Kwako Lusinde na Kenani; Dkt. Bashiru aliwahi kusema maneno haya akiwa Katibu Mkuu wa CCM. Je, hamkumuelewa enzi zile?

Kwako Lusinde na Kenani; Dkt. Bashiru aliwahi kusema maneno haya akiwa Katibu Mkuu wa CCM. Je, hamkumuelewa enzi zile?

Nimetulia na kusoma hizi hoja naona kuna nondo alizitema ingawa bahati mbaya sana alijenga majukwaa ya kutishiana enzi zake na yanamtafuna sasa
Hapana watanzania tunakosea sana.
SIO watu wote wameumbwa Kwa AJILI ya Kupigana vita . Hata Malaika SIO wote wanapigana vita. Kuna wengine ni Wa kufikisha ujumbe tu.

Hata Martín Luther King Jr hakuwahi kushika mtutu Wa bunduki Bali watu walihamasika Kwa kufuatilia kauli zake zenye hamasa na Kutia Moyo na kipinga dhulma.
Wananchi ndio waliotakiwa wafanye mapinduzi ya fikra Kwa kauri za Dr. BASHIRU SIO yeye MTU Mmoja.

Kumbuka ALIKUA ni Katibu mkuu Wa Chama na alikisema chama chake sana .
Wananchi walitakiwa wahamasishane Kwa kurejea kauli za kizalendo na kimapinduzi SIO kusubiri Haki mezani kutoka kwenye Dola. Unategemea watu kama Akina Mahita na wengine walionufaika na ugandamizaji wanaweza kuangalia MTU Mmoja alete mabadiliko eti Kwa sababu ni Kiongozi Wa chama. Bunge la CCM utarajie lifanye mageuzi ya kikatiba Kwa sababu ya Bashiru amepinga uovu Wa watawala. Kumbuka , Kuna mlolongo MKUBWA Wa wezi wa Mali za umma na wanatumia udhaifu Wa Katiba kujilimbikizia Mali.
Dr. Bashiru roho ilikua inamuuma Lakini haikuwa Rahisi kuleta mabadiliko Bila nguvu ya umma. Wananchi wamelala wanasubiri Lema alete mabadiliko peke yake. Lisu anapigwa risasi na waliompiga wangeweza kupatikana Kwa nguvu ya umma lakini umma ukakaa kimya.

Tulia Akson akaja na kauli mbiu yake ya kunyooka na wakosoaji kama Akina BASHIRU na aliwalenga Wanasiasa majasiri wasioogopa kusema lakini wananchi walikaa kimya Bila kuandamana nchi nzima na kunyooka na uspika wake. Hayo ndiyo mageuzi na mapinduzi ya kifikra na kijamii.

Tumiwabeza watu wenye kauli zilizosheheni ukweli na uzalendo eti Kwa sababu tunataka wao ndio waseme na watende peke Yao tutachelewa sana na watawala kwa Kujua kuwa KUMBE ukweli unapimwa kutokana na itikadi basi watakua wanawanyamazisha au kunyooka nao halafu jamii inabaki kimya na wahuni wanalamba asali Bila kuwa na mzinga.
 
Kama Mungu asingemuita kwake, 2025 ilikwa ni Dr. Bashiru!. Pascal Mayalla amchambua Dkt. Bashiru, adai aliandaliwa kuwa Rais 2025

Unaweza kuusikiliza uchambuzi huu kutoka DW
P

Hakuna kipindi CCM imefanya siasa za kishamba na kishenzi kama kipindi Bashiru ni katibu Mkuu. Kipindi hicho CCM ilishindwa kabisa kufanya siasa za ushawishi, ikaishia kutumia ulevi wa madaraka wa Magufuli kufanya siasa. Hiki kinachomkuta Bashiru leo ndio picha halisi kuwa demokrasia ndani ya CCM ni ndio mzee. Yeye Bashiru alipopota madaraka ndio aligeuka akawa kikwazo kikubwa cha demokrasia.
 
