Kwako Lusinde na Kenani; Dkt. Bashiru aliwahi kusema maneno haya akiwa Katibu Mkuu wa CCM. Je, hamkumuelewa enzi zile?

Nimetulia na kusoma hizi hoja naona kuna nondo alizitema ingawa bahati mbaya sana alijenga majukwaa ya kutishiana enzi zake na yanamtafuna sasa
Hapana watanzania tunakosea sana.
SIO watu wote wameumbwa Kwa AJILI ya Kupigana vita . Hata Malaika SIO wote wanapigana vita. Kuna wengine ni Wa kufikisha ujumbe tu.

Hata Martín Luther King Jr hakuwahi kushika mtutu Wa bunduki Bali watu walihamasika Kwa kufuatilia kauli zake zenye hamasa na Kutia Moyo na kipinga dhulma.
Wananchi ndio waliotakiwa wafanye mapinduzi ya fikra Kwa kauri za Dr. BASHIRU SIO yeye MTU Mmoja.

Kumbuka ALIKUA ni Katibu mkuu Wa Chama na alikisema chama chake sana .
Wananchi walitakiwa wahamasishane Kwa kurejea kauli za kizalendo na kimapinduzi SIO kusubiri Haki mezani kutoka kwenye Dola. Unategemea watu kama Akina Mahita na wengine walionufaika na ugandamizaji wanaweza kuangalia MTU Mmoja alete mabadiliko eti Kwa sababu ni Kiongozi Wa chama. Bunge la CCM utarajie lifanye mageuzi ya kikatiba Kwa sababu ya Bashiru amepinga uovu Wa watawala. Kumbuka , Kuna mlolongo MKUBWA Wa wezi wa Mali za umma na wanatumia udhaifu Wa Katiba kujilimbikizia Mali.
Dr. Bashiru roho ilikua inamuuma Lakini haikuwa Rahisi kuleta mabadiliko Bila nguvu ya umma. Wananchi wamelala wanasubiri Lema alete mabadiliko peke yake. Lisu anapigwa risasi na waliompiga wangeweza kupatikana Kwa nguvu ya umma lakini umma ukakaa kimya.

Tulia Akson akaja na kauli mbiu yake ya kunyooka na wakosoaji kama Akina BASHIRU na aliwalenga Wanasiasa majasiri wasioogopa kusema lakini wananchi walikaa kimya Bila kuandamana nchi nzima na kunyooka na uspika wake. Hayo ndiyo mageuzi na mapinduzi ya kifikra na kijamii.

Tumiwabeza watu wenye kauli zilizosheheni ukweli na uzalendo eti Kwa sababu tunataka wao ndio waseme na watende peke Yao tutachelewa sana na watawala kwa Kujua kuwa KUMBE ukweli unapimwa kutokana na itikadi basi watakua wanawanyamazisha au kunyooka nao halafu jamii inabaki kimya na wahuni wanalamba asali Bila kuwa na mzinga.
 

Hakuna kipindi CCM imefanya siasa za kishamba na kishenzi kama kipindi Bashiru ni katibu Mkuu. Kipindi hicho CCM ilishindwa kabisa kufanya siasa za ushawishi, ikaishia kutumia ulevi wa madaraka wa Magufuli kufanya siasa. Hiki kinachomkuta Bashiru leo ndio picha halisi kuwa demokrasia ndani ya CCM ni ndio mzee. Yeye Bashiru alipopota madaraka ndio aligeuka akawa kikwazo kikubwa cha demokrasia.
 

Uko sahihi kwa maelezo yako marefu, lakini huyo Bashiru sio muumini wa hayo usemayo. Kama angekuwa muumini wa haya maelezo yako tusingeona akishirikiana na Magufuli kunajisi chaguzi za nchi hii, na kuua nguvu ya wananchi kuhoji. Si yeye alikuwa anatambia kukaa madarakani kwa nguvu ya dola? Maelezo yako ni sahihi, lakini unachemka unapomfamya Bashiru ni mtu sahihi.
 
SIO kweli mkuu.

