nimefika episode 20, now nimeamua kuiweka kiporo kwa muda usiojulikana
family drama na somo la food chain
park family + yeon family + chae family + cha family (familia zote zinategemeana)
Park Yoo-Ha
vs Chae Sung-Woon
baadhi ya nyakati wanawake munafanya makosa ya kujitakia wenyewe kwa sababu ya kupenda kwenu kunakoambatana na wingu zito la huruma dhidi yetu..... si vibaya kuolewa na mwanaume uliyevutiwa naye iwe anatokea kwenye familia yenye heshima zaidi yako au kinyume chake na ni ndoto ya wanawake wengi kuolewa au kuwa na mahusiano na wanaume waliojaaliwa neema ya kipato, jambo muhimu zaidi unalopaswa kulipa kipaombele kwenye mahusiano yako ni hili kabla ya kuangalia vigezo vyenginevyo:
huyu mwanamme atakuwa tayari kujitoa kwa shida na raha dhidi yangu?
imagine binti alizima ndoto zake za kuwa daktari ili apate wasaa au muda zaidi wa kuwa karibu na boyfriend wake huku akifahamu familia zote mbili hazifurahishwi na mahusiano yao, cha ajabu bwana yule kwa jinsi alivyo taka taka, dhaifu na muoga hakuwa na uwezo hata wa kumlinda mke wake ( mke wake alifikia hatua ya kuwa mtumishi wa ndani) na mwisho alimtelekeza kwa sababu ya ushawishi wa familia yake
jamaa hakuwa na uwezo wa kupata mtoto(infertile, infecund) hivyo basi kivyovyote walikubaliana pamoja na mke wake wafanye adoption ya mtoto ( ambaye ni eunsoo) au watumie njia za kimaabara, maajabu yalitokezea pale familia ilipohitaji paternity test ili kupata vithibitisho vya uhalali wa mtoto bwana yule akaanza kubweka ovyo, mara aje na wazo la kumpeleka nje mtoto wao ili siri yake isijulikane.
licha ya udhaifu wao wanawake sidhani kwenye dunia hii kama yupo mwanamke aliye tayari kumsafirisha au kutengana na mtoto wake aliye chini ya miaka mitano, nilivutiwa sana na uamuzi wa mwanadada park yoo ha wa kutokuwa tena tayari kuwa mtumwa wa familia kwa kutenganishwa na mtoto wake kwa hoja dhaifu ya kuficha siri ya mume wake hatua ambayo hatimaye ilipelekea apoteze haki ya kurithi au kupata gawio lolote la mali baada ya talaka (alimony).
licha ya kuachwa pia sheria haikumruhusu kutoka mbele ya hadhara kutangaza kuvunja kwa ndoa yake (nasubiri episode za mbeleni ateme cheche dhidi ya familia ile)
ndoa za tajiri na masikini zimejaa utumwa na manyanyaso (si ndoa zote)
View attachment 1398470