Kwako Jemedari Said, JefLea na Collegemate Wilson Oruma

Kwako Jemedari Said, JefLea na Collegemate Wilson Oruma

Mleta mada una akili kubwa umeandika jambo kwa weredi.
Mimi nilichoelewa ni kuwa, barua rasmi ya Simba ya kusema hawatacheza mchezo dhidi ya Yanga ilitosha kwa bodi ya ligi kuchukua hatua stahiki dhidi ya Simba na sio kutangaza kuhairisha mchezo. Yanga wana haki ya kudai fidia na kupewa haki zote.
 
Simba hanamamlaka ya kuhairisha mchezo alisema lakini yawezekana hakuwana maanisha ila aliwatumia barua bodi ya ligi juu ya kusudio lake! Hila baada ya kusomanakujiridhisha waliahirisha mchezo ili wafanye uchunguzi kwanini Simba alizuiwa kuingia uwanjani! Simba ana kesi mwenye mpira wake ndye kaahirisha mchezo wewe chura una lipi la kusema!
Hoja za Yanga ni dhidi ya bodi ya ligi kushindwa kuwapa point tatu baada ya Simba kutangaza rasmi hatacheza ule mchezo.

Uamuzi wa bodi ya ligi kutangaza kuhairisha mechi ya Yanga dhidi ya Simba baada ya Simba kutangaza rasmi kutokucheza ule mchezo ulilenga kuinyima Yanga point tatu za mezani, jambo ambalo Yanga wamelitengenezea madai.
 
Yanga kamwe haitakuja kupewa hizo Points hata Mahakama yoyote duniani, dawa hapa ni kukubali tu kucheza derby tarehe itakayopangwa tena na TFF
 
Hata hii ni tafsiri yako, kama ni hivyo hizo Points 3 wadaini Simba na sio bodies ya ligi. Maana bodi ilishatoa taarifa ya kuahirisha mechi. Maana yake hata Simba wangetengua barua baada ya tangazo la TFF na kusema wataenda uwanjani bado mechi isingechezwa kisheria! Points 3 kwa mwamuzi gani aliyekuwepo pale uwanjani zaidi ya Yanga na mashabiki wao?
 
Tunaendelea kuaminishwa kwa vitendo huko utopoloni mwenye akili ni mmoja tu.

Kuanzia point namba 2 na 3 ndio hayo hao wachambuzi wameyasimamia na wewe umekiri ni makosa kutoka kwa bodi ya ligi sasa hao wachambuzi kosa lao lipi?
 
Ili Simba waweze kucheza mchezo ule walipaswa waandike barua nyingine ya kuitengua barua ya kwanza. Simba ni taasisi, walitoa maamuzi ya kugoma kucheza na waka communicate na t
Taasisi huska na General public. Kwahiyo hata wangepeleka timu uwanjani bila kwanza kutengua barua Ile, hiyo timu isingekuwa Simba, hao wangekuwa wahuni tu na Bodi isingepaswa kuwapokea. Barua Ile ya kugoma hadi leo haijatengiliwa. Simba waligoma na kwa barua rasmi kabisa.
Acha utahira bana unawadhalilisha utopolo yanga
 
Hiyo ni tafsiri yako mkuu, tafsiri yangu mimi Bodi waliahirisha mchezo ambao tayari haupo. Simba waligoma kucheza mechi na kwa maandishi na barua ya kugoma ipo na hajawahi kutenguliwa. Bodi hakuna walichoahirisha. Waaahirishe wasihahirisha mchezo ulikuwa tayari haupo kwakuwa Simba walikuwa wameshagoma. Ni kweli Bodi walipaswa wafanye huo utaratibu. Kutokufanya huo utaratibu maana yake Bodi walikiuka kanuni, kama ndivyo, ukiukwaji huo wa Kanuni hauwezi kufanya Yanga ikose haki yake.

Unachosema wewe maana yake hivi.. fikiria unatakiwa kulipa deni kesho kwa
ku with draw pesa bank ila anayekudai mmekubaliana mtakutana bank umlipe .. kisha mdai wako atoe taarifa polisi kuwa anawasiwasi kesho atavamiwa kuporwa pesa zake bank then polisi waamue kuwaambia bank
Kesho msifungue ofisi.. ila bado wewe ujiendee bank ujikute uko peke yako hakuna wa kukuhudumia ila bado useme mi ndo nishakulipa maana nilifika bank hukuja.. wakat ki uhalisia ulikutana na walinzi maana hata hao wafanyakazi wa bank ambao wangekuhudumia hawakuwepo maana waliambiwa wasije hakuna siku kazi hiyo..

Sasa wewe unaona hapo uko sahihi kung'ang'ania kuwa umelipa deni?

