mwishoni mwa episode 20
lady min (mke wa bang won) na kabila lake(min clan) ni suala la muda tu kabla na wao hawajaingia kwenye mdomo wa mamba, bang won amekuja na mkakati wa kuondoa vikosi binafsi vya ulinzi vinavyomilikiwa na makabila pamoja na familia maalum(tumeona huko nyuma mfalme taejo aliwatunuku wanawe wanajeshi kwa ushauri wa malikia aliyekuwa na lengo la kuwatengenezea mazingira ya kupumbazika na kufanya uhaini). hapo nyuma sambong alikuja na wazo la kufuta wanajeshi binafsi(military disbandment) lakini akapata upinzani mkali kutoka kwa lee bang won, leo hii bang won anataka kupita mule mule alimopitia adui yake sambong ndio maana kabila analotokea mke wake hawamuelewi juu ya mpango wake huo na khofu yao bila ya shaka wanaamini kutokuwa na majeshi ya kulinda kabila lao ni sawa na kuchomolewa maarifa na ufahamu kwenye vichwa vyao na watakuwa chawa wa mfalme milele, wakati baba mkwe dhumuni lake haswa ni kuitawala joseon kupitia sketi ya mwanawe wa kike (wanaume wa scotland nao wanavaa sketi) huku wakipata msaada wa kiulinzi na kifedha zitakazowawezesha kutawala nafasi zote nyeti za kiserikali.wakati yeye anawaza hivyo upande wa pili anaamini kwenye uendeshwaji wa serikali itakayoongozwa na nguvu ya mtu mmoja (hata kuwa kama baba yake aliyetawaliwa zaidi na sambong pamoja na malikia sindeok). lady min anamwambia bang won nyakati za shida tulikuwa pamoja, tulicheka pamoja pale tulipopatwa na jambo la kufurahisha, tulikejeliwa na kudhihakiwa pamoja. leo wachukua maamuzi muhimu ya kuongoza nchi peke yako, kama huwezi kuishawishi familia yangu juu ya mpango wako wa kuondoa majeshi binafsi basi nishawishi mimi, utakaponishawishi mimi ni sawa na kuwa umeishawishi familia yangu. hivi umesahau kuwa nusu ya mafanikio yako yametokanwa na mimi(akiwa na maana ya kabila lake).aigooo marehemu khadija baramia aliwahi kuimba wimbo wake wa taarab asilia..... njoo njoo mpenzi wangu njoo, rudisha yako imani wachochea moto ukija kuwaka mzimaji nani, eti lady min?....umeshasahau kuwa mume wako amewaua ndugu zake, amemfungia baba yake na kumuondoa ndani ya mji kaka yake. mara hii atazitafuta shingo za ndugu zako wawili na baba yako..... nilifikiri naongea na lady min. kumbe naongea na mkorea wa makunduchi. basi naambatanisha na samahani isiyoonyesha kujutia kosa langu.
The King of Tears Lee Bang Won, ni moja ya drama nzuri sana. Inafaa sana kina dada na kina mama muitizame hii drama. Katika drama hiyo inaonyesha vile mwanamke anapaswa kumsimamia mume wake katika nyanja nyingi mno, kiushauri na ata kumpambania mume wake ili atimize ndoto zake. Bonge la drama kwakwel. View attachment 2164877
Boooonge la drama, akili kubwa tupu zinatumika humu!
Yote uliyoyasema ongezea na sapoti. Unajua mwanaume anaweza kuwa anataka kufanya jambo kubwa la manufaa ila akasita au lah akapingwa na watu wengine… hapa ndipo inapohitajika sapoti ya mwanamke wake!
Nimekuwa inspired sana na ushupavu wa Queen Sindeok na Lady Min, sana sana!
ndio mwanzo wa kuvurugika kwa mahusiano yao ya kindoa na kiukoo, kwa mujibu wa maandiko lee bang won atawaua hao kaka zake wawili ambao wamekuwa msaada mkubwa sana katika kampeni ya kufanya mapinduzi, baadae watatofautiana kwenye urithi wa madaraka ya bang won, lady min na ndugu zake wengine wawili walimpigia kampeni mtoto wao wa kwanza awe mrithi wa madaraka wakiamini ndiye atakayeweza kurudisha mahusiano yaliofifia kati ya pande mbili hizo, taarifa za bang won za kutaka kuachia madaraka ziliwapa bashasha na furaha hao ndugu jambo lilimughadhibisha taejong, akawapa adhabu ya kuwatekeleza nafikiri na hao wawili wengine pia aliwauaKweli Lady Min ana mchango mkubwa kwenye mafanikio ya mumewe Bang Won ila sio kama anavyotaka! Ati nusu ya Joseon ni mali yake? Ujinga mtupu anaojazana na baba yake.
