Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

hili andiko lako nimelirejea kulisoma mara nne ndipo angalau nikapata cha kukujibu, kiukweli hili andiko limenifanya muda huu niitafute episode ya 11 hadi ya 15,wakati asubuhi nilisema nataka niiweke kiporo sasa kwa huu ushawishi wa andiko lako kwa nini nisikuite sunbaenim?
kiukweli nimevutiwa zaidi na urafiki wa tokea utotoni kati ya ryu seung ryong, yi soon shin na won kyun. huyu ryu seung ryong baadae anakuja kuwa na nyadhifa mbali mbali kwenye utawala wa mfalme seonjo na kwenye vita ya imjin war alishika nyadhifa ya waziri wa ulinzi na ndie aliekuwa akimpa support kubwa sana yi soon shin. baada ya kuona mfalme seonjo amekuwa na hofu na yi soon shin aliamua kuacha shughuli za kisiasa, kama sikosei episode ya 3 ya drama hii anaamua kupeleka barua ya kuacha kazi kwa mfalme seonjo.
Hahaaa Damushin Sunbae unavituko ww sasa hapo kuna ushawishi gani.? Yah, walipendana sana toka utotoni japo mwanzo walimnyanyapa sana kutokana na kuwa muoga na aliye kuwa anaonekana hajui kitu. Mpaka yule rafiki yake mwingine akawa nae bega kwa bega na kuhakikisha anajisikia amani na furaha kama wenzake. Kinacho nifurahisha ni yule rafiki yake aliyekuwa akimtenga baadae akaja kumuelewa na kushika urafiki imara sasa wakawa watu watatu Hahaa.

Bado najiuliza ile risasi iliyo mpata Admiral Yi Soon Shin kifuani je, ilimfanya akapoteza uhai ama ilikuwaje? Na je, ile series inaanza katika vita zile zilikuwa vita za mwishoni ama? Na inamaana baada ya kuanza kuona maisha yake inamaana mbeleni tutaenda alafu tufike pale tulipo komea kwenye tukio la Admiral Yi Soon Shin risasi inampata?
 
Damushin Sunbae bila kupoteza mda ikiwezekana kesho naishusha hii Drama The book of corrections Jingbirok. Mkuu kuna andiko hapo page za nyuma umeshuka mpaka nimekuogopa aisee.
 
Hahaaa Mkuu UHURU JR kuna Drama kama Tatu nazisubiri kwa hamu kubwa sana aisee.

RADIO ROMANCE
186f1e91cea39b06136a27af588e56b1.jpg
Ni moja kati ya Drama tatu ninazo zisubiri kwa hamu sana. Kinacho nafanya niisuburi kwa hamu kubwa namna hiyo ni huyo Mdada Song Geu Rim natamani nione kipaji chake kilivyo kikubwa hasa upande wa hizi drama za Romance. Nilivutiwa nae kwenye ile Drama ya While you were sleeping Mdada huyu alinivutia sana. Nataka nione humo ndani amefanya nn baada ya kuaminiwa na kupewa nafasi. Pia nataka nione Kijana Ji Soo Ho kafanya nn humo ndani baada ya kucheza kwa umaridadi mkubwa katika Drama ya Because this is my first life. Hizo sababu zinafanya niisuburi kwa hamu na shauku kubwa mno. Radi Romance itakuwa hewani kuanzia Tarehe 29 Januari na itakuwa ikirushwa kila Jumatatu na Ijumanne katika kituo cha KBS 2.

MR. SUNSHINE
6e384f28b45e22473baa76d94959f47e.jpg
Sababu kuu ya kuisubiri ni kutokana na huyo muhusika mkuu Lee Byung Hun. Huyo Mkuu Binafsi sijabahatika kutizama Drama yake yoyote baada ya ile ya IRIS 1, huenda zipo tu nyingi lakin sijataka kuzitafuta. Kwahiyo hicho kitendo cha kukaa mda mrefu bila kutizama drama yake yoyote hasa ukizingatia kwenye IRIS 1 alitulia vizuri mno ndio kinanifanya niisuburi kwa hamu nijue kaja kivip tena. Wanadai itaanza kuonyeshwa kati ya Juni ama Julai kwenye kituo cha tvN.

