Kwa Yanga hii,Kaze utakosolewa na kushutumiwa sanaaa

Kwa Yanga hii,Kaze utakosolewa na kushutumiwa sanaaa

Itafika hatua hii timu itaanza kulilia shoot on target. hali ni mbaya
Kilichonishangaza ni kuona Kaze akiwakumbusha wachezaji wake mara kadhaa kutulia na kuweka mpira chini. Hivi kweli mchezaji wa Yanga unahamasishwa kuweka mpira chini dhidi ya Kengold? Nina hofu sana na uwezo wa baadhi ya wachezaji.
 
Dah, mbona kama mikia FC wanawashwa sana na pilipili iliyo shambani?
 
Kwani hao kengold walienda kuuza mihogo uwanjani..?? Acheni ujinga nyie utelembwe
 
Ramli zimeanza tena, ligi ilipoanza mara mtibwa, mara Mbeya City etc tukapiga wote, Simba akachoropoka mkoni ila Mapinduzi Cup tukajipigia, kwani hii ni Simba ipi unayoizungumzia?
angalia teams ulizotaja za ramli HALAFU ANGALIA HIZI RAMLI IKATOLEWA KWA PLATEAU UTD, PLATINUM,AS VITA, AL AHLY..did you notice any difference?
 
Kwani hao kengold walienda kuuza mihogo uwanjani..?? Acheni ujinga nyie utelembwe
Hoja si Yanga kupata ushindi kiduchu,hoja ni namna timu inavyocheza na viwango vya wachezaji. Hao madogo pamoja na kukamia game ila walikuwa na makosa mengi sana ya kimchezo. Kama Yanga ingekuwa na 'Quality'nzuri wale walikuwa wapigwe zaidi ya goli 5.
 
Ukiwa na kocha ambaye kwake kila mechi ngumu hata kama anacheza na alliance girls fc ujue huna kocha hapo.
tatizo la Yanga ni pamoja na wachezaji tusimlaumu kocha peke yake. kwa ukubwa wa Yanga kuna lundo la wachezaji hawana hadhi ya kuwepo kikosini. wajitathimini wachezaji wao kama wana hiyo quality ya kuwa 'Wananchi'
 
Kaze amekuja kabla ya Didier lakini bado tu hajapata muunganiko. Mwenzake Didier muunganiko umeshapatikana. Labda huyo Kaze tumletee SUPER GLUE ili atengeneze muunganiko.
Dada Rosaria hajaiunganisha Simba Bali kakuta mfumo mzuri Wa timu na wachezaji wanaoelewana kiuchezaji na wengi wamekaa pamoja muda mrefu.
 
acha kukaza shingo wewe. unazungumzia mambo ya mwaka juzi huko. toa ushauri kwa uongozi hapa ufanye kitu gani
Na wewe usikaze shingo kwa kutaka watu wasitoe reference. Mnavyopayuka utadhani ni jambo la kustaajabisha sana. Ni bora hili tungepayuka zaidi sisi weenyewe na si ninyi mana Haya yalishawakuta na ninyi tena mlitolewa kabisa mashindanoni japo hatujifichi kwenye hicho kivuli
 
Baada ya sare kadhaa kwenye ligi wachambuzi wa soka walimshutumu na kulaumu mbinu za Kocha wa Yanga hali iliyopelekea Kaze mwenyewe kutoka hadharani na kueleza kusikitishwa na namna wachumbuzi wa soka nchini wanavyomsema na kukosoa mifumo yake.

Kwa mtu mwenye ufahamu na uelewa mzuri wa mpira ataungana nami kwamba kocha Kaze ameshindwa kuitengeneza timu. Kila mchezaji anacheza kivyake. Viwango vya wachezaji vimeporomoka sana.

Mashambulizi yanayotengenezwa na washambuliaji wa Yanga ni rahisi kuyatabiri.Wachezaji hawana ubunifu kabisa katika eneo la mwisho.

Kwangu timu inapokosa mbinu,mtu wa kwanza kulaumiwa ni kocha na Kaze ajiandae kisaikolojia. Endapo timu itaendelea na mwenendo huu basi atakosolewa sanaa.

Kama hataki kusemwa basi lazima abadilishe kitu kwenye timu.
Kaze sio kocha kabisa yani Hua hajiongez yani nchimb sijui anampanga kwa nn pia kocha angekua na akil angeweza kujua kua kila calinho anavyo ingia basi team mbele Hua inacheza mpira wa kutulia Sana angalia mechi zake zote calinho lazima awe ametengeneza pasi au kafunga

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Dada Rosaria hajaiunganisha Simba Bali kakuta mfumo mzuri Wa timu na wachezaji wanaoelewana kiuchezaji na wengi wamekaa pamoja muda mrefu.
Hata ukimwita dada haipunguzi ubovu wa utopolo. Gomes kakuta wachezaji bora Kaze kakuta magalasa. Klabu inayosajili wachezaji zaidi ya 20 ndani ya msimu mmoja halafu inawatema 16 halafu inasajili tena 14 ujue hapo hamna timu zaidi ya kubahatisha tu.
 
Dada Rosaria hajaiunganisha Simba Bali kakuta mfumo mzuri Wa timu na wachezaji wanaoelewana kiuchezaji na wengi wamekaa pamoja muda mrefu.
asipoelewa na hii hoja basi kuna shida kwenye halmashauri yake ya kufikiri.
 
tatizo la Yanga ni pamoja na wachezaji tusimlaumu kocha peke yake. kwa ukubwa wa Yanga kuna lundo la wachezaji hawana hadhi ya kuwepo kikosini. wajitathimini wachezaji wao kama wana hiyo quality ya kuwa 'Wananchi'
Wewe ni shabiki halisi wa Yanga! Hakika wachezaji walio wengi wa Yanga ni wa kawaida sana! Hasa wale wa kikosi cha pili.

Hata wakati wa usajili, baadhi tulilamikia humu usajili wa wachezaji kama Waziri Junior, Zawadi Mauya, nk. Huwezi kulinganisha na Mikia Fc! ambao hata wachezaji wasio na namba kwao, bado wakipewa nafasi wanafanya kitu. Sisi timu yetu asipokuwepo Mukoko pale nyuma, ndiyo basi tena!

Washambuliaji wetu ni butu! Usajili wa mwalimu nao ni majanga tu! Huyo Saido ni spana mkononi! Fiston nae anaruka ruka tu uwanjani! Hana kabisa match fitness!! Kiukweli tunatia huruma kwa kiasi fulani.
 
Back
Top Bottom