Huu ni mtihani mwingine ambao natamani kuuona Bang Won atauvuka vipi?
Bado baba yake (Bang Won) aliyepata ruhusa ya kuondoka kwenye palace alikowekwa kizuizini na Bang Won, je huko nyumbani kwao alikoenda atatulia tuli bila kulipiza kisasi?
Mwanzoni alipokweka kizuizini alijaribu kumtumia swahiba wake Ji Ran kufanya shambulizi la kulipiza kisasi Ji Ran akagoma…
Naisubiri kwa hamu ep 21 na 22!
uzuri hiyo drama imebase na historical events, natumai watatuonyesha upande wote wa bang won mpaka kuondoka kwake. kama utakuwa na mzuka baadae itafute the great king sejong drama. huyo mzee kim young chul aliyeigiza yi seong ye ndiye ameigiza uhusika wa lee bang won. utamchukia
Zimetajwa juu hapo tu...rudi page ya nyuma kama hazipo page hiiMwenye list ya romantic drama zile ambazo mwanzoni wahusika wanakua maadui alafu mwishoni wanapendana naomba anitajie tafadhali!
ndio mwanzo wa kuvurugika kwa mahusiano yao ya kindoa na kiukoo, kwa mujibu wa maandiko lee bang won atawaua hao kaka zake wawili ambao wamekuwa msaada mkubwa sana katika kampeni ya kufanya mapinduzi, baadae watatofautiana kwenye urithi wa madaraka ya bang won, lady min na ndugu zake wengine wawili walimpigia kampeni mtoto wao wa kwanza awe mrithi wa madaraka wakiamini ndiye atakayeweza kurudisha mahusiano yaliofifia kati ya pande mbili hizo, taarifa za bang won za kutaka kuachia madaraka ziliwapa bashasha na furaha hao ndugu jambo lilimughadhibisha taejong, akawapa adhabu ya kuwatekeleza nafikiri na hao wawili wengine pia aliwaua
(sina uhakika). bang won aliongeza mke na inasemekana lady min akawa anamtesa huyo concubine, pia lady min alizaa mtoto mwengine wa kike na hakumtaarifu mume wake jambo lililozidisha ghadhabu na inasemekana bang won alimsusia mkewe.mwishoni bang won akamuachia madaraka mtoto wake wa tatu(mfalme sejong the great) badala wa kwanza kama kumkomoa mke wake na ukoo wao. licha ya kumuachia madaraka mtoto wake lakini bado aliendelea kuwa remote kuu ya serikali ndio maana si ajabu akamuua baba mkwe wa mtoto wake. bang won alikuwa ni mshenzi mwenye uelewa mkubwa wa siasa na diplomasia.
uzuri hiyo drama imebase na historical events, natumai watatuonyesha upande wote wa bang won mpaka kuondoka kwake. kama utakuwa na mzuka baadae itafute the great king sejong drama. huyo mzee kim young chul aliyeigiza yi seong ye ndiye ameigiza uhusika wa lee bang won. utamchukia
Nalipataje hilo file jipya..majanga yamezidiNdio yangu iligoma nikaenda upya telegram kuvuta file hilo hilo nikaongeza sh 20 ikakubali kudownload. Jaribu kulivuta file upya weka ka pesa kidogo inaweza kukubali
Why unateseka na hizo file wakati kuna kitonga Tigo townNalipataje hilo file jipya..majanga yamezidi
Nalipataje hilo file jipya..majanga yamezidi
Unazingua mkuu, watu mkoje lakini?Kwa wale tuliokua tunafatilia young lady and a gentleman nadhani tutakua tumeridhishwa na bonge moja la happy ending!
Tutammis sana ms wang,sejong na dan dan wa kulia lia[emoji23]
Lete makitu..kwa sasa nimerudi kwa Wire Tun japo mwendo wa kobe ila nimefanikiwa kupata episode 3 za Love in the moonlightWhy unateseka na hizo file wakati kuna kitonga Tigo town