ARE YOU HUMAN TOO?
f788a8054ef1c0d23aa7ef571daa956e.jpg
Hahaha drama ya mwisho ninayo isubiri kwa hamu ni hiyo. Kinacho nifanya niisuburi ni jina lake. Hahaa jina lake tosha Mm linafanya niisuburi kwa hamu kubwa mno.

Mkuu UHURU JR kwangu mm hizo ndio Drama ninazo zisubiri kwa hamu na shauku kubwa. Ngoja kina Damushin Sunbae, EMPTY, aminas, Prishaz na wengineo watakuja wakujuze ni drama zipi wanazo zisubiri kwa hamu.

mjr95.

Ah! mwenzio hapa sijui nimejichanganya nini nikaanza kuitafuta drama moja hivi niidownload inaitwa Misty ,basi kila niki search siioni hadi kwenda kutizama vizuri kumbe inatoka Feb 2 ipo kwenye list yangu ya drama nazozisubiri kwa hamu.
 
Ah! mwenzio hapa sijui nimejichanganya nini nikaanza kuitafuta drama moja hivi niidownload inaitwa Misty ,basi kila niki search siioni hadi kwenda kutizama vizuri kumbe inatoka Feb 2 ipo kwenye list yangu ya drama nazozisubiri kwa hamu.
Hahaaa kweli leo umepatikana haswaa. Vp ni nzuri ili niongeze katika lisiti yangu pia.
 
Damushin Kuna Kitu Nakifatilia Kuhusu Nyuma Ya Kpop Coz Hii Ndo Nimeona Watu Wengi Wanaongelea Tofauti Na Kdrama.
Kuna Madudu Sana Kwenye Hii Kitu
Kweli Kila Penye Nzuri Kuna Bays.
aminas noona kwa ajili yako imenibidi nami leo nianze kufuatilia habari zinazohusu tasnia ya muziki wa kpop ili nami nipate kujifunza yalio nyuma ya pazia.
kwa kuanza nimeona niweke habari hii ilioripotiwa mwezi march 2017 na mtandao mmoja maarufu unaoandika habari za korean entertainment. ninaomba radhi kwa tafsiri isiyo rasmi ya kiswahili, hii lugha ya kiingereza huku kwetu pwani imekuja kwa majahazi ndio maana imezidi kuwa ngumu kuielewa.
niliwahi kukutana na mzungu akaniuliza
what is your name?
nikamjibu: your name is Damushin
aigooooo kupatwa kwa kiingilishi
nikipita wasaa nitaweka kila nitakachokiona kwenye mtandao ambacho hakivunji sheria na utamaduni wa mama Tanzania.

8 Major Entertainment Companies Face Reforms In Unfair Contract Clauses
takribani makampuni 8 yanayojishughulisha na masuala ya sanaa nchini korea yamegundulikana kuwa yameingia mikataba ya kitumwa (slave contract) na waliowaajiri (trainees)
taasisi ya Korea Fair Trade Commission (KFTC) walifanya uchunguzi wao kupitia makampuni 8 yanayokadiriwa kumiliki asset zenye thamani ya zaidi ya won 12 billion (takribani $10 million).
na kuamua kuvirekebisha vifungu sita vya mkataba ambavyo havimpi haki muajiriwa.
baadhi ya makampuni yaliotajwa ni pamoja na SM Entertainment, YG Entertainment, JYP Entertainment, Loen Entertainment, FNC Entertainment, Cube Entertainment, Jellyfish Entertainment,na DSP Media.