Mungu Bado ana watu wake ndani ya Taifa hili.
Ni ukweli usiopingika kama Hawatakuwepo watu aina ya Dr. Bashiru, Tundu Lisu, Mnyika ,Dr. Slaa, Polepole, Jaji Warioba, God bless Lema, Mch. Msigwa , Antony Mtaka, Askofu Bagonza,Askofu Shoo, Askofu Mwamakula, Mpina n.k. basi nchi hii itakua Mali ya Shetani kama zilivyo nchi nyingi za Ulaya ya Leo yenye kizazi kilichopotoka na Sasa Ulaya inaporomoka na kuondoka kwenye ushawishi wake kidunia. Tanzania inakwenda kuwa na watu wa hovyo na watawala watakua ni mapandikizi ya Wala rushwa ,mashoga, wauza madawa ya kulevya, wafanyabiashara walaghai wa kitaifa na kimataifa, nchi yenye vifo vingi vya magonjwa ya kutengeneza, wawekezaji wezi wanaokuja na makaratasi wanaondoka na mabilioni ya Dola ,wasagaji, watoto wahovyo wasio na maadili,nchi isiyojali maadili ya kifamilia na kiutumishi.

Watanzania tukidhani hii nchi ni ya mtu mmoja na wale anaowapenda na kuwapa madaraka tutakua wendawazimu na Leo wameanza kutangazia Dunia kuwa watanzania wengi wengi ni wagonjwa wa akili. Maana yake ni kwamba Kuna siku watakua wanawakamata watu na kuwafunga pingu za miguuni na mikanoni na kutangazia ulimwengu kuwa huyu ni kichaa tunampeleka Mirembe.

Wameshiba na watoto wao lakini Bado wanatuchagulia viongozi waovu na wabaya wasiofaa ,wezi na wahuni Kwa sababu wametudharau bila kujua kuwa dharau zao ni Kwa sababu ya maskini na sio utajiri wao. Ndio,ni Kwa sababu ya watoto wa maskini wanaowalinda huku wao na watoto wao wakistarehe na kuwatukana na kusema kuwa wanakula kutokana na urefu wa kamba zao.

Ipo siku watoto wa maskini watajua kuwa hawana kesho ya watoto na wajukuu zao kama wataendelea kuwalinda wezi na wahuni.

Dr.Bashiru ni Sauti ya wanyonge ole wake mtu atakayepingana na sauti ya Wanyonge.
Wakulima Mmesahau kuwa Hawa wanaowaletea Mbolea wameshapiga dili zao kwenye miamala na Mbolea ni geresha ndio maana hata Mungu amewanyima mvua? Hiyo Mbolea labda muweke kwenye pesa za Mikopo labda zitaota na kuzaa Dola. Mvua ni Chache sana. Na wale mliowekeza kwenye kilimo Cha umwagiliaji Sasa ndio mmeambiwa marufuku kutumia maji ; mana wameshindwa kutafuta vyanzo vya maji Kwa ajili ya maji ya kunywa Dar es Salaam Jiji linalokaribiana na mito mikubwa kama Ruvu, Wami, na Rufiji, Mito inayohitaji tu uzalendo kuongeza uzalishaji na sio mvua.
Ukiwauliza mbona maji kwenye Mito hiyo Bado yanaingia Baharini hawana majibu zaidi ya kukaa ofisini na kalamu na kuandika dodoso za vikao na kulipana posho na Sasa Wanakwenda Tanga kucheza michezo ya kuvuta kamba na kukimbiza Kuku Kwa pesa za Mikopo Toka Oman , Falme za Kiarabu na Kwa Wale watetezi wa ndoa za jinsia Moja na nyingine zisiyo na Ziwa kubwa kama Ziwa Victoria Wala ardhi kubwa kama tuliyonayo lakini Wana uzalendo TU na akili zao wamezitumia vizuri kuliko wanyama.

Shame on you .Mmebaki kumshambulia Dr.Bashiru ; mnataka awalambe nyayo zenu zilizokanyaga jasho la wanyonge.

Uko sahihi kwa maelezo yako marefu, lakini huyo Bashiru sio muumini wa hayo usemayo. Kama angekuwa muumini wa haya maelezo yako tusingeona akishirikiana na Magufuli kunajisi chaguzi za nchi hii, na kuua nguvu ya wananchi kuhoji. Si yeye alikuwa anatambia kukaa madarakani kwa nguvu ya dola? Maelezo yako ni sahihi, lakini unachemka unapomfamya Bashiru ni mtu sahihi.
 
Huyu nduli mnafiki ndio alikuwa Engineer wa wizi wa kura mkubwa kuwahi kutokea Tanzania uliofanywa na CCM, waliiba viti vyote vya ubunge wa upinzani na kuwