Kwaheri TTCL, kila lenye mwanzo halikosi mwisho

Kwaheri TTCL, kila lenye mwanzo halikosi mwisho

Yaani kuanzia juzi nakjaribu kununua bando la internet wanasema kunatatizo la kiufundi. Basi tena hivi nivyochati natumia bila kujiunga basi tena 5000 iishe tu nijue moja
Pole sana mkuu
Mimi mwenyewe nimepata masekeseke kama hayo siku 2 3 hapo nyuma ndo namilizia bando langu la mwisho hapa.
 
Mashirika mengi ya serikali yanafanya uzembe wa makusudi sababu serikali ndiyo inalipa mishahara.

Haya mashirika yameajiri watu wabovu ajira za kudumu.

Ukienda ttcl kuna wazee wengi sana wasio na msaada, hawa walitakiwa wastaafishwe kwa lazima.

Haya mashirika yana wafanyakazi wengi kuliko utendaji kazi wao

TTCL inajenga makao makuu Dodoma wakati haitengenezi kitu.

Airtel wameipa serikali gawio la Bilion 39, kwa hisa 49%

Ukija kwa atcl huko napo pamejaa ujinga mtupu

ATCL ina marubani 147 kwa ndege 6 zinazofanya kazi kwa sasa

Ina hosts zaidi ya 300 kwa ndege 6 zinazofanya kazi

Shirika lina wafanyakazi zaidi ya 600 kwa ndege 6 afu tutegemee kupata faida

TRC wanajiibia wenyewe, wanashindwa kuwa wabunifu.

Hawajawahi tangaza wala kutafuta tender ya kusogeza makontena
Ndio shida ilipo kwenye administration costs, hasa salaries and wages.

Wote wanafanana serikalini, sema wengine ni cashcows tu kama bandari, TPDC na wengineo wanaovuna automatic tu bila ya mshindani ndio maana wanafaida.

Bank ambazo serikali ni mmbia zinafaida leo kwa sababu zinaendeshwa kibiashara na wakurugenzi wako responsible to shareholders. Lakini kabla ya hapo na zenyewe ilikuwa wanatengeneza hasara kila siku kutokana na matatizo haya haya waliyonayo mashirika ya umma ya kibiashara yanayomilikiwa na serikali 100%.

Kuna paper moja ya Kimei akiongelea matatizo ya banking zama hizo sababu za banks nyingi kufeli ilikuwa; serikali kuu na taasisi zake kuzikopa na kushindwa kuzilipa kwa wakati na kuzifanya kuwa na ukwesi, managers wasiokuwa na sifa za banking na mikopo holela ya kibiashara kwa sababu watu wanajuana tu bank managers.

Hiyo paper ya Kimei iliandikwa in the 90’s wakati Mwinyi raisi na Kimei sio mkurugenzi wa CRDB.

Since then nothing has changed kwenye taasisi za serikali hao ATCL CCM na serikali ikijisikia tu inachukua ndege kwa matumizi yao, bandarini tunaambiwa ukwepaji kodi umerudi, TANESCO toka waanze kununua gas TPDC awajahi lipa ilikuwa inadaiwa trillions, bank za serikali kwa asilimia 100 kuna watu wanapata mikopo kiholela mmoja kakimbia nchi, Serikali ndio wadaiwa wakubwa wa pension funds na awalipi on time.

Yaani matatizo ni yale yale aliyoyaongelea Kimei in the 90’s ndio yaliyopo leo 30 years later, wamebadilika watu wanaoendesha serikali; ila tabia za serikali ni zilezile.

Akitokea mtu wa kubadilisha culture ya ufanyaji mambo serikalini, salaleh atatukwana huyo mitandaoni na kuitwa katili wakati kazi yenyewe ndio kwanza ipo kwenye ku scratch surface tu. Tanzania dhana ya uwajibikaji serikalini bado kueleweka.

Ndio hayo mashirika yanaendeshwa ovyo, ila serikali nayo inachangia kuanguka kwake kwa namna inavyoyasimamia na kuhujumu pia hizo taasisi; wewe uwezi kuita ndege ya shirika at whim na si ajabu usilipe hizo flight costs halafu ushangae wakipata hasara.
 
Baada ya ripoti ya CAG Kutolewa na kueleza madudu ya TTCL, Rais Samia Hassan amependekeza shirika hilo la umma libaki kusimamia mkongo wa Taifa tu, lachane na biashara ya mawasiliano ya simu.

Kwa kauli hii ya Rais bila shaka huu ni uamuzi kamili wa kuizika rasmi TTCL kwenye simu za viganjani.

Sasa sijui hizi line zetu itakuwaje yaani, tutafidiwa chochote au ndio vile tena?

Tunaitakia kila la heri.
Alivoenda tu huko huyo Peter Ulanga nikajua itakuwa hivyo tu!
 
Mashirika mengi ya serikali yanafanya uzembe wa makusudi sababu serikali ndiyo inalipa mishahara.

Haya mashirika yameajiri watu wabovu ajira za kudumu.

Ukienda ttcl kuna wazee wengi sana wasio na msaada, hawa walitakiwa wastaafishwe kwa lazima.