baadhi ya vifungu vilivyobadilishwa
  1. adhabu kubwa kwa mwenye kuvunja mkataba :kwa mujibu wa KFTC makampuni makubwa kama vile SM entertainment, JYP entertainment na mengineo wameweka kifungu cha sheria kinachomtaka yoyote atakayevunja mkataba wake basi anapaswa kulipa gharama mara mbili au tatu zaidi ya gharama zilizotumika katika kumsimamia muajiriwa,kwa kuzingatia mkataba wa kawaida ni takribani miaka mitatu inakadiriwa adhabu itakuwa si chini ya won million 150($130500).KFTC wao wametoa mapendekezo ya kivungu hicho kibadilishwe na kwamba trainee atakayevunja mkataba basi anapaswa alipe kiasi cha gharama zilizotumika katika kumhudumikia.
  2. kuwalazimisha wasanii kuongeza mikataba yao baada ya mkataba wa mwanzo kuisha muda wake:JYP Entertainment, Cube Entertainment, na DSP Media wamekuwa wakiwalazimisha wasanii kuongeza mikataba yao au kuwalazimisha kulipa mara mbili ya kiwango cha pesa walichowekeza juu yao.KFTC kwa upande wao wamebadilisha kifungu hiki na kuzitaka kampuni zinazojoshuhulisha na masuala ya burudani kufanya mazungumzo ya awali na wasanii pindi mkataba unapomalizika.
  3. makampuni kuwa na mamlaka ya kuvunja mkataba bila ya kumpa taarifa au kumshirikisha muajiriwa:kifungu hiki kinawapa mamlaka makampuni kuvunja mikataba na waajiriwa wao bila ya kumshirikisha muajiriwa, kifungu hiki kimebadilishwa hivyo basi pande zote mbili zina mamlaka ya kukaa pamoja na kusuluhisha mgogoro.miongoni mwa makampuni ambayo waliweka kifungu hiki ni pamoja na Loen Entertainment, YG Entertainment, Cube Entertainment, JYP Entertainment, na DSP Media.
  4. kuvunja mkataba bila sababu maalumu (ambigous reason): kifungu hiki kinawaruhusu makampuni kuvunja mikataba na wateja wao bila ya sababu zilizowazi nacho pia kimeondolewa,miongoni mwa makampuni ambayo waliweka kifungu hiki ni pamoja na SM Entertainment, FNC Entertainment, na DSP Media
  5. kuwalazimisha trainees kulipa adhabu au faini kwa haraka:kifungu hiki nacho kimebadilishwa juu ya ukiukwaji wa mkataba ili kufuata na kulinda haki za kiraia za nchi ya korea.
 
Song Seung Heon And Liu Yi Fei Confirmed To Have Broken Up
wawakilishi wa muigizaji song seung hun leo hii wamethibitisha taarifa za mteja wao kuachana na muigizaji mwenye asili ya nchini china anayejulikana kwa jina la liu yi fei.
ni kweli wameachana na suala hilo ni lao binafsi na sisi hatujui sababu zilizowapelekea kuachana.
wawili hao walitangaza mahusiano yao mnamo mwaka 2015 baada ya kukutana pamoja kwenye movie inayokwenda kwa jina la Third love.

8684f963-2db9-4e51-9fff-87c7a7686fa8.jpg

NB:
huyu dada nilimpenda kwenye movie ya forbidden kingdom,nimeanza kumuogopa Khantwe noona haiwezekani wapinzani wake wote wanaachwa solemba ila yeye bado anabaki kupendwa.
why always khantwe.
film__4435-the-forbidden-kingdom--hi_res-cf6be1fe.jpg

hahahahaaaaa nimecheka sana nilipokuwa nasoma statement ya agency wa song seung hun pale aliposema wawili hao sababu ya kuachana haihusiani na THAAD.
THAAD imeleta mgogoro mkubwa sana kati ya China na Korea jambo ambalo limesababisha China kupiga marufuku masuala yote yenye kuhusu utamaduni wa korea kusini.
 
Hahaaa Damushin Sunbae unavituko ww sasa hapo kuna ushawishi gani.? Yah, walipendana sana toka utotoni japo mwanzo walimnyanyapa sana kutokana na kuwa muoga na aliye kuwa anaonekana hajui kitu. Mpaka yule rafiki yake mwingine akawa nae bega kwa bega na kuhakikisha anajisikia amani na furaha kama wenzake. Kinacho nifurahisha ni yule rafiki yake aliyekuwa akimtenga baadae akaja kumuelewa na kushika urafiki imara sasa wakawa watu watatu Hahaa.

