Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

punguza bangi mjukuu wangu...
kila siku natumia kissasian kupakua drama, sielewi kiupande wako inagomaje..
hebu tiririka kwa sababu gani zinakugomea?
Acha majungu mzee baba mambo ya mjukuu yametokea wapi?by the way imekubali sasa hiv mwanzo ilikuwa na id nyingi ukitaka kudownload.
 
kuzungumza na kupanga(budgeting) ni tofauti kabisa na kutenda mjinga weweee.....
bahati mbaya watanzania wanavutiwa zaidi na mazungumzo kuliko matendo ndio maana wanajazana zaidi kwenye viwanja vya kampeni kuliko siku za uzinduzi wa miradi ya kimaendeleo.

kazi kwako muhuni weweee
  • either uwaondoe watanzania kwenye upofu wa kupenda mazungumzo kwa kuwatafutia tiba itakayoweza kuwasahaulisha jinamizi hilo
  • au uzidi kuwazamisha kwenye upofu huo kwa kujiweka mbali na filamu za siasa.
2020TwendeNaDaemusin
Juzi nilimsikia mwanasiasa mmoja akisema Watanzania ni washamba ndio maana wanajazana pale JK. Nyerere kwenye kupokea......
😁😁 Wanashindwa kujazana kwenye uzinduzi wa miradi ya maemdeleo sababu wanahofia kuitwa washamba. Hahaha Sometimes tujiulize Je! Haya maji machafu chanzo chake ni wapi na si kung'ang'ana kuyatoa wakati hujatazama chanzo.

Je wapo tayari kujifunza?.
Huwezi kujua kusoma kama hupendi kusoma (All learning starts with interest and Genuine) kwahiyo kabla ya kumfunza mtu lazima ajifunze namna ya kujifunza.

hahaha Karibu sana Pyeongyang.
 
Kijana MB zangu,SIMU yangu,Usingizi wangu na bado kiherehere cha kujua kilichomo ni changu. Huwa sina kawaida ya kuuliza uliza,navuta naangalia,kama mbaya naangalia mpaka mwisho kisha nalaumu kupoteza mb na muda inaisha ili mradi nimemaliza ile hamu ya kuiona movie husika

Jifunze kuishi bila maoni ya watu sio kila maoni ni mazuri,mengine yatakukosesha uhondo.
Ina maana hiyo jackpot umeangalia bila kusikiliza maoni ya wana Kama ni nzuri au la?Me binafsi siwezi kuangalia drama yoyote bila maoni ya watu kwanza.
 
Kwa umri wake ni first born wa mwanagu kabisa(ukubwa raha sana) huyo hajiwoni mbona sio mzuri kivileeee bora suzy,kim nana(jina lake halisi sijalishika)

Ila kijana ananifurahisha akiwa anga hizi na kule celebrity
weweeeee umesahau ya kwamba ahjumma ha ji won nimemchagulia mimi babu yake.
acha kumpotosha mjukuu wangu asiyetaka kukitambua cheo changu.
 
Hahaha aiseee hapa nasubiria amalize VIP aje aulize uzuri wa movie nyingine,sijui itakua ipi hio

My next target

Stove league
Crash landing on you
Queen love
Black dog
Diary of prosecutor

Aah wanazichelewesha,baadhi zingekua zimeshaisha
power of love
love doesn't ask why


mjukuu ameniambia hapendi wasichana anaolingana nao kiumri kwa sababu wana fyoko fyoko nyingi zinazodi umri wao...

honey nataka sabuni anayokogea beyonce
honey nataka mswaki wa bamboocha
honey nataka gari ya lamborghini

kwa mujibu wa maneno yake anadai wazee hawana fyoko fyoko nyingi... wao shida yao ni paketi la sigara na ndoo ya sabuni ya unga
 
Hahahaha aiseee hapo kwa huyo handsome umenitamanisha pamoja na kwamba umempondea balaa ila nimejikuta naipenda,muhimu sana kuiangalia hii

Kuna movie ya the liar and his lover(sijui nimepatia jina,hii imenishinda kabisa kuiangalia,bahati nzuri nilivuta episode 2 tu) hio black dog ntaenda nayo hivyo hivyo.
black dog : ilinishinda njiani tokea episode 4 (niliamua nipambane na diary of prosecutor kwa lengo la kupunguza ulevi)

queen love: nimeipotezea kwa sababu ya lead actor (wangelitafuta matured actor ningelipoteza muda wangu, ukiangalia supporting actors hususani wazee wapo vizuri sana)

mwanamme amejaa dimples mashavuni utadhani andazi la bakhressa.
ananifanya niwe uncomfortable kama mdogo wako meok goo anaponyimwa fedha ya kununulia bakuli la wali na gavana
akinuna dimples
akicheka dimples

wengine dimples zetu zimeingia ndani zaidi kama vishimo vya kuchezea gololi
View attachment 1344569
 
1 mpaka 4 nitasubiria ziishe ili nizivute vizuri,namba 5 sijawahi kuiwaza na 6 kama ni criminal iniepuke sipendi presha mie

Hizo za 2019 nazisubiria kwa hamu ziishe nifaidi kilichomo maana ongoing moja tu inanipa tabu mpaka march 2020
teh teh teh
huu mwaka nisipokuwa makini huenda nitavunja rekodi ya kuangalia drama, nimekusudia nipunguze tena dozi ila huenda ikaongezeka zaidi..
kila drama niliyojaribu kuiangalia kwa mwaka 2020 basi inaleta vishawishi ya kuendelea nayo:

ewe Mungu weeeee bora wamarekani watuwekeee vikwazo vya kutokuangalia wakorea ili wengine tuhamie kwenye siasa tukapate pesa za kufidia hasara ya bandow