Haya mashirika yana wafanyakazi wengi kuliko utendaji kazi wao

TTCL inajenga makao makuu Dodoma wakati haitengenezi kitu.

Airtel wameipa serikali gawio la Bilion 39, kwa hisa 49%

Ukija kwa atcl huko napo pamejaa ujinga mtupu

ATCL ina marubani 147 kwa ndege 6 zinazofanya kazi kwa sasa

Ina hosts zaidi ya 300 kwa ndege 6 zinazofanya kazi

Shirika lina wafanyakazi zaidi ya 600 kwa ndege 6 afu tutegemee kupata faida

TRC wanajiibia wenyewe, wanashindwa kuwa wabunifu.

Hawajawahi tangaza wala kutafuta tender ya kusogeza makontena

Inasikitisha sana,
Hakuna namna sasa, CEO's wa haya mashirika plus operation managers lazima tutangaze nafasi na tuajiri expart wakiwa na targets na tuache kila siasa.

Imedhihirisha kabisa watu wetu ni bogus tu kwenye modern internation business, bado watu wetu wanawaza kizamani, flexibility nayo zero.
 
Ntakupa scenario moja..!!
Kwa makampuni binafsi ya simu, mhandisi wa kwenye minara anapewa gari, mafuta, laptop na toolbox. Kwa mfano, mhandisi huyu anaishi, Say, Temeke Dar na minara aliyogawiwa kuihudumia incase ina tatizo ipo Kuanzia Mbagala, kuelekea direction ya Ikwiriri na hadi Utete. Mtu huyu kama kuna tatizo kwenye backborne site yoyote, say Mwalusembe, ambayo kuzima kwake kunamaanisha Lindi, Mtwara na Tunduru mawasiliano yanakata. Akipewa taarifa hiyo hata usiku wa manane. anawasha gari safari kuelekea Mwalusembe na anaiwasha site inarudi kwenye utaratibu wake wa kawaida na watu wanaendelea kuwasiliana.

Tuje kwa TTCL..!! Huku ni hatari. Gari analo dereva, ambaye atamfuata Mhandisi anayejua minara pindi mnara fulani unapozima. Sasa zamani, makampuni ya simu yote, kutoa mawasiliano Dar na kuyafikisha nje ya Dar, wengi walikuwa wanakodi tower space kwa TTCL, ground space na transmision zao kwenye minara yao mbalimbali nchini. Sasa waza sehemu kama Mkuranga ambapo, let say airtel, wamekodi nilivyovitaja hapo juu kwa TTCL. Sasa mnara wa TTCL ukizima, kwa airtel wao, ina maanisha Lindi, Mtwara na Tunduru kunazima koteee..!!! Sasa kwenye mazingira kama hayo, atatafutwa dereva wa TTCL, awashe gari na kumfutana mhandisi aliko, halafu ndiyo waende eneo la tukio. Bila kusahau dereva naye lazima apate ruhusu toka kwa bosi wake (wa logistics). Bila hivyo hawashi gari.

Kumbuka wakati hayo yote yanafanyika, wateja wa Airtel hawawasiliani and hence REVENUE LOSS KWA AIRTEL. Kwa delays walizokuwa wanazisababisha, airtel towers zinakuwa chini kwa muda mrefu. Kwa sababu hii na nyinginezo;

1. Makampuni binafsi ya simu yakajijengea towers zake. Hence TTCL wakapoteza mapato makubwa sana ya kila mwezi toka kwenye kukodisha tower space, ground space na transmission.

2. Baada ya makampuni binafsi kujiondoa kwenye miundombinu ya TTCL, wao hawakubadirika, waliendelea na uzembe huo huo, kiasi kwamba walikosa wateja.

3. Hadi leo hii, market share ya TTCL ni less than 1.5%. Na si ajabu, kuna watu hata humu JF hawazijui hata codes za TTCL. Mfano, mtu akisema namba yangu ni 0784xxxxxx unajua ni airtel, au 0713yyyyyy unajua nitiGo etc

NB. KWA MAKAMPUNI BINAFSI, KUMPA MTU GARI LA KUZUNGUKA NALO MINARANI NA HUKU AKIWA ANAKAA NALO NYUMBANI LIKI NA FULL TANK, NI GHARAMA NDOGO KULIKO KUZIMA BACKBORNE SITE KWA LISAA LIMOJA.

KWA TTCL, GARI ANAKUWA NALO BOSI AU DEREVA. MHANDISI KUWA NA GARI NI ANASA

watu wetu vichwa vigumu sana, wanakosa kabisa modern styles za kurun business na kugenerate profit.
 
Nashauri shirika livunjwe na vijana waandike proposal bila kuwahusisha wenye mitandao ambao inawezekana wazee waliopo posta wanashirikiana na wenye mitandao kudumaza posta.posta is there to stay.kunaitajika vijana energetic kuliendesha kwa mikataba kama wanayopewa na mamitandao mingine.if you don't delivery thud is the end of you contract. Kuna wanaokodoa macho shirika life wao kwa kupitia kampuni zilizoandikishwa nje wakanunua.wenyine ni haohao waliokwapua mabilioni ya $
na £.hivyo hivyo wanaitaka bandari yetu kwa kutodelivery .baadaye.
 