Bado najiuliza ile risasi iliyo mpata Admiral Yi Soon Shin kifuani je, ilimfanya akapoteza uhai ama ilikuwaje? Na je, ile series inaanza katika vita zile zilikuwa vita za mwishoni ama? Na inamaana baada ya kuanza kuona maisha yake inamaana mbeleni tutaenda alafu tufike pale tulipo komea kwenye tukio la Admiral Yi Soon Shin risasi inampata?
wenyewe wanaita flash back kama sijakosea, admiral yi soon shin kifo chake kinatokana na kupigwa risasi kwenye vita ya noryang na bila shaka pale ndio itakapokuwa mwisho wa yi soon shin kwa sababu sidhani kama risasi ile itamfanya apone.hivyo basi maisha yake ya mwisho kabla hajakutana na muumba wake tumeshayaona.
We are at the height of battle. Don't let anybody know about my death!
moja kati ya maneno yake ya mwisho kuyazungumza wakati anapigania uhai wa maisha yake baada ya kupigwa risasi.
 
Eeeh! Mola.
Mi nimedownload Kipindi Cha Ye Huiyeol Sketchbook Special Summer Episode
Umo ndani Ameunganisha Zile Best Ballad,Akiwemo Hyoshin,IU,Taeyon, Lee Juck Ailee, Urban Zakapa,Oh hyuk Na Wengine Kibao Basi Hii Nikilala Ipo Maskioni Nikiamka Ipo Maskioni Mpka Baadhi Ya Nyimbo nimeaza Zishika.

Uyu Oh Hyuk Ana Sauti Flani Ivi Dah!!!
nilibahatika kuiangalia ile episode,ailee kivazi chake alichovaa hmmmmm ila wimbo wake wa
I Will Go To You Like the First Snow
alioimba umetumika kama ost kwenye drama ya goblin.
wasanii wa kiafrika itawachukua muda sana kupata pesa yangu kwa kisingizio cha kuangalia shoo zao, haiwezekani nilipie pesa yangu halafu uniambie mikono juu kila wakati, mara machizi piga keleleeeeeee.
 
jamani hii likizo kwangu mimi itawezekana?
EMPTY dongsaeng umenifanya leo hii kwa hamu yako ya kuisubiri drama ya mother umesababisha niidownload episode 1.
nimejiwekea nisifuatilie drama yoyote mpya isipokuwa viporo vyangu tu na going on kama money flower, hwayugi na black knight ila naona naelekea kushindwa.
DSpz-N9VoAAaXSV.jpg

mungu jaalia hii drama iwe mbaya mnoooo ili niachane nayo
aaaaaameeeeeeennnnnnnnnn.
 
pale unapojikuta unawasifia lady jay dee, shilole,vanessa mdee na wengineo eti wanajua kuimba na kuacha kumsifia mwanadamu kama huyu kwa kisingizio cha uzalendo.acha tu niendelee kutokuwa mzalendo na nipo tayari kupokea hata adhabu ya bakora 100 kwa kosa la kutokufuatilia muziki wetu.
aminas noona sijui nishawahi kukusifia huyu kiumbe anayeitwa so hyang?
b6f5bf65fa0.jpg
 
jamani hii likizo kwangu mimi itawezekana?
EMPTY dongsaeng umenifanya leo hii kwa hamu yako ya kuisubiri drama ya mother umesababisha niidownload episode 1.
nimejiwekea nisifuatilie drama yoyote mpya isipokuwa viporo vyangu tu na going on kama money flower, hwayugi na black knight ila naona naelekea kushindwa.
DSpz-N9VoAAaXSV.jpg

mungu jaalia hii drama iwe mbaya mnoooo ili niachane nayo
aaaaaameeeeeeennnnnnnnnn.
Iko sikitisha Sana.
Kuna Page Moja Nimeona Wakisema kuwa Kama unamoyo Mdogo Achana Nayo,Ila ni Nzuri Though Sijaiona.
 
Song Seung Heon And Liu Yi Fei Confirmed To Have Broken Up
wawakilishi wa muigizaji song seung hun leo hii wamethibitisha taarifa za mteja wao kuachana na muigizaji mwenye asili ya nchini china anayejulikana kwa jina la liu yi fei.
ni kweli wameachana na suala hilo ni lao binafsi na sisi hatujui sababu zilizowapelekea kuachana.
wawili hao walitangaza mahusiano yao mnamo mwaka 2015 baada ya kukutana pamoja kwenye movie inayokwenda kwa jina la Third love.