Kumbuka Mapolisi na usalama Wa Taifa wengi WALIKUA wanapigania maslahi na kuhongwa vyeo na madaraka. Bashiru asingekua na nguvu peke yake wakati Wabunge Wengi WALIKUA hawaoni pa kutokea na Kwa wazi wote walitegemea nguvu ya Dola.

Ingekua ni ngumu sana KUFANYA mabadiliko ya kikatiba Kabla ya awamu ya Pili ambapo walipanga kulitumia Bunge lile dhaifu kupitisha katiba ya Warioba. Hapo ndio malengo ya serikali Ile yalpokuwa. Pangekua na Katiba Nzuri na uongozi Bora sana Baadae. Mitandao ya wizi na kupeana madaraka kifamilia ilikua imesambaratishwa kabisa.

Hapo tungeweza Kukaa mezani na kulinda Taifa Bora.
Kwa Sasa Ndugu yangu hakuna Jambo la kizalendo linaloweza kufanyika Tena . Hata Katiba mpya haitawezekana mana imelenga kuwanufaisha Wanasiasa zaidi kimaslahi. Ni masuala ya utawala Tuu zaidi . Hakuna Welfare ya wananchi kuishi Maisha Bora kwenye nchi Yao.

Makazi Bora,Maji, chakula Bei nafuu n.k. hakuna. Katiba itawanufaisha Bado watawala na wamasiasa. Ni majina tu ya vyama yatabadilika lakini watu watakua ni hawa Hawa Akina Makamba ,Nape,Mwigulu, Ridhiwani,Mwinyi, Bashe, Musukuma n.k.

Awamu ya mabadiliko ya Katiba ilikua ni hii ya Pili ya JPM AMBAYO ilidondoka na kuokotwa na awamu iliyojipa Jina la awamu ya Sita Ili isogeze Mbele maazimio MENGI ikiwemo ya Katiba.

Kwa hiyo katiba inapaswa kuletwa awamu hii. Anayedhani kuwa anakubalika 2025 basi aingie kwenye uchaguzi chini ya Katiba mpya na si Vinginevyo.
 
Ndugu yangu ipo hivi.
Bashiru ameweka hoja mezani na kinachoendelea sasa ni CCM kudhihirisha udhaifu wake na ninavyomjua malkia alivyo na hasira za ndani kwa ndani muda huu Bashiru atakuwa under home arrest. Hatoonekana hadharani kwa muda hadi anyooke.

CCM ni zimwi ambalo lazima ulikubalie kila kitu hata kama gharama yake ni kuua nusu ya Watanzania.

Kataa CCM liokoe Taifa
 
Nimekuelewa
 
CCM ni kundi la fisi, mwenzao akichafuka na damu wanamtafuna mzima-mzima.
 
Bashiru sichoki kumsikiliza anaongea kwa mamlaka sana na ni vile hana mamlaka akiwa na hayo mamlaka watanzania mtalimia meno
Hahah.. jamaa Yuko vizuri sana. Anaongea kama mtu mwenye mamlaka. Anatufaa sana huyu mwamba. Tuondokane na Hawa lonyalonya
 
Umesahau na ile kauli aliyosema CCM lazima itumie dola kubaki madarakani.
Chama dola kwa maana chama kilicho madarakani kina advantage ya kutumia yale waliyoyafanya ili kupewa ridhaa ya kuendelea kubaki madarakani.
 
Vyema, ila sijaona alipokemea kusifia na kuwapigia mapambio watawala wakati akiwa madhabahuni. Kwenye Ukatibu Mkuu wake ndio mambo ya Mh Rais tunakushukuru kwa kutuletea Milion 500 kwa ajili ya kituo cha afya, nk yalianza na kushamiri! Sikusikia akisema Mh Rais hana pesa za kugawa kwa wananchi, pesa zote hupitishwa na Bunge. Leo ndio anakumbuka kwamba kusifia si sahihi?
 
Bashiru, hata kama yako makosa amewahi kufanya, ila haiondoi ukweli wake kuwa, ni kati ya vijana wachache wenye uchungu haswaa na nchi, hana skendo za wizi na ufisadi!

Bashiru Ally Ni hazina ya Taifa
Hivi Bashiru ni kijana mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…