Kwa yanayoendelea kesi ya Sabaya, naamini tutakuja kujua waliohusika kumshambulia Tundu Lissu na wasiojulikana kujulikana

mngony

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2012
Posts
5,555
Reaction score
6,972
Tunaanza kusikia tuliyokuwa hatuyajui au kuthibitisha yale tuliyokuwa tukidhania, kwa yanayondelea kutamkwa na Sabaya ni wazi hata kitendawili cha waliomshambulia Tundu Lissu na kilichowasukuma kinaweza kutatuliwa.

Sabaya anatamka kabisa kuwa alifika KIA akakutana team ya watu 4 ambao hawezi kuwataja ambao alienda nao kufanya operation aliyopewa na Mamlaka ya uteuzi.

Anaenda mbali kusema operation hiyo baadhi ya watu waliifahamu, inawezekama lengo ni kuhakikisha operation inaenda salama bila kukatizwa hata kama wengine hawajui ni operation gani na mengi aliyoongea.

Nikiangalia naona kabisa kuwa hata suala la Kushambuliwa Lissu, inawezekana pia ilikuwa operation nyingine, ukizingatia kulikuwa na fununu za Bashite kuwepo Dodoma wakati shambulizi linatokea.

Lakini pia wakati shambulizi linatokea inawezekana mamlaka zingine na watu wa makazi hayo( tunaambiwa ni ya viongozi) waliambiwa kuna operation japo hawajui ni aina gani na ndio inaweza kuwa sababu hakukuwa na ulinzi kabisa tofauti na siku zote na hata camera kutolewa?

Kingine kinachoonekana kuna watu wachache sana waliaminiwa na Mamlaka ya uteuzi kuweza kufanya operation za namna hii, ndio maana yule Sabaya alitoka Hai kwenda Arusha kufanya operation, na inawezekana mwingine alitoka Dar kwenda Dodoma.

Tundu Lissu mwenye alisema wakati anashambuliwa Mkuu wa Mkoa wa Dar alikuww Dodoma.


Ninachojiuliza hizi zilikuwa 'Rogue' operation? Inaonekana kuna kikundi cha watu( wasiojulikana) kiliundwa nje ya Taasisi rasmi, ndio maana zimefanya mambo 'kishamba' sana.

Nimpongeze Lissu kwa akili za haraka za kuamua kukilaza kitu yeye na dereva wake na kivuweka mbali viungo muhimu sana vya mwili, kana kwamba alipitia mafunzo, pia faida ya kuwa na tinted hawakuweza kuonwa kuwa wamelala.

NB; Majuma kadhaa kabla ya tukio kulitolewa amri ya kuondoa tinted zote kwenye magari mkoani kwake, baadae nadhani ikawa ngumu huenda operation ilipangwa ifanyike Dar ndio maana Lissu alianza kulalamika kuwa kuna gari zinamfatilia

Je wasiojulikana wanaanza kujulikana?

===

Pia soma: DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali
 
Plainly huyu alihusika kwa tukio la kumpiga Lisu Risasi. It seems Jiwe alimtumia katika kuua watu.
 
Pia inasemekana shambulizi dhidi ya Lissu uenda lilikuwa chini ya Mwenyekiti!
 
Mbona wanajulikana waliotaka kumuua lisu si mwendazake na genge lake
 
Mbona wengi sana huku kijini nyandolwa tunajua ni mbowe na genge lake.
 
Sabaya kakiri walikuwa wakitumwa kufanya uhalifu nadhani bashite nae akibana tutawajua wasiojulikana.
Ofisi ya raisi imechafuliwa vibaya na Sabaya.
 
Kwa ushahidi aliotoa Ole Sabaaya siku ya jana tarehe 13, ni wazi amefungua vifungo vya koti la maasi na dhambi za Mwendazake.

Pressumption iliokua mwanzoni kwa raia wakihisi matukio yaliokua yakifanyika nchini ni Maagizo kutoka kwa Mwendazake, sasa Ole Sabaaya kwa kauli yake ya kupokea maagizo kutoka kwa Mwendazake imekuja kuthibitisha hilo na kuweka wazi, alivyosema na kukiri kwamba amewahi kutekeleza baadhi ya maagizo ya Mwendazake kitaifa, ni kwamba matukio mengi yalifanyika nchini kwa shinikizo au maagizo kutoka kwa Mwendazake.

Mfano wa matukio ambayo yana connection na maagizo ya Mwendazake ni;

1) Kutekwa Mo Dewj.

2) Kutekwa Roma Mkatoliki.

3) Kutekwa na Kupotezwa kwa Ben Saanane na Azory Gwanda na wengine.

4) Kukamatwa kwa Yusuf Manji na Kubambikizwa Kesi Ya Kumiliki Mihuri na Nguo Za Jeshi, sambamba na kufilisiwa mali zake.

5) Kubambikizwa Kesi, Kutekwa Na Kuuliwa Wanasiasa Wa Upinzani Kitaifa.

6) Kutekwa na Kufunguliwa Mashtaka Ya Uhujumu Uchumi kwa Baniani Midevu na Rugemarila.

"
 
Plainly huyu alihusika kwa tukio la kumpiga Lisu Risasi. It seems Jiwe alimtumia katika kuua watu.
Ikiisha ya kesi Sabaya zije ya Makonda, huyu kafanya mabaya zaidi
 
Bado miili ya waliookotwa kwenye viroba
 
Sabaya kakiri walikuwa wakitumwa kufanya uhalifu nadhani bashite nae akibana tutawajua wasiojulikana.
Ofisi ya raisi imechafuliwa vibaya na Sabaya.
Huyu Bashite bado yuko Arusha?
 
Mo anajua siri aliyemteka
 
Pia inasemekana shambulizi dhidi ya Lissu uenda lilikuwa chini ya Mwenyekiti!
Siku ya tukio Mkubwa akiwa live jumbe jeupe alisema " huwezi ukawa msaliti uka survive"
 
Mkuu mngony , thanks for this, its a good analysis na inafikirisha, hivyo ni kweli kuna uwezekano wa kuwajua wale wasiojulikana ila 'wasiojulikana' kamwe hawatajulikana!, kama nilivyoeleza hapa.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…