Nyaka-One
JF-Expert Member
- Oct 27, 2013
- 4,730
- 6,736
Akacheze na wenzie🤣.Peleka mtoto shule za kata akapoteze muda .
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Akacheze na wenzie🤣.Peleka mtoto shule za kata akapoteze muda .
Watoto wako watajuta kukufahamu
English medium ya 1.5 haiwezi kufanana na ya 3M; na sio kwamba wanakula hela hapana, bali ndio kiwango cha pesa walichonacho, hivyo wazazi ndio wanaosababishia watoto wao mateso huku wakinufaisha biashara za watu bila kuchuja ninaweza kuchagua kilicho bora (EM za bei ghali) au kilichopo (Gvt)
Ila Walimu wananyonywa sio Serikalini au BinafsiMpo Salama!
1. Waalimu kulipwa mishahara Duni
Unapopeleka mtoto English Medium au shule yoyote Jambo la Kwanza Kabisa lazima uulize mishahara ya waalimu. Wanalipwaje?
Mshahara wa Mwalimu ni kiashiria namba Moja kuonyesha mtoto wako atapata Elimu Bora. Matokeo ya mitihani huweza kupokwa.
Mtu Anayelipwa vizuri huwa na moyo wa kutoa kilichobora.
English Medium wengi mishahara yao inawanyonya waalimu.
Mwalimu analipwa Laki mbili, Laki tatu. Hivi huo mshahara unategemea mtoto wako ajue kingereza au apewe Elimu ya kueleweka?
Halafu wakati huo wewe umetoa Ada kubwa lengo ni mtoto wako apewe Elimu nzuri
Lazima ufuatilie waalimu wanalipwa pesa Zao kwa wakati, lazima ufuatilie wanapewa kiasi gani ili ujue watajituma kwa kiwango gani.
Lakini utakuwa mpumbavu na mjinga ambaye unatoa pesa lakini hujui Yule anayemfundisha mtoto wako atakuwa analipwa kiasi gani.
Ni muhimu wakati wa unamuandikisha mtoto uulize uongozi wa Shule mishahara ya waalimu na uwaambia unaruhusiwa kuwauliza waalimu kuhusu malipo Yao.
Kwa sababu wewe ndiye boss WA wote, mwenye shule na waalimu na wafanyakazi.
2. Umahiri wa Waalimu wa kumfundisha mtoto wako
Waambie shule kuwa unaomba nakala za Profile la waalimu watakaoenda kumfundisha mtoto wako.
Je wako qualified.
Kazi hiyo usiiachie serikali pekee. Serikali haitoi Ada ya Mwanao🤓🤓.
Ni jukumu Lako kujua wasifu WA waalimu wanaomfundisha mtoto wako sio kwa mdomo Bali wakupe nakala za Profile Zao.
Lazima ujue waalimu wapo wangapi
Waalimu wengi wa hizi English Medium hawana quality ya kueleweka.
3. CHAKULA
Shule ya serikali huwezi ulizia suala la chakula Kwa sababu labda serikali itakulipia. Si unajua chakula cha kupewa huwezi ulizauliza.
Pesa ya chakula unayotoa English Medium inaendana na chakula anachokula mtoto Akiwa shule.
Usilete akili za kitumwa kuwa mtoto hajaenda Kula shule ilhali umetoa pesa yako.
Ni lazima ulinganisha pesa yako na kile unachopewa.
4. Hutakiwi kumsaidia mtoto Homeworks anazopewa shule
Ndio maana ulitoa Pesa.
Ni jukumu la shule kumfundisha mtoto wako aelewe kile ambacho wamemfundisha. Homeworks ilenge kujenga kumbukumbu na bangua bongo ya mtoto.
Sasa hizi English Medium wanakuandika maswali Mia moja ya Likizo alafu ukimwambia mtoto afanye hafanyi hata robo ya maswali.
Mengi ya maswali Mpaka umsaidie. Huo ni Utapeli.
