Kwa wataalam wa sheria masaada unahitajika

Kwa wataalam wa sheria masaada unahitajika

Nilikuwa nae alipewa risiti ya efd
1. Nenda dukan umuombe akusaidie kupata report ya mauzo ya Ile siku umeenda kununua na muda pia uzingatie,

2. Maduka mengi yana security camera Kama vp omba mwenye duka akusaidie video

3. Google wanahifadhi kila kitu kila mtu ataje siku aliyoanza kuitumia hyi simu na reference zote zinapatikana kwenye apps (G mail, G photo, G locations, G message na zinginezo)

Mjin akili
 
Nitamshauri jamaa awaambie polisi hicho kitengo cha cybe kifanye kazi yake. Na vipi hapo ikitambulika demu alikuwa anajaribu kumtapeli jamaa kisa hana risiti je mshkaji anaweza kumfungulia huyo dem mashtaka ya udhalilishaji? Maana jamaa anasema alibebwa juujuu kama mwizi toka mtaani kwao hadi kituo cha polisi anasema ilikuwa ni aibu kubwa sana kwake pale mtaani anapoishi.
Akitaka anaweza.
 
Huyo demu ni tapeli,hapo jamaa aandae mpunga kidogo kufukia hyo aibu,na gharama zake zitarud asihofu..mjini akili mzee
 
Muda huo upo rumande.
Polisi gani ana muda wa kupoteza
Mbona rahisi hilo polisi wanalimaliza mapema, waandike barua kujua namba iliyotumia hiyo simu muda fulani watajua nani mkweli
 
Risiti za magumashi zipo kibao anashindwaje ku foji hyo risiti huyo jamaa naye mzembe watu wanafoji cheti cha 4m4 ishindakane hlo jambo dogo mkulungwa kaingia king kizembe sana.
 
Habari wadau, natumai mko vizuri....

Iko hivi, kuna mshkaji wangu mmoja hivi yeye yuko mwanza huko.

Juzi jumaatatu alitangaza kuuza simu yake kwenye mtandao flani wa hapa bongo.
Sasa anasema ni watu wengi waliipenda Ile simu Ila kikwazo ni kwamba walikuwa wakiuliza kama ana risiti ya simu pamoja na box lake na pia emai ya risiti ifanane na ya kwenye simu ndiyo watainunua bila shida lakini kwa bahati mbaya jamaa yangu risiti na box la simu alishavipoteza kitambo kidogo Ila simu alinunua kwenye Duka kubwa tu la muuzaji mkubwa Sana wa simu pale mwanza na siku ananunua tulikuwa nae Ila Mimi kwa sasa sipo mwanza.

Jamaa anasema akatokea dada mmoja akaonesha uhitaji Sana wa hiyo simu kwa bei waliyokubaliana ilikuwa ni simu Aina ya REDMI NOTE 10pro ambapo walikubaliana wakutane jana na huyo dada kwajili ya mauziano rasmi.

Jamaa anasema mida ya asubuhi wakawasiliana na yule dada ili waonane kumbe Yule dada baada ya kuusoma mchezo kuwa mwamba Hana risiti demu akawahi kituo cha polisi Pale mwanza na kuripoti kuwa Kaibiwa simu akaitaja Ile Ile ya mshkaji na mwizi wa hiyo simu yake aka mtaja mshkaji pia na mpaka rangi ya simu aliitaja ileile maana aliona picha za simu jamaa alizopost wakati ananainadi bidhaa yake.

Sasa kumbe wakati yule demu anaenda kuonana na jamaa kwajili ya makabishiano aliongozana na polisi kama wanne hivi wamevaa kiraia mshkaji akatiwa mikononi mwa polisi na kubebwa juu juu mbele za watu maana walikubaliana waonane barabarani kisha watulie sehemu demu aikague simu ili kama ataridhika nayo basi aichukue.

