Kwa Watanzania walio na malengo ya kuishi kutafuta kazi au kusoma nchini Ubelgiji au Uswisi someni hapa

Mungu atatenda kitu kwako mkuu usife moyo
 
Karibu mkuu na tuko pamoja.
Usiku kunakuwa kumetulia na usisahau niko lock-down
Umenikumbusha Ghent mkuu, palee Red Light District walikula hela yangu ikaniuma kishenzi. Nilipata msala hapo nikakaa kama wiki sita pale UZ-Ghent (hospital nadhani ni ya chuo). Pombe bei rahisi sana pia vyakula, nimepiga sana Martin na ile miwine yao ya kenye maboksi.
 
Maisha mazuri sana ule mji lazma uinjoy, 😃😃kwamba pesa yako ilikuuma?
 
Maisha mazuri sana ule mji lazma uinjoy, 😃😃kwamba pesa yako ilikuuma?
Iliniuma kwa sababu nilichotarajia hkikuwa hivyo, Euro 50 yangu ikaenda hivyo na kwa siku nilikuwa napewa Euro 30 tu. lakini kweli.
 
Iliniuma kwa sababu nilichotarajia hkikuwa hivyo, Euro 50 yangu ikaenda hivyo na kwa siku nilikuwa napewa Euro 30 tu. lakini kweli.
Pole sana mkuu, ulishaondoka huko?
 
Ukija kihalali why nisikupokee mkuu, ilimradi usiwe na historia ya uhalifu au uvunjaji wowote wa kisheria
Sawa sawa mkuu as long as tuko woote jf ngoja tuwe karibu muda ndio utaamua
 
Ngoja corona iondoke, visa ziruhusiwe...
 
Mkuu Parabora nimefuatilia comments karibu zote ktk uzi wako huu leo walau umeongea mengi ya msingi yenyevmsaada kwa vijana sio km ule uzi wa Uswis uliokuwa umejikita kwenye kula bata na sehemu za starehe.

Sema shida inayotukabili vijana wengi humu ni pamoja na

*Level za elimu ya members walio wengi humu ni Diploma na high school pasi kuwa na taaluma zingine/Fani.
*Umri pia ni kikwazo kingine unakuta members wengi washagonga 30+ au 35 na ushee maana 25- wengi bado wako kwa wazazi ss unakuta umri wa kupewa kipaumbele na wenzetu wengi wameshavuka.
*Vipato duni vya kuwasafirisha watu kuanzia mchakato wa viza hadi kufika huko nao mtihani kwa baadhi ya members japo hili wanaweza kupambana nalo.
*Wenyeji wa kuwavuta huko nao mtihani..

Swali langu kwenu wenzetu mliojwishapata nafasi ya kuishi huko hv mmeshawahi japo kutenga wema kidogo ukaamua kusema sasa mm namvuta mbongo mwenzangu mmoja kila baada ya mwaka mmoja then ukamwambia wema huu utamlipa mwingine mbele???Kama ile ya PAY IT FORWARD ya bwana Dhar man?

Mm naamini sio kuwa kila mtanzania ni muhuni au anajihusisha na biashara haramu wengi ni waungwana ila wahuni wachache hawakosekani ila kiukweli km mngekuwa na moyo wa kuvuta wenzenu japo mmoja kwa miaka hata miwili kwenye akiba zetu za wema mngekuwa japo mna watu 3 ambao nao wangekuwa na wengine kadhaa nyuma yao tungekuwa tumefika mahali..
Hebu km vp ndugu zangu tuanze na hili wazo wema ni hazina ya baadae mm bw Dhar man huwa ananifubdisha vitu vingi sana japo najua wanaigiza ika ukweli vipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushauri mzuri sana huu mkuu
 
Ushauri mzuri sana huu mkuu
Nashukuru sana mkuu kwa kuu acknowledge ushauri wangu..

Na km kwa kuanzia unaweza ukaanza hata na mm then i will Pay it Forwad to another and another and another halafu tukiingia JF mkuu inakuwa full raha na sherehe kubwa sana..

Ukiona inafaa unaweza kunialika PM kwako,mm kwa sasa siwezi kuja maana najua kuna msururu wa maswali utakuwa unauliza huko.

By the way i wish you guys in the Diaspora good lucky and all the best.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usiogope mkuu nicheki tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…