Kwa wenye umri wa miaka 25 na kuendelea

Kwa wenye umri wa miaka 25 na kuendelea

Ben Saanane

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2007
Posts
14,580
Reaction score
18,193
Hebu niulize swali la kizushi,wakuu ni kosa gani ambalo umeshawahi kulifanya ukiwa na umri wa miaka 25-30 wakati ulipokua chuoni,kazini ambalo limekugharimu huko baadae na au ambalo ungetamani kuwa kama ungepewa nafasi nyingine ya umri kama huo usingelirudia?

Tunataka tu kujifunza kutoka kwa wengine
 
Kampuni niliyokuwa naifanyia kazi mara ya kwanza ilikuwa liquidated, nikapewa mafao 2M kipindi hicho (Y2K), sikuifanyia lolote zaidi ya kuzinywa na kurekebisha tabia za warembo!!

Only if wishes were horses...huh!
 
Kuishi maisha ya useja nikidhani nitatesa huko mbele ya safari. Sasa nimegundua kwamba hiyo nafasi nimepoteza kwani huku nilipo sasa ndo kugumu kuliko maelezo.
 
Kampuni niliyokuwa naifanyia kazi mara ya kwanza ilikuwa liquidated, nikapewa mafao 2M kipindi hicho (Y2K), sikuifanyia lolote zaidi ya kuzinywa na kurekebisha tabia za warembo!!

Only if wishes were horses...huh!

Duh,mkuu kweli kwenye hii range ya miaka hali ni critical.Mkuu kwani kipindi hicho hukua na mchumba?ilikuchukua muda gani kujijenga upya?
 
Kipindi hicho nilipewa mradi wa biashara kuiendesha(kusimamia) lakini kwa uzembe za kupenda anasa baada ya kuwa na pesa nyingi vilinipotezea nikashindwa kufanya mambo mengi ya msingi katika maisha, nikaja kuamka wakati nanyang'anywa mradi.

Natamani muda huo ungekuwa sasa kwani maisha nilichezea leo hii nalala njaa... CHEMSHA BONGO.
 
Kipindi hicho nilipewa mradi wa biashara kuiendesha(kusimamia) lakini kwa uzembe za kupenda anasa baada ya kuwa na pesa nyingi vilinipotezea nikashindwa kufanya mambo mengi ya msingi katika maisha, nikaja kuamka wakati nanyang'anywa mradi.

Natamani muda huo ungekuwa sasa kwani maisha nilichezea leo hii nalala njaa... CHEMSHA BONGO.

Inauma lakini ni vizuri sana kwani ilikutokea wakati bado una muda wa kurekebisha makosa. Shukuru Mungu kama umetoka salama kwani tulio wengi pia umri ulio tayari ulishavamiwa na upupu! Experience is the best teacher.

Wenzio hata experience kama zako tunazisikia kwenye bomba. Nahofia yanaweza kutukuta yale ambayo wengi wanasema kuwa ukimiss ujana wako utautafuta uzeeni. Ngoja nione kama nitakuwa Guinea pig!
 
Kampuni niliyokuwa naifanyia kazi mara ya kwanza ilikuwa liquidated, nikapewa mafao 2M kipindi hicho (Y2K), sikuifanyia lolote zaidi ya kuzinywa na kurekebisha tabia za warembo!!...Only if wishes were horses...huh!

Huna sababu ya kujuta. utumishi wa umma enzi ulikuwa upuuzi mtupu mbele ya wafanyabiashara. 2m vilikuwa visenti tu enzi za ruksa na kupanga matumizi kwa figa hiyo ungepata kichaa vingine vyo ungerudi nazo kijijini pengine muda huu ungekuwa diwani
 
Hahahaha mimi kitu nilichofanya nikaja kujutia lkn sasa hivi majuto yameisha ni kwamba ktk biashara zangu nilifanikiwa kuwa na saving kubwa. Sasa nilipokuwa nimepanga nyumba watoto wa kike wa mama mwenye nyumba walikuwa waanichokonoa sana kwa kero za kila namna sijui ilikuwa ni wivu maana nilikuwa dogo nina shughuli zangu wao wanashinda home tu!

Siku moja kero zikanizidi rohoni nilikuwa na kiwanja nikatafuta fundi ujenzi nikamwonyesha ramani akafanya quotation, bila kufikiria nikajenga nyuma nzima hadi ikaisha nikahamia na visent vyangu benki navyo vikaisha na biashara ikayumba halafu sikuwa na hela za kuisave biashara, nilitamani kuchanganyikiwa na jumba nilliliona kama kaburi, watu walikuwa wananipa hongera wanasema mambo yako supa lkn walikuwa hawajui rohoni nilikuwa na crisis!

