Kwaheri Dkt. Magufuli, karibu uonevu

Kwaheri Dkt. Magufuli, karibu uonevu

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Ni mengi yatakimbia na kuonekana kama ndoto iliyootwa usiku na kusimuliwa na baadae kutoweka.Inaeleweka wazi na bila ya chenga zozote kuwa Mheshimiwa marehemu Raisi John Pombe Magufuli alikuwa kioo cha utawala bora Tanzania, kwa maana mema yake yalionekana na mabaya yake hayakujificha.

Kwa mtazamo huo yeyote yule atakaechaguliwa atasoma kutoka kwa marehemu na ataelewa Watanzania walipenda kitu gani na walichukizwa na jambo gani, vyombo vingi vya serikali vilikaa sawa kwa wananchi na vyombo hivyohivyo vilitumika kuikiza haki.

Wananchi wanaosemekana ni wanyonge walitumika kama ukuta mkubwa unaozuia kuona yaliyo ndani na ndio hivyo hivyo sifa zilipatikana nyingi kwani maovu yalikuwa machache na yanahesabika japo kuna yasiyofutika na yanayotia huzuni kwa wachache.

Kuna vyombo au viongozi wa Serikali waliokuwa wameficha makucha yao hili ni kundi lenye hasira sana ,maana wakati ule wakiogopa hukumu za papo kwa papo ,zinazotka kwenye mamlaka na sio mahakama.

Sasa tuelewe mazuri yote yalitokana na Raisi mwenyewe yeye kama yeye na ukichunguza mabaya yote yalitokana na Chama chake kwa ujumla wake na ujumla wao.

Rais alikuwa na roho nzuri sana lakini chama chake kimejaa walio na roho mbaya, Rais aliweza kuwadhibiti hawa katika mamlaka yake na kwenye zile njia zitakazompaisha kama ni mpenda maendeleo na mpenda kuona mwananchi wa chini hadhulumiwi anahakikisha anawasaidia hata kwa kutoa hela zake mfukoni, akiwajengea mazingira rafiki ya kufanya kazi, si bodaboda, si mamantilie si wamachinga na wengine wengi.

Hili ndilo lilompa uthubutu wa kupendwa huku uraiani, mambo makubwa ambayo yaliutia doa utawala wake yapo na yataendelea kuwepo. Rais aliepo madarakani anaweza kuyatumia hayo yakazidi kumpa respect kwa upande wake.
 
Mama Samia S Hassan, the Iron lady, ametuhakikishia hakuna litakalo haribika🙏! Hapa ni kazi tu! Tuendelee kufanya kazi! RIP our hero! Your spirit 'll live on ✊!
 
Ndio maana tunapiga kelele mifumo iboreshwe, kama sheria zipo, polisi wapo mahakama, bunge lipo, kwanini tuhofu kuonewa? Ni kwa sababu hizo taasisi haziko imara. Yeye JPM ndio kachangia kwa sababu aliwaaminisha watu yeye ndio suluhu ya kila kitu, Si mahakama si Bunge wala Jeshi, akifanya uamuzi hakuna wa kupinga.

Sasa matokeo yake Yeye kaondoka tunarudi kwenye wasiwasi uleule alioukuta na akaucha, yeye aliamini katika Mtu imara sio taasisi imara.
 
Tulimuamini sana JPM tulijua jambo la kipuuzi likifika kwake waliofanya upuuzi lazima wakione cha moto. Na watendaji walijua Magufuli anamaanisha na hatanii ndio maana hata kama walifanya kwa uoga lakini iliwabidi wafanye.

Mkurugenzi akisikia kuna uozo sehemu hata kama ni mzembe alijua asipofatilia yeye ndio atawajibishwa so aliibana system yake and so on.

Mama Samia kazi yake kubwa itakuwa kuongeza uzito kwenye kusimamia uwajibikaji, kero za watanzania ni mambo madogo madogo uko kwenye maofisi ya halmashuri, kwenye mahospitali kwenye idara za serikali. Walirudi zama zile za ukiwa ukifanyiwa dhulma hakuna pakusema Mama atatuangusha na atawapa msemo hiki chama cha kaskazini.
 
Ndio maana tunapiga kelele mifumo iboreshwe,kama sheria zipo,polisi wapo mahakama,bunge lipo, kwanini tuhofu kuonewa?Ni kwa sababu hizo taasisi haziko imara,Yeye JPM ndio kachangia kwa sababu aliwaaminisha watu yeye ndio suluhu ya kila kitu,Si mahakam si Bunge wala Jeshi,akifanya uamuzi hakuna wa kupinga,

Sasa matokeo yake Yeye kaondoka tunarudi kwenye wasiwasi uleule alioukuta na akaucha,yeye aliamini katika Mtu imara sio taasisi imara.
Tutawalazimisha wawajibike! Tumeshaonja utamu lazima tuchonge mzinga i see! RIP our hero 💔🙏!
 
Back
Top Bottom