtarajiwa baada ya miaka 20 kwa sababu:
  1. anapenda simba sports club wakati mimi napenda ile timu kutoka mozambique a.k.a msumbiji inayoitwa UD Songo pamoja na yanga
  2. anapenda liverpool fc wakati mimi napenda man utd pamoja na everton fc.
  3. anampenda haji manara na maneno yake ya ovyo na hajiwezi kukaa bila ya kusoma comment zake wakati mimi nachukizwa na tabia zake anazoziwasilisha kwa njia ya uandishi (tabia za dharau na ujuaji mwingi)
  4. anajua kuzungumza kiingilishi wakati mimi hata kuandika barua rasmi kwa kiingilishi kunanipa tabu mpaka nitembelee gogoli.
 
Loo! Wakati King Goonyae( Sujong) yeye alilazimishwa na kwa nguvu mno kuoa, Jamaa alikuwa hapendi wanawake yule, alikuwa anahisi ni kama watu ambao wametanguliZa hisia badala ya mantiki.
alikuwa anajifanya maitreya (buddha mpya) kumbe ni mshenzi aliyekuwa anajificha kwenye kivuli cha dini.
huyo mjinga aliichoma moto familia yake hadharani akiwemo mke wake na watoto wake wawili mapacha.
baadae alikuwa mkatili sana ndio maana wafuasi wake wakaribu wakaamua kumpindua kwa kumtumia general wang guhn ambaye alimchukulia kama ni mdogo wake wa kupanga.
 
Msimulizi anadai huyo binti wa mfanyabiashara wa Geumsung ndiye aliyemzaa mrithi wa Wang guhn.
kwa mujibu wa drama mtoto wa kwanza kuzaliwa na wang guhn pamoja na mke wake wa kwanza alifariki dunia ndipo baadae mke wake wa pili ndio akafanikiwa kumzalia mtoto mwengine aliyeitwa wang mu a.k.a mfalme hyejeong.
bahati mbaya sana alifariki miaka miwili tokea afanikiwe kurithi madaraka ya baba yake.

mke wa kwanza baadae alijaaliwa kupata watoto takribani sita na miongoni mwa watoto hao yumo wang so ambaye baadae alikuwa mfalme wa nne wa goryeo.
 
@aminas kumbe tupo pamoja kwa Liverpool
 
Jamaa( Sujong) na mshikaji wake( Advisor) jamaa wanaonekana wakatili 100%, halafu maovu yao wanayaficha kwa kujichekesha kila mara, walinikera walipomuua Madam Bukwon( binti wa General Yangil), kiukweli hiyo miamba ilikuwa mikatili.
 
Kuna drama nipo sehemu ya pili yaani lifalme( King Seonjo) halijitambuii linashindwa kutambua kati ya mbwa na mbwa mwitu. Pia Wajapan hawa walikuwa watu wakatili na Joseon na Goryeo walikuwa wanapafanya kama kwao, shout-out kwa 'King Gwanggaeto the Great' naweza kusema ndiye mkorea mbabe katika history ya taifa hilo, maana Wajapan walikutana na balaa zito walipojaribu kuivamia Silla iliyokuwa Chini ya Serikali ya Gogryeo iliyokuwa ikiongozwa na Phantom of the North ( Tam Toek/Gwanggaeto the Great) nadhani waliogopa kufika maeneo yale maana ingekuwa balaa huko nchini kwao.
 
Ni pote. Mara ya kwanza nilipata hasara ya GB 10 maana nilijiunga kisha kuicheki dramania majanga tupu na sikua nafahamu sehemu nyingine ya kudownloadia movies
Wakuu dramania yng inafanya ivi nikitaka ku donwload ni zote au yng tu haliti chochote na hata uki lazimisha ina feli tu ni week ya 3 sasa View attachment 1189916
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…