Wanachotakiwa kufanya yanga ni kuidai bodi ya ligi gharama ilizoingia za mchezo sio point. Maana hakuna kilichofanyika. Ili upate point ilitakiwa Bodi waache waone simba kama
Hawajaja basi taratibu zifatwe.. simba hakwenda uwanjani kwa sababu bodo walihairisha mechi... kama haki ya point alikuwa nayo simna 2021 maana marefa na officials wote walikuwepo
 
Mbona unamtoa Yanga kwenye makosa wakati barua ya bodi inaeleza kuwa walinzi ambao baadhi yao walifahamika kwa sura kuwa ni walinzi wa Yanga walienda uwanjani kuanzisha vurugu?
Walinzi wa Yanga ni kina nani ? Wbu wa identify kwanza
 
Watajwa hapo juu tangu juzi hadi leo baada ya habari ya Yanga kuandika barua kuomba pointi 3 kutoka Bodi ya Ligi, Mmekuwa kwa kujiamini mkidai kuwa Yanga hawezi kupata pointi hizo kwakuwa Mechi iliahirishwana na Bodi ya Ligi na Simba asingeweza kupeleka timu uwanjani wakati mchezo umeahirishwa.

Lakini mnasahau mambo yafuatayo.

1. Simba kwa barua rasmi aliutarifu umma kuwa hachezi mchezo ule. Kwahiyo Simba aligoma kucheza mchezo, yaliyofuata yote baada ya hapo hayabadilishi chochote kwenye hilo. Hivyo, mtu anaweza kusema Bodi ya Ligi hakuna walichoahirisha kwakuwa hadi wanakaa kikao Simba haikuwa imebadilisha msimamo. Hivyo iko wazi kikao cha Bodi ya Ligi na maamuzi yake yalikuwa juu ya kitu ambachi hakipo. They decided on nothing. Mechi iliisha kwa barua ya Simba hadi wanakaa mechi ilikuwa hamna. Huwezi kiahirisha mchezo ambao tayari upande mmoja umeshasema haupo tena kwa barua rasmi.

2. Baada ya barua ya mgomo ya Simba, Bodi wakafanya Kosa la kuitisha kikao na kufanya boko la kiahirisha mechi ambayo tayari haikuwepo kwakuwa Simba walikuwa wameshasema hawachezi na kwa barua rasmi.
3. Bodi wakacheza Boko la tatu, wakaacha kupeleka Maafisa wa mechi Ili kukamilisha utaratibu wa kuwapa Yanga Pointi 3 kwa mjibu wa Kanuni. Yanga kwa kulijua hilo wakapeleka timu uwanjani.

Kwakuwa Simba waligoma kucheza mchezo, ilikuwa ni wajibu wa Bodi kuendelea na taratibu. Sasa basi, kwakuwa Simba alikosea, Bodi ya Ligi nayo ikakosea, mtu hawezi kusema kuwa makosa ya Bodi ya Ligi yanaifaidisha Simba. Simba ataadhibiwa kwa kugoma kucheza mchezo bila sababu, Bodi ya Ligi itaadhibiwa kwa kushindwa kuwema taratibu za kuipa Yanga pointi 3 kwa mjibu wa kanuni. Na baada ya hayo, yatatoka maelekezo ya yanga kupewa haki yake kwa mjibu wa sheria. Yanga hawezi kunyimwa haki yake kwa makosa ya Bodi ya Ligi kushindwa kutafsiri Sheria.
Kiufupi bodi ya ligi imetoa boko sana na imeingia kwenye kikaango kibaya .Ila Point namba 1 sikubaliani nayo kiongozi

Wenye mamlaka ya kuendesha mchezo walishaahirisha mchezo hivyo kusingekuwa na uwezekano/ uhalali timu kwenda uwanjani
 
Watajwa hapo juu tangu juzi hadi leo baada ya habari ya Yanga kuandika barua kuomba pointi 3 kutoka Bodi ya Ligi, Mmekuwa kwa kujiamini mkidai kuwa Yanga hawezi kupata pointi hizo kwakuwa Mechi iliahirishwana na Bodi ya Ligi na Simba asingeweza kupeleka timu uwanjani wakati mchezo umeahirishwa.

Lakini mnasahau mambo yafuatayo.

1. Simba kwa barua rasmi aliutarifu umma kuwa hachezi mchezo ule. Kwahiyo Simba aligoma kucheza mchezo, yaliyofuata yote baada ya hapo hayabadilishi chochote kwenye hilo. Hivyo, mtu anaweza kusema Bodi ya Ligi hakuna walichoahirisha kwakuwa hadi wanakaa kikao Simba haikuwa imebadilisha msimamo. Hivyo iko wazi kikao cha Bodi ya Ligi na maamuzi yake yalikuwa juu ya kitu ambachi hakipo. They decided on nothing. Mechi iliisha kwa barua ya Simba hadi wanakaa mechi ilikuwa hamna. Huwezi kiahirisha mchezo ambao tayari upande mmoja umeshasema haupo tena kwa barua rasmi.

2. Baada ya barua ya mgomo ya Simba, Bodi wakafanya Kosa la kuitisha kikao na kufanya boko la kiahirisha mechi ambayo tayari haikuwepo kwakuwa Simba walikuwa wameshasema hawachezi na kwa barua rasmi.
3. Bodi wakacheza Boko la tatu, wakaacha kupeleka Maafisa wa mechi Ili kukamilisha utaratibu wa kuwapa Yanga Pointi 3 kwa mjibu wa Kanuni. Yanga kwa kulijua hilo wakapeleka timu uwanjani.

