Kwaheri Kocha Nabi umeacha alama ya mafanikio tunakutakia kila lenye heri uko uendako

Kwaheri Kocha Nabi umeacha alama ya mafanikio tunakutakia kila lenye heri uko uendako

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Ni kawaida kwa kocha yeyote kulinda heshima yake baada ya mafanikio makubwa kwenye carrier ya kazi yake.

Kocha Nabi amelifanya hilo jambo kwa uweledi mkubwa sana akiwa na klabu ya yanga, kapata mafanikio kuliko kocha yeyote yule kwenye mpira wa Tanzania, kavaa medali ya caf confederetion cup, kavaa medali ya ligi kuu, kavaa medali ya FA cup, kavaa medali ya ngao ya hisani, ni mafanikio ya kiwango cha juu kabisa.

Kwa mantiki iyo ilikuwa ni ngumu sana kumbakisha kutokana na vilabu vingine vikubwa vyenye misuli ya kiuchumi kumwekea ofa nono ambayo ni ngumu kuikataa.

Kwa mantiki iyo tunamtakia kila la heri kutafuta changamoto mpya!

Pia napenda kuwajuza mashabiki na wanachama wa yanga kuwa watulivu kwa kuwa aliyemleta Nabi wasisahau bado yupo, Nabi uyu wakati analetwa alipondwa sana but waliomponda leo ndio wanafurahi kuondoka kwake kwamba amewapa ahueni! Kwangu mimi ahueni aiwezi kuwepo hata akija kocha mwingine.

Yanga hii mpaka inafika hapo ilipofika imejengwa na vitu vingi sana kuanzia menejimenti, mashabiki,wanachama, squad ya timu husika, umoja na mshikamano vimechangia pakubwa kuifanya kazi ya Nabi iwe rahisi sana!

Kwa maana hiyo kocha anaekuja ataanzia pale alipoishia Nabi na kuendelea kuuwasha moto kutokana na ubora wa kikosi kilichopo na maingizo machache yenye ubora yatayoingizwa msimu ujao!

Nabi kaacha msingi na jengo tiyali kinachofata ni kuezeka tu kwa kocha anayekuja aitokuwa kazi ngumu zaidi ya mbinu tu za kiufundi kwa kuwa kikosi kimekamilika kila idara,
Na uongozi ulishatambua kuondoka kwa Nabi mapema kabisa na walishaanza mchakato wa kumpata kocha mpya ata kabla ya kuitimishwa kwa mechi za ligi ivyo muda si mrefu kocha mpya atatangazwa rasmi!

Aluta continua mapambano yanaendelea!
 
Hivi Mashabiki wa Yanga Hata UANDISHI WA kamakala kadogo haka ni mtihani.

Mbona nyuzi zenu zina Kila aina ya changamoto?????????

Jitahidi kuweka Aya kwenye maandiko yako.

Hapa JF ukifuatilia Nyuzi nyingi za hovyo ni za yanga.

Ndio Maana yanga ilikuwa timu ya Wananchi wenye uelewa mdogo.
 
TunamshukurukwaalipotufikishanatunamtakiamemaaendakoVIVAYANGA[emoji172][emoji172][emoji172][emoji172][emoji172]
 
Ni kawaida kwa kocha yeyote kulinda heshima yake baada ya mafanikio makubwa kwenye carrier ya kazi yake, kocha Nabi amelifanya hilo jambo kwa uweledi mkubwa sana akiwa na klabu ya yanga...
hapo umechemsha kwamba ndo kocha mwenye mafanikio makubwa zaidi kuliko kocha yoyote yule kwenye mpira wa Tanzania.

mbona King Kibadeni alivaa medali zote hizo akiwa na Simba miaka 30 iliyopita plus na Muungano plus Afrika Mashariki na kati plus, tena mzawa sio wa kunuliwa kutoka.
 
Ni kweli anastahili kuagwa kwa heshima ila hizi hype mnazompa ndio shida yenyewe, Nabi kama makocha waliowahi kupita ameshinda kombe la ligi,FA na ngao ya jamaii mara mbili.