Sasa mtoto anakuwaje wakwanza, au anapataje Wastani wa A Alafu Homeworks za Likizo alizopewa maswali Mia hawezi kufanya hata robo ya maswali. Huo ni Uhuni
Karibuni
Ha haenglish medium za watu binafsi za mtaala wa necta ni magumashi hata wakikulipisha ada kubwa
Kwa mzazi anaempeleka mtoto kusoma kwenye shule kama hiyo ndiye anaepaswa kushauriwa kumrudisha tu mwanae kwenye shule ya Kayumba.Juzi nimepeleka mtoto wangu wa Ke, shule Moja hapa jirani na Jiji njia ya kwenda Rufiji, pre form 1, wamemaliza group la wazazi likacharuka Kwa feedback mbovu mbovu, kunguni wa kutosha, maji shida kuoga mara Moja au hakuna kabisa, mtoto anachapwa akifumwa anaoga Kwa siri, kuosha chombo maji Kwa beseni na hakuna kumwaga utaoshea tena na tena. Watoto walikubwa na dhamama ya kuhara na kutapika Uongozi uka mute as if nothing happened. Nimehamisha mtoto sababu kuu maji, kunguni wanatibika japo kisingizio watoto wasilale wasome.
The vice versa is the truth.Watoto wako watajuta kukufahamu
The vice versa is true.Hela natafuta lakini siwezi kupigwa kifala kwenye shule za EM..
Siwezi kutoa hela yangu kumpa Bwana Mugetta mmiliki wa Muggeta Nursery and Primary School
Pdidy wakati tunasoma English medium ilikuwa IST na Olympio tu. Wewe umesoma ipi?Hahahaha tusingefika chuo
Hio cancer inakuja baada ya muda gani? Maanake nina miaka zaidi ya 40 nakula broiler.3. Hapo namba 3 kwenye chakula siku ya kuku huwa wanalishwa kuku broiler. Kuki broiler ni kansa promax
Hapa wanaongelewa wanaolazimisha kusomesha EM hawa obviously wako kwemye shule za ada chini ya 3m kwa mwaka.Tatizo mnafanya generalisation, kwenye nyuzi zote sijaona mnaongelea shule zipi, shule za private zinatofautiana ubora kwa vigezo mbali mbali, kuanzia kiwango cha elimu, malezi ya tabia pamoja na ada
Zipo shule nyingi sana za EM zinazotoa elimu bora ukiacha hizo mnazosema za kimataifa, ni milioni zako zinaongea acheni porojo
Umeanza Kula broiler lini?Hio cancer inakuja baada ya muda gani? Maanake nina miaka zaidi ya 40 nakula broiler.
Hujaelewa hoja ya mtoa madaMimi nianze kufuatilia profile ya mwl, unisaidie nini, mshahara wa mwalimu mm unisaidie ? Nisipopewa ushirikiano maana yake nisipopewa ushirikiano nimfundishe mimi mtoto wangu?
Mamlaka za elimu zinafanya kazi gani zisikague hayo yote, haya mwl analipwa laki mbili, kwa hiyo Mimi nikamuongezee,?
Poor
Tangu nimeanza kutafuna miaka zaidi ya 40 iliopita.Umeanza Kula broiler lini?
Muongo wewe kwanza broiler zenyewe zimeanza miaka ya elfu2Tangu nimeanza kutafuna miaka zaidi ya 40 iliopita.
wabongo wengi waoga Sana kwann usiulize na km hupewi ushirikiano uoni tyr hiyo sio shule tena timuka na vumbi neneNdio maana ya utapeli huo.
Fuatilia watoto wa medium utajionea walivyoweupe.
Pole sana. Broiler zipo miaka mingi sana. Wewe ndio umeanza kupata akili miaka 2000 unaona kila kitu kimeanza miaka ya 2000. Unaijua interchick ilianza kufanya kazi lini hapa Tz? Biashara yao kubwa unaijua?Muongo wewe kwanza broiler zenyewe zimeanza miaka ya elfu2
🙏🏻🙏🏻🙏🏻🙏🏻Pole sana. Broiler zipo miaka mingi sana. Wewe ndio umeanza kupata akili miaka 2000 unaona kila kitu kimeanza miaka ya 2000. Unaijua interchick ilianza kufanya kazi lini hapa Tz? Biashara yao kubwa unaijua?