KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Inasikitisha kuona kwamba taifa linafanya mchezo wa maigizo yanayoligharimu taifa mabilioni ya dola na kumbe hawako serious.
Tumejenga reli ya Umeme kwa gharama kubwa sana, halafu kutoka huko Kadogosa mkurugenzi wa shirika la reli anakuja na ajenda ya kununua vichwa vya dizeli.
Tunafahamu kwenye mchakato wa MANUNUZI ndio kuna wizi MKUBWA wa FEDHA ZA UMMA.
Kama Umeme unahujumiwa, je solution ni kurudi nyuma tulikotoka au ni kupambana na kudhibiti hujuma taifa liende mbele?
KAZI ya idara ya usalama wa taifa ni mshauri mkuu wa taifa na mlinzi wa usalama wa miundombinu Na maendeleo ya taifa.
Cha kusikitisha, eti nao wameshindwa kumdhibiti Kadogosa na mipango yake dhalimu ya kulihujumu taifa letu.
Uzalendo UKO wapi? Nahisi hiki kinachoendelea ni mlolongo wa uhalifu wa kimkakati unaohusisha mamlaka na watu wakubwa ndani ya serikali.
Hatuwezi kusonga mbele kama taifa iwapo watu kama kina Kadogosa wasio na uchungu Na uzalendo wataendelea kuongoza taasisi nyeti za taifa letu.
Rais kama hashiriki mpango huu dhalimu, ampige chini Kadogosa mara moja, achunguzwe na Polisi, Takukuru na idara ya usalama wa taifa.
Akipatikana na hatia afikishwe mahakamani mara moja
Tumejenga reli ya Umeme kwa gharama kubwa sana, halafu kutoka huko Kadogosa mkurugenzi wa shirika la reli anakuja na ajenda ya kununua vichwa vya dizeli.
Tunafahamu kwenye mchakato wa MANUNUZI ndio kuna wizi MKUBWA wa FEDHA ZA UMMA.
Kama Umeme unahujumiwa, je solution ni kurudi nyuma tulikotoka au ni kupambana na kudhibiti hujuma taifa liende mbele?
KAZI ya idara ya usalama wa taifa ni mshauri mkuu wa taifa na mlinzi wa usalama wa miundombinu Na maendeleo ya taifa.
Cha kusikitisha, eti nao wameshindwa kumdhibiti Kadogosa na mipango yake dhalimu ya kulihujumu taifa letu.
Uzalendo UKO wapi? Nahisi hiki kinachoendelea ni mlolongo wa uhalifu wa kimkakati unaohusisha mamlaka na watu wakubwa ndani ya serikali.
Hatuwezi kusonga mbele kama taifa iwapo watu kama kina Kadogosa wasio na uchungu Na uzalendo wataendelea kuongoza taasisi nyeti za taifa letu.
Rais kama hashiriki mpango huu dhalimu, ampige chini Kadogosa mara moja, achunguzwe na Polisi, Takukuru na idara ya usalama wa taifa.
Akipatikana na hatia afikishwe mahakamani mara moja