8684f963-2db9-4e51-9fff-87c7a7686fa8.jpg

NB:
huyu dada nilimpenda kwenye movie ya forbidden kingdom,nimeanza kumuogopa Khantwe noona haiwezekani wapinzani wake wote wanaachwa solemba ila yeye bado anabaki kupendwa.
why always khantwe.
film__4435-the-forbidden-kingdom--hi_res-cf6be1fe.jpg

hahahahaaaaa nimecheka sana nilipokuwa nasoma statement ya agency wa song seung hun pale aliposema wawili hao sababu ya kuachana haihusiani na THAAD.
THAAD imeleta mgogoro mkubwa sana kati ya China na Korea jambo ambalo limesababisha China kupiga marufuku masuala yote yenye kuhusu utamaduni wa korea kusini.
Doooh! Love Ni Ngumu Sana..
 
US539Cj.jpg

The End..

Ni Time Ya Awa Watu Sasa Kupumzika Duuhh!
2017 Wameitendea Haki Ikiwa Na Mafanikio Kibwena.
Wawe Na Gud Time Sa Ivi, Ama Wajipe Break..
 
NvQXWnD.jpg


Nchi Ina Baridi Hii..Niliona Juzi Kwenye Page Ya Seung Gi Akionyesha Nyuzi Joto Lao Kwa Siku Ile Ilikuwa 13

Na Awa WameFanya Hii Kazi Kwenye Baridi Sana.
 
Song Seung Heon And Liu Yi Fei Confirmed To Have Broken Up
wawakilishi wa muigizaji song seung hun leo hii wamethibitisha taarifa za mteja wao kuachana na muigizaji mwenye asili ya nchini china anayejulikana kwa jina la liu yi fei.
ni kweli wameachana na suala hilo ni lao binafsi na sisi hatujui sababu zilizowapelekea kuachana.
wawili hao walitangaza mahusiano yao mnamo mwaka 2015 baada ya kukutana pamoja kwenye movie inayokwenda kwa jina la Third love.

8684f963-2db9-4e51-9fff-87c7a7686fa8.jpg

NB:
huyu dada nilimpenda kwenye movie ya forbidden kingdom,nimeanza kumuogopa Khantwe noona haiwezekani wapinzani wake wote wanaachwa solemba ila yeye bado anabaki kupendwa.
why always khantwe.
film__4435-the-forbidden-kingdom--hi_res-cf6be1fe.jpg

hahahahaaaaa nimecheka sana nilipokuwa nasoma statement ya agency wa song seung hun pale aliposema wawili hao sababu ya kuachana haihusiani na THAAD.
THAAD imeleta mgogoro mkubwa sana kati ya China na Korea jambo ambalo limesababisha China kupiga marufuku masuala yote yenye kuhusu utamaduni wa korea kusini.
Hehehe niacheni nijinafasi wapi aminas unakumbuka lile agano letu [emoji23]
 
baada ya takribani miaka 4 mwanadada anayejulikana kwa kina la han hye jin hatimaye amerudi tena kwenye ulimwengu wa uigizaji baada ya kukubali ofa ya kuwa muigizaji mkuu wa kike kwenye drama inayoitwa “Let’s Look at the Sunset Holding Hands" ambayo itaonyeshwa na shirika la MBC
Han-Hye-Jin.jpg

Ni drama inayozungumzia simulizi nzuri yenye kuvutia inayowahusu wanandoa wawili ambao wanaamua kurudisha upendo wao waliokuwa nao baada ya kukabiliana na kifo (confronting the matter of death).
Nam Hyun Joo ni msichana aliyetokezea kumpenda mvulana tokea walipokuwa chuo kikuu, katikati ya maisha yao ya ndoa anaamua kuachana na mume wake na kuamua kwenda kutafuta upendo sehemu nyengine kwa ajili ya kutumia siku zake za mwisho wa uhai wake akiwa kwenye hali ya furaha na utukufu.
drama hii itakuwa ni ingizo jipya kwa mwezi Machi.
 
Back
Top Bottom