Pre GE2025 Kwa yaliyojitokeza Mkutano Mkuu wa CCM, Hakika Kikwete ni mtoto wa mjini na ni jabali la siasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nani wa kupasua CCM? ACHA KUOTA NDOTO ZA ALINACHA. Yaliyofanyika ni mipango tu ya kazi. Nani atatoa hiyo fomu?. Ilikuwa itolewe fomu moja tu.
 
Kwahiyo kambi msoga imeshinda?

Ngoja Sasa tusubiri kambi Marangu na Singida
Msoga wana hali ngumu ila inabidi wasake tu chaka la kujificha maana makamu alikua wa upande wa Lowasa hujui sahivi na yeye anaenda na gia gani....labda kama wawe wameyajenga....ila msoga waliwekeza nguvu kubwa sana kwa January na wenzake,,,na upepo umebadilika ghafla kwahio lazima watafute sehem yakujishikiza na ambao kidogo zinaweza zikaiva ni wale wa Laigwanan kama wameweka tofauti zao kando..........Sukuma wanacheza kete kote kasoro upande wa msoga tu
 
Angekuwa mtoto wa mjini yeye na wenzake wengi wangechezeshwa kama mwanasesere na wadau wa huko nje ? Nadhani ungekuwepo enzi zile hata Mangungo ungemuita mtoto wa mjini ? (History will judge these people worse than the likes of Mangungo wa Msovero)
 
CCM, nikaona mzee mzima analazimishia azimio

SIasa, ni mchezo kama draft, CCM ikisha fanya maamuzi ya kikatili ... maumivu kwa wale waliojeruhiwa

Tuendelee kumuenzi huyu Mzee Kikwete,

Umesema Jakaya kafanya ukatili. Amelazimisha azimio. Watu wamejeruhiwa. Maneno yako hayo.

Halafu unasema tumuenzi.

Hivi kwa nini shule zetu hazitujengi kwenye logic ??? Assuming umesoma.

Pia unasema siasa ni kama draft. Hivi draft lina rafu ??? Ukatili, na kujeruhi, na kulazimisha maamuzi, maazimio ?? Unajua drafti linavyofata rules zisizo na mjadala? Jifunze kujenga hoja zenye
logic!
 
Kikwete ndo kazidiwa kete maana alitaka kuwaweka vijana wake na amefeli
 
Kikwete ndo kazidiwa kete maana alitaka kuwaweka vijana wake na amefeli
Haha wanaficha aibu,,,,hao kete zao ilikua ni wale vijana wa wazuri hawafi ila kwa sasa lazima warukeruke waonyeshe pia na wao wamo........sahivi wanajipa moyo maana wameona kuna mwana mtandao mwenzao wa enzi hizo, ila wanasahau wao wenyewe walishaanza kucheza rafu na watu wanakumbuka kwahio watalipiza tu
 
Watanzania wengi ni watu wa kwenda kwa emotions ukitaka kujadili mambo kwa facts hawawezi hata kutetea hoja zao kwa facts.
 
but we dont need that, huo “utoto wa mjini” utatufikisha wapi kama nchi ? tunataka maendeleo na siyo majungu, sijawahi kusikia nobel prize ya majungu na fitina ila kuna ya uchumi, peace na mambo kama hayo …
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…