NAMSHUKUU JEHOVA HIRE AMENIVUSHA NA SASA NAENDELEA VIZURI TENA lkn nilijifunza mambo mengi kutokana na kosa hilo.
 
Kampuni niliyokuwa naifanyia kazi mara ya kwanza ilikuwa liquidated, nikapewa mafao 2M kipindi hicho (Y2K), sikuifanyia lolote zaidi ya kuzinywa na kurekebisha tabia za warembo!!

Only if wishes were horses...huh!

ha ha ha ha PJ
 
SOMEWHERE IN BETWEEN ndio nimeoa!
sasa sina uhakika kama NIMEKOSA MIMI,NIMEKOSA MIMI,NIMEKOSA SANA
 
Ben, nilipata pesa nikasahau shule, nikajirusha sana, nilivyokuja kukumbuka shule nikakuta wenzangu wako mbali, Nikarudi shule kwa nguvu! nashukuru niliweza kuziba ile Gap.
 
Dah! Hii imekaa vizuri sana. Nakumbuka mwaka 1998 nilipata kazi moja yenye mshahara mzuri sana kwa wakati ule. Jambo kubwa nililofanya kwanza kabisa ni kununua Chaser Mayai. Mazee huwezi kuamini sikumbuki kama niliwahi kusave pesa bank maana mshahara na pesa nyingine nilizokuwa nakamata at that time ziliishia pale Kwa Macheni magomeni na Lango la jiji ni mwendo wa kubadili akina dada kila kukicha. Mwisho wa yote ili kubaki kuwa juu nikaanza mpaka kudokoa na pesa za ofisi siku auditors wametia timu nilikuwa natoka jasho mpaka kwenye kucha za vidole vya miguu. Kiukweli nilitimuliwa kazi ingawa nashukuru sikushitakiwa na gari nikauza. Niliyumba sana mpaka nilipokuja kukaa sawa. Laiti nafasi ile ningeipata nikiwa na akili za sasa hivi ningefanya mambo makubwa zaidi.
 
Hahahaha mimi kitu nilichofanya nikaja kujutia lkn sasa hivi majuto yameisha ni kwamba ktk biashara zangu nilifanikiwa kuwa na saving kubwa. Sasa nilipokuwa nimepanga nyumba watoto wa kike wa mama mwenye nyumba walikuwa waanichokonoa sana kwa kero za kila namna sijui ilikuwa ni wivu maana nilikuwa dogo nina shughuli zangu wao wanashinda home tu!

Siku moja kero zikanizidi rohoni nilikuwa na kiwanja nikatafuta fundi ujenzi nikamwonyesha ramani akafanya quotation, bila kufikiria nikajenga nyuma nzima hadi ikaisha nikahamia na visent vyangu benki navyo vikaisha na biashara ikayumba halafu sikuwa na hela za kuisave biashara, nilitamani kuchanganyikiwa na jumba nilliliona kama kaburi, watu walikuwa wananipa hongera wanasema mambo yako supa lkn walikuwa hawajui rohoni nilikuwa na crisis!

NAMSHUKUU JEHOVA HIRE AMENIVUSHA NA SASA NAENDELEA VIZURI TENA lkn nilijifunza mambo mengi kutokana na kosa hilo.

Lakini Cheusimangala kwa nn ulijuta huoni kama nyumba ni asset kubwa kwako ..kuliko pesa kukaa bank kila siku unacheki balance tu
 
Mhhhhhhhhhhhhh to me I keep on making mistakes, but I take the as challenges and new experiences and move on cause kuna muungwana alisema "experience is what people calls their mistakes" Life to me is a school so everyday I learn new stuff and personal I dont regret any thing happened to my life cause they are significant in my life.
 
Dah....Kosa kubwa ambalo najutia sana(Naomba Mungu anisamehe) ni kuhusu uchaguzi wa kozi za kusoma huko chuo.Sikutaka kufuata moyo wangu unataka nini au ninapenda kusoma nini ambacho nitakifanyia kazi ninayoipenda.Nilifuata mazingira yanataka nini na watu(wakiwemo wazazi na serikali) wanataka nini(si mnajua zile za masomo ya sayansi).
Kama ingekuwa tunarudisha muda,Nisingesomea hii profesheno niliyonayo.
 
Back
Top Bottom