karibuni darasani walevi wenzangu, najua ulimwengu wa bando umetukalia vibaya ila nawakumbusha.
sigara iliuzwa shilingi 20 mpaka leo imefikia 200 na bado wahuni wanavuta moshi.
tutabana hapa hapa sote kwa bibi bando.
Under the queen umbrella drama:
ndio drama ninayoiangalia
King Yi Ho: tofauti na tulivyozowea katika dramas nyingi tulizoangalia, huyu bwana mfalme (choi won young) kihistoria ametokea katika mikono ya concubine, je ilikuaje mtoto wa concubine akabeba madaraka ya kifalme badala ya mtoto wa malkia.....Je kipi kilitokezea?
mfalme ana wanawake kama wote na watoto takribani 11.
Queen Im Hwa-Ryeong: uhusika huu umeigizwa na mwanamama kim hye soo, jamani eeehhh mabachela wenzangu huyu mama ana miaka 52 ya kuzaliwa na inaonekana hajaolewa....kwa wale wanaotaka kuzaa na kulea mjukuu munakaribishwa....Nimesema kuzaa mjukuu.
mkasa mzima wa hii drama unamuhusu huyu malikia na watoto wake watano wenye vichwa vibovu (troublemakers). moja kati ya jukumu kubwa la malikia ni kuyasimamia maswala yote ya ndani yanayohusu royal family wakiwemo wapinzani wake (concubines) , lakini pia ana wajibu wa kuhakikisha familia yake inakulia katika mazingira bora hususani swala zima la upataji wa elimu bora itakayowafanya wawe na hakiba bora ya urithi wa madaraka (grand princes). kwa kuwa yeye ni malikia basi ana wajibu wa kuwafunika watoto wake katika mwamvuli wake ili awaepushe na dhoruba ya mvua inayonyesha katika ikulu ya kifalme kila wakati.
Je mwamvuli wake utatosha kujifunika yeye mwenyewe na watoto wake wote watano kwa wakati mmoja.
queen dowager: kihistoria huyu bibi mchoyo alikuwa ni concubine na ndiye mama wa king yi ho, katika harakati zake za kuitafuta nguvu ya madaraka alihusika kwa kiasi kikubwa sana katika jaribio la kumuondoa madarakani malikia aliyekuwa na nyota njema mbele ya uso wa mfalme ila akakosa nguvu ya kumlinda (alitokea familia dhaifu).
Wivu na tamaa za madaraka ziliigeuza nafsi ya concubine huyu na hatimaye akajiingiza katika mchezo mchafu wa kumsambaratisha crown prince na malikia kwa dhumuni la yeye kutwaa madaraka pamoja na mwanawe. Yote hayo yaliwezekana kwa sababu ya nguvu ya familia anayotokea iliomuwezesha kwa kiasi kikubwa sana kutengeneza mtandao utakaoweza kumtii, kumtumikia na hata kumsujudia ndani ya royal palace.
Hatimaye malikia yule akasambaratishwa kwa kufukuzwa ikulu, watoto wake waliobakia nao wakajikuta wanaingizwa bila ya kupenda katika jehannamu ya umauti....
.jamani eeehhh kim hae sook anazeeka kwa kasi ya 6G.
Crown Prince: mtoto wa kwanza wa malikia, ni mweledi, muelewa, mjawa wa khulka njema....je ataweza kuilinda nafasi yangu inayoangalia kwa jicho la mwewe na watoto wa concubines?
Grand Prince Seongnam: ni mtoto wa pili aliyekulia maisha ya nje ya jumba la kifalme, hakupenda kujishughulisha sana na kusoma, ni kijana mwenye msimamo usioyumba juu ya jambo analoliamini. maisha ya nje ya ikulu yamemfanya awe ni kiijana mwenye ufahamu mkubwa wa fursa na changamoto wanazozipitia wananchi wa taifa la Joseon.......anaonekana kuwa ni kijana mwenye potential ya kuwa kiongozi bora ila hilo litawezekana ikiwa atasimamiwa na walimu bora.
Grand Prince Muan: ni mara yake ya kwanza kuonekana katika televisheni zetu lakini hilo halijamzuia kuonyesha kipaji chake alichojaaliwa cha uigizaji.....huyu bwana mdogo ni msumbufu kweli kweli, ni free spirit.......somo pekee analolielewa kwa haraka ni lile linalohusu ulimwengu wa ndoa na yanayofanyika ndani yake (tendo la ndoa).....hayo mambo ya falsafa na utawala amewaachia wengineo....
wakati huu ambao familia imeshampoteza kaka mkubwa, bwana mdogo ataendelea kuwa trouble maker au atarudisha majeshi nyuma na kumsikiliza mama yake anayetishiwa na wanasiasa wanaonyemelea nafasi ilioachwa wazi na mwanawe wa kwanza aliyefariki?
mimi sijui
Grand Prince Gyeseong: ni kijana mweledi na mwenye uelewa mkubwa sana pindi anapokuwepo darasani, lakini ana siri moja ya ajabu sana ambayo kama jamii itaifahamu siri hiyo basi huenda hukumu itakayomuangukia ni kifo....Anaonekana kuwa ni kijana mwenye kuvutiwa zaidi na maisha ya usichana.....
je ni baradhuli au ni hormones zinampelekesha vibaya?
mimi sijui..... malikia ana kazi kubwa ya kuendelea kuufungua mwamvuli utakaoweza kuendelea kumlinda mtoto wake dhidi ya wapinzani wake wanaotamani kuifahamu siri hiyo ya mwanawe.
Grand Prince Ilyoung: ndie mtoto wa mwisho wa malikia, naye ameamua kufuata nyayo za kaka zake, kaka mkubwa akienda guest naye huyooo anafuata njia, kaka mkubwa akikimbia darasani naye huyoooo anafuata.
Prince Uiseong: ndiye mtoto wa kwanza wa mfalme ila ametokea katika mapaja ya mwanamama concubine...babu yake ndiye chief councillor wa serikali.....anatamani sana kuwa crown prince kama walivyo wazazi wake...
prince bogum: ni great thinker, ana potential ya kuwa kiongozi mweledi ila bahati mbaya naye ametokea katika mapaja ya concubine.......kibaya zaidi historia ya mama yake inafanana sana na historia ya DONG YI......mama yake alikuwa ni mtumishi wa malikia....hana connection yeyote itakayomuwezesha angalau jamii imuone kuwa kiongozi sahihi ajaye.
watoto wengine mutaenda kuwasoma nyie.
haya karibuni uchawini, leo nimeamua kushitua vidole vyangu.