Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,413
- 23,592
Kuna adui namba moja aliyetufikisha hapa tulipo kama Watanzania na adui huyo ni unafiki.Mimi nimemshauri Lisu namna ya kufika huko anakotaka kufika. Hiyo ni juu yake kuelewa kwa namna yako au Kwa namna atakayoona yeye
Jitihada zozote za kuupaka rangi ukweli, ili kupunguza makali yake, ni kuzidi kukomaza unafiki
Kuna njia mbili tu za kudanganywa ambazo CCM imezitumia kwa ufanisi mkubwa hapa kwetu
Kwanza ni kupiga vita ukweli na pili kuukumbatia uongo...ndoa ya CCM na uongo imewaacha uchi!
Mh. Lissu katundika bandera na kusimama kwa heshima kutetea ukweli, haki, na uhuru kwa wote
KIsha akasema kile anachokiamini toka moyoni kuwa ni kweli kwa nguvu na ujasiri na bila woga
Ukweli hupita katika hatua tatu. Kwanza, ni kudhihakiwa. Pili, ni kupingwa kwa nguvu. Tatu, ni kukubalika kwa wengi. Endelea kupiga hatua Mh. Lissu, taifa liko katika hatua ya tatu...tutafika tu watake wasitake!