2020 KOREAN DRAMA
  1. touch drama (hii sijawahi kuiangalia na sina mpango huo)
  2. money game drama (bonge ya vita inayohusu pande mbili zinazotofautiana kisera za kiuchumi, maisha yote taifa linapo ongozwa na wachumi uchwara hutumbukia shimoni, ngoja tuone jinsi gani hii nchi itakavyojiokoa na second IMF crisis kama ilivyokuwa 1997)
  3. itaewon class drama (hii imeanza ijumaa na episodes mbili za mwanzo zimenitia mzuka, inaakisi uhalisia wa maisha wanayopitia vijana wengi wasiokuwa na nguvu, mpaka wanapofanikiwa kimaisha wanajikuta wanapitia changamoto nyingi sana zenye kuumiza tofauti na kelele za bongo zozo zisizoumiza )
  4. romantic doctor kim season 2 (mpambano umezidi kuwa mkali humu ndani, watamuangusha huyu daktari genius? hata sijui bwanaaa)
  5. forest drama (hii sijaiangalia mpaka muda huu ila episode zote ninazo, sielewi kwa nini hii drama inachelewa kuwekwa subtitle, huenda viki hawana haki ya kuitafsiri hii project) Itapendeza zaidi kama project hii itakuwa ni mbayaaa ili ulevi upungue.
  6. tell me what you saw drama (imeanza jana na ndio project ya mwanzo ya OCN kwa mwaka huu kama nitakuwa nipo sahihi, wazee wa criminal, thriller and action. Jang hyuk amerudi tena akiwa ni genius criminal profiler). Nimeshaihifadhi episode 2 muda huu japokuwa haina subtitle
2019 KOREAN DRAMA
  1. Crash landing on you drama (imebaki episode 4 kumalizika)
  2. stove league drama(imebaki episode 3 kumalizika): natamani man utd tuajiri mtendaji mwenye sifa kama za huyu jamaa wa humu ndani ili atuokoe na huu mkwamo.
  3. diary of prosecutor drama (imebaki episode 4 kumalizika) : (hivi ni nani aliyekwambia ya kwamba waendesha mashitaka ni malaika? : prosecutors wanacheza kamari wakiwa ghetto then wakirudi ofisini wanaanzisha kampeni ya kutafuta magenge ya wacheza kamari... hivi hii ni haki? ukitaka kufahamu maisha ya kila siku ya hawa mabwege wanaofunga watu basi itafute hii drama... kumbe hawa mabwege wanakwenda chooni kama sisi watuhumiwa watarajiwa
 
Halafu wa kwanza kulalamika maisha magumu mara mishahara midogo ila kwenye kunywa wanasahau hilo,kila saa ofa za msosi au pombe. Mabingwa wa kushika mikasi ya kukatia nyama,kuagiza kuku
wakorea wanapenda kula
wakorea wanapenda kupeana offer ya vinywaji
wakorea hawawezi kunywa pombe bila ya nyama choma
 
Halafu wa kwanza kulalamika maisha magumu mara mishahara modogo ila kwenye kunywa wanasahau hilo,kila saa ofa za msosi au pombe. Mabingwa wa kushika mikasi ya kukatia nyama,kuagiza kuku
Naona leo mmetengeneza kikao Chenu cha majungu na uchochezi na mwenzako Daemusin kwa ajili ya kumzungumzia Mume halali wa Ha ji won Innocent dependent me nawaangalia tu ila nimependa kitu kimoja kwenye kikao Chenu mmenipa na drama za kuangalia maana sasa nimekomaa na drama zangu VIP pamoja na Woman of 9.9 billion nikizimaliza hizi nakuja huko.
 
Wakorea naomb niulize instant noodles kwa kwet n chakula kipi,

na soju kwa bongo tutaifannsha n bia gan, je manufacturer wake n mmoja nationalwide?

Asante[emoji1374]



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Instant noodles kwetu ni Tambi,sema sie tumezoea tambi za aina moja(santa nanii) ila ukienda supermarket zipo za aina nyingi.

Soju kama k vant,konyagi etc(huwa wanakunja sura kwa ukali wake). Maana naona wanalewa zaidi kuliko wakinywa bia za kawaida
Wakorea naomb niulize instant noodles kwa kwet n chakula kipi,

na soju kwa bongo tutaifannsha n bia gan, je manufacturer wake n mmoja nationalwide?

Asante[emoji1374]



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Soju is a clear, colorless distilled beverage of Korean origin. It is usually consumed neat, and its alcohol content varies from about 16.8% to 53% alcohol by volume. Most brands of soju are made in South Korea.

Soju, a Korean variation on vodka traditionally made from rice but more commonly from sweet potatoes these days. With 24% alcohol, soju is stronger than beer (4% to 5%) or wine (about 13%) but packs a weaker punch than virtually all vodkas, which are 40% alcohol.

Soju is, at it's most basic, a clear, 20-24 percent alcohol by volume spirit. It's from Korea, and is mostly consumed in Korea, Japan, and China. Soju is neutral-tasting like vodka, but doesn't have the harsh alcohol burn thanks to having around half the percentage of alcohol.

The Taste of Soju
Soju has a clean, neutral taste that makes it a good accompaniment to Korean food or Korean snacks. People often say that the taste reminds them of vodka, but most commercial soju sold today has a sweeter and less aggressive flavor than vodka.
 
Back
Top Bottom