What's so special?
 
hapo umechemsha kwamba ndo kocha mwenye mafanikio makubwa zaidi kuliko kocha yoyote yule kwenye mpira wa tz....
mbona King Kibadeni alivaa medali zote hizo akiwa na Simba miaka 30 iliyopita...plus na Muungano plus Afrika Mashariki na kati plus.... tena mzawa sio wa kunuliwa kutoka......
Leta ushahidi hapa
 
Hivi Mashabiki wa Yanga Hata UANDISHI WA kamakala kadogo haka ni mtihani.

Mbona nyuzi zenu zina Kila aina ya changamoto...
Katika watu wanaojuwa kuandika wewe ni sufuri kabisa, yani zero plus.

Ni shule ipi uliyofuyofundishwa kuchanganya caps kwenye sentensi?

Wewe ni bure kabisa.
 
Ni kweli anastahili kuagwa kwa heshima ila hizi hype mnazompa ndio shida yenyewe, Nabi kama makocha waliowahi kupita ameshinda kombe la ligi,FA na ngao ya jamaii mara mbili.

What's so special?
Special ni kuvaa medali ya afrika kombe la shirikisho kwa kufika fainali tuambie miaka mingapi imepita mpaka Nabi anakuja kufika hapo alipofika
 
Special ni kuvaa medali ya afrika kombe la shirikisho kwa kufika fainali tuambie miaka mingapi imepita mpaka Nabi anakuja kufika hapo alipofika
Kwahiyo Aussems nae tuseme ni kocha bora kwakua aliweza kuchukua Ngao, makombe ya ligi, FA na kuipeleka Simba Sc makundi ya CAF baada ya miaka mingi?

Swala la medali ni fluke tu ndiomaana alitoka CAFCL akiwa katika hatua za playoffs.

Nabi ni kocha mzuru ila sio mzuri kuwahi kutokea hapa Tz.
 
Kwahiyo Aussems nae tuseme ni kocha bora kwakua aliweza kuchukua Ngao, makombe ya ligi, FA na kuipeleka Simba Sc makundi ya CAF baada ya miaka mingi?

Swala la medali ni fluke tu ndiomaana alitoka CAFCL akiwa katika hatua za playoffs.

Nabi ni kocha mzuru ila sio mzuri kuwahi kutokea hapa Tz.
Inawezekana ukawa uko sahihi lakini Kwa miaka hii karibuni ni lini Yanga walikaa na kocha mmoja walau misimu miwili bila kugombana? Chanzo cha ugomvi ni mataji...

Nabi was so special kaipa Yanga mataji muhimu kwa level ya Taifa mbele ya Simba ambayo ilikua imeshaweka Utawala Kwa miaka minne na pia kimataifa ilikua imejitengezea kaufalme flani hivi lakini pote huko Nabi kafanya vizuri Sana. Na kaacha timu imara sana ambayo hata kocha mgeni akija hatapata tabu kubwa kuendeleza gurudumu.

Yanga ni Bora Sana Kwanza nikukumbushe Tu kua mpinzani mkubwa ambaye ni Simba sio kwamba alikua mbovu kama wengi wanavozani, fikiria Tu msimu huu Simba kapata ponti 75 out of 90 lakini kakosa ubingwa, pia kafika robo huko CAF so ilikua Timu nzuri tu, lakini Yanga imesukwa hasa na Nabi ndo inafanya Simba ionekane ya kawaida kabisa...
Ukweli bila Nabi huu msimu Simba angekua bingwa. Hivo ndo maana Nabi anaonekana so special
 
Hivi Mashabiki wa Yanga Hata UANDISHI WA kamakala kadogo haka ni mtihani.

Mbona nyuzi zenu zina Kila aina ya changamoto?????????

Jitahidi kuweka Aya kwenye maandiko yako.

Hapa JF ukifuatilia Nyuzi nyingi za hovyo ni za yanga.

Ndio Maana yanga ilikuwa timu ya Wananchi wenye uelewa mdogo.
Wewe ndiyo unajua kuandika wakati hata proof reading umeshindwa shame on you
 
Apewe heshima yake na anaondoka nayo kwani msimu ujao hakuna shaka makocha wa ndani na nje ya Tanzania watakuwa wameandaa Timu zao kumkabili. Hivyo, busara inamtuma aondoke asije kushindwa kuifikisha timu fainali tena kwa kuwa Yanga bado haijawa moja ya timu kubwa barani Afrika
 
Back
Top Bottom