Kwakuwa Simba waligoma kucheza mchezo, ilikuwa ni wajibu wa Bodi kuendelea na taratibu. Sasa basi, kwakuwa Simba alikosea, Bodi ya Ligi nayo ikakosea, mtu hawezi kusema kuwa makosa ya Bodi ya Ligi yanaifaidisha Simba. Simba ataadhibiwa kwa kugoma kucheza mchezo bila sababu, Bodi ya Ligi itaadhibiwa kwa kushindwa kuwema taratibu za kuipa Yanga pointi 3 kwa mjibu wa kanuni. Na baada ya hayo, yatatoka maelekezo ya yanga kupewa haki yake kwa mjibu wa sheria. Yanga hawezi kunyimwa haki yake kwa makosa ya Bodi ya Ligi kushindwa kutafsiri Sheria.
Sasa mbona wewe mwenyewe unakiri bodi ya ligi ndiyo iadhibiwe na huamini Yanga atapewa point tatu kama wanavyosema hao waandishi uliowataja katika andiko lako?

Yaani unakubaliana na waandishi ambao kwenye tittle ya mada umepinga wanachokiamini.

Point 3 hampewi
1.Mlifika uwanjani nje ya muda wa timu kufika uwanjani
2.Saa ya mechi ilikuwa saa 1:15 ninyi mliondoka uwanjani chini ya saa hiyo.
(Kwa kifupi mlikimbia mechi kikanuni)

3.Hamkukaguliwa kama sheria zinavyotaka.
4.Mechi iliahirishwa na wanaosimamia ligi ndiyo maana hawakuleta makamishna na marefa
5.Ili upewe point 3 sharti mwamuzi wa kati awepo na athibitishe Simba hawakufika kwenye game.

Mtapewa point za meza ya mbao
😂😂😂
 
Watu wa simba mna upumbavy sna😂😂.. hivi kauli kufika taasisi kama simba ya kutipeleka timu uwanjani mnahisi ni nyepesi na ina athari gani kwenye mechi husika!!. Kisheria ni kosa ambalo timu inapaswa kupewa adhabu kali. Acheni upuuzi mbwa nyie
Kwa hiyo timu ikisema kwa barua rasmi kuwa haitaenda uwanjani, lakini ikaenda na kushinda mechi au kupata sare, bado timu pinzani inatakiwa ipewe point 3 kwa kuwa ile ilishatoa tamko la kutokwenda?
 
... hivi kauli kufika taasisi kama simba ya kutipeleka timu uwanjani mnahisi ni nyepesi na ina athari gani kwenye mechi husika!!. Kisheria ni kosa ambalo timu inapaswa kupewa adhabu kali. Acheni upuuzi mbwa nyie
Unaweza ukasema sipeleki timu uwanjani ili kumpoteza mpinzani, lakini ukaibuka na kushinda. Kwani mara ngapi makocha wanasema mchezaji wao tegemeo ataukosa mchezo, au yupo 50/50 kucheza, lakini baadaye mnamkuta kwenye starting XI ?
 
Nini Msingi wa Simba kugomea mchezo husika?.... Sababu ni Nini?..... Nini chanzo Cha tatizo?
 
Unaweza ukasema sipeleki timu uwanjani ili kumpoteza mpinzani, lakini ukaibuka na kushinda. Kwani mara ngapi makocha wanasema mchezaji wao tegemeo ataukosa mchezo, au yupo 50/50 kucheza, lakini baadaye mnamkuta kwenye starting XI ?
Huna akili kabisa😂😂... Yaani umewahi kusikia wapi na timu gani inafanya mind game ya kipumbavu na kijinga kiasi hiki?. Punguza utoto.... Kauli ya simba ina adhabu yake na sio sawa na kusema mchezaj fulan hata kuwepo. Mna tumia nn kuwaza asee!!
 
Umemjibu vizuri sana.
Tena sana, shida ukiweka ushabiki maandazi ndo matokeo yake, Simba na Bodi nani ana nguvu kisheria kuahirisha mchezo? kama bodi, ingeamua kukaa kimya na kupeleka maofisa wake uwanjani, Yanga angepewa point 3 na magoli 3 on the spot...bodi hata kama walipiga boko, kanuni waliyoitumia ngumu sana kuwatoa kwenye reli
 
Mleta mada una akili kubwa umeandika jambo kwa weredi.
Mimi nilichoelewa ni kuwa, barua rasmi ya Simba ya kusema hawatacheza mchezo dhidi ya Yanga ilitosha kwa bodi ya ligi kuchukua hatua stahiki dhidi ya Simba na sio kutangaza kuhairisha mchezo. Yanga wana haki ya kudai fidia na kupewa haki zote.
Bodi kwa kanuni walioitumia walisema pia kuna taarifa wamezipata kutoka kwa afisa usalama, we unazijua ni taarifa zipi uwalazimishe wasiahirishe mechi? kanuni walioitumia mtazurula dunia nzima hamtapata point za mezani...
 
Back
Top Bottom