Afrika nakutamani ikiwemo Tanzania tunakwama wapi?
Almost mashirika yote ya Umma in almost African countries kama hayapo ICU basi ni RIP.
Is our brain not aligned for success?
Au tunahitaji kufanyiwa genetic modified brain?
No body loves African unless its sport scene or drama.
TTCL ina kila sababu ya kustawi.
Mkonga wa taifa ndio tanzanite ya TTCL.
Nadhani wamejipanga vizuri kusambaza data kwa mfumo wa wifi majumbani.
Just imagine,nyumba milioni 5 Tanzania zifungwe wifi kwa tozo la huduma ya sh 50,000 kwa mwezi=5,000,000 ×50,000=
250,000,000,000 yaani B 250 kwa mwezi.!!
Tuanzie hapo.
Akitaka msaada tupo wengi tupewe/tuuziwe hisa.
 
Tulishafahamu hili tena limechelewa.

Wanaomiliki makampuni ya simu wanashirikiana na TCRA, wengine wanatetea hawa mbweha hadi bungeni kupandisha bei ya bando na wizi wa makampuni ya simu kwa wateja, wanafahamika wote.

Walizuia starlink kuleta huduma ya internet Tanzania, ndio hao hao wanahujumu TTCL.

TTCL tishio kwao sababu huduma ya internet ni nafuu zaidi ya hao wengine, wameona heri kuifuta.
WEZI WOTE WA NCHI HII MUNGU AWAUE
 
Afrika nakutamani ikiwemo Tanzania tunakwama wapi?
Almost mashirika yote ya Umma in almost African countries kama hayapo ICU basi ni RIP.
Is our brain not aligned for success?
Au tunahitaji kufanyiwa genetic modified brain?
No body loves African unless its sport scene or drama.
TTCL ina kila sababu ya kustawi.
Mkonga wa taifa ndio tanzanite ya TTCL.
Nadhani wamejipanga vizuri kusambaza data kwa mfumo wa wifi majumbani.
Just imagine,nyumba milioni 5 Tanzania zifungwe wifi kwa tozo la huduma ya sh 50,000 kwa mwezi=5,000,000 ×50,000=
250,000,000,000 yaani B 250 kwa mwezi.!!
Tuanzie hapo.
Akitaka msaada tupo wengi tupewe/tuuziwe hisa.
Hii Nchi haina viongozi
 
Hii Nchi haina viongozi
Lakini viongozi wanatokana na jamii yetu.
Either wrong governance or genetical disorders to the masses.
We are not serious on crucial and sensitive matter's such as economy and technology building capacities.
Ukipanda bangi utavuna bangi sio pamba.
 
Sasa hivi TTCL PESA huwezi kutuma pesa wala huduma ya lipa kwa simu haipo. ukiwauliza wanakwambia wanafanya marekebisho.
Marekebisho zaidi ya wiki kweli!

Mbona mitandao mingine huwa wanafanya saa sita usiku hadi saa 11 alfajiri huduma inakuwa imerejea!
Nilikuwa na kahela kadogo imebidi ninunue bundle tu maana haina uwezo wa kutuma kwenda mitandao mingine na hata mawakala wenyewe wa kutafuta
 
Sasa hivi TTCL PESA huwezi kutuma pesa wala huduma ya lipa kwa simu haipo. ukiwauliza wanakwambia wanafanya marekebisho.
Marekebisho zaidi ya wiki kweli!

Mbona mitandao mingine huwa wanafanya saa sita usiku hadi saa 11 alfajiri huduma inakuwa imerejea!
Nilikuwa na kahela kadogo imebidi ninunue bundle tu maana haina uwezo wa kutuma kwenda mitandao mingine na hata mawakala wenyewe wa kutafuta
Pole sana
 
Baada ya ripoti ya CAG Kutolewa na kueleza madudu ya TTCL, Rais Samia Hassan amependekeza shirika hilo la umma libaki kusimamia mkongo wa Taifa tu, lachane na biashara ya mawasiliano ya simu.

Kwa kauli hii ya Rais bila shaka huu ni uamuzi kamili wa kuizika rasmi TTCL kwenye simu za viganjani.

Sasa sijui hizi line zetu itakuwaje yaani, tutafidiwa chochote au ndio vile tena?

Tunaitakia kila la heri.
Biashara ya mawasaliana ya Simu inalipa sana tatizo wanaopewa dhamana ni wajinga na wapumbavu kumbuka Tanzania nzima watu wakisema tu, hallow haya makampuni yanaingiza kiasi gani
 
Mawakala wote wa Tpesa wameachana nao.yaani ni kama shirika limekufa..nadhani ndio ilikuwa nia yao!Magufuli alishalifufua hili shirika likatishia hadi mashirika mengine ya simu..Mama amekuja kumtoa Waziri Kindamba aliyelifanya shirika lipae akamleta Ulanga,matokeo yake sote tumeyaona!
 
Back
Top Bottom