Mchizi anasema alisombwa juujuu hadi kituoni akituhumiwa kumwibia huyo dada hiyo simu na kama simu ni yake alinunua basi aoneshe risiti ya hiyo simu kama anayo na wakati huo jamaa anasema demu alikuja na karisiti
kake mchizi hajui demu amekatoa wapi hako karisiti na akawapa wale Askari kale karisiti.

Lakini cha ajabu mshkaji Kila akiomba risiti ya huyo demu aiangalie kama ni ya hiyo simu kweli polisi waligoma kumuonesha wakabaki wameishikilia wenyewe na kumwambia mchizi aende Duka aliponunua hiyo simu huwa wanabaki na kopi za risiti pindi unapoinunua ikiwa mpya na wanaandika kwenye kompyuta watampa ili aipeleke hapo central police waangalie emai za risiti na simu na pia wajue Nani tapeli Kati ya mchizi na huyo demu wa mjini

Na demu kakomaa kwamba simu ni yake na mchizi ndo aliyemwibia huku akaonesha yeye anarisiti yake ambako ni karisiti uchwara sasa na mchizi hajui huyo demu kachongesha wapi hako karisiti.

Sasa wadau kama kuna aliyewahi kukutana na kesi ya kubambikiwa na kutaka kutapeliwa namna hii je hili swala linasoviwa vipi!!?

Je mchizi akienda pale tuliponunua simu kweli atapewa hiyo kopi ya risiti yake ama hizo kopi zinakuwaga hazipo. Maana sasa mchizi anatuhumiwa kuiba simu yake mwenyewe kisa hana risiti.

Kisheria hii ikoje wadau. Na je ikibainika kwamba demu ni muhuni jamaa anaweza akamfungulia mashtaka huyo demu?

Mods tafadhali naomba mnirekebishie spelling za tittle hapo juu ni msaada na sio masaada kama nilivyoandika.

Ahsante.......
Huyo jamaa yako aende dukani aliponunua wanabaki na kumbukumbu kibao.Akumbuke tarehe na mazingira yalibyokuwa siku hiyo.Ikibainika demu anadanganya,hiyo ni jinai polisi warare naye mbele ila Nina wasiwasi huenda polis wamekula Mchongo na huyo dada.Kama vipi atafute mwanasheria ampe msaada.Kwanini hawataki jamaa aikague risit na simu?
 
Huyo jamaa yako aende dukani aliponunua wanabaki na kumbukumbu kibao.Akumbuke tarehe na mazingira yalibyokuwa siku hiyo.Ikibainika demu anadanganya,hiyo ni jinai polisi warare naye mbele ila Nina wasiwasi huenda polis wamekula Mchongo na huyo dada.Kama vipi atafute mwanasheria ampe msaada.Kwanini hawataki jamaa aikague risit na simu?
Hivi risiti za simu zinakuwaga na IMEI namba za simu husika?
 
Wadau nashukuru Sana kwa ushauri wenu maana Mambo mliyosema hapa ndiyo nilienda kumweleza mchizi na akafanya kama nilivyo mwambia na kesi ameshinda.

Alienda lile Duka tuliponunua simu akapewa kopi ya risiti kisha akaipeleka pale kituo cha polisi na demu ndiyo akaonekana muhuni mpaka saizi yeye ndiyo anashililiwa na polisi kama tapeli la kimtandao.

Mbalikiwe saaana. Maana huyu jamaa ni mdogo wangu kabisa mumeplay part kubwa Sana katika Maisha yake katika kumwokoa na cello ya police.

God bless you all mliotoa mawazo yanu juu ya hili.

Ahsante
 
Mbona rahisi hilo polisi wanalimaliza mapema, waandike barua kujua namba iliyotumia hiyo simu muda fulani watajua nani mkweli
Waandike kwenda wapi?
TCRA?
Huu ushauri ni bora zaidi na utamfunga huyo dada kama kweli man simu ni yake
 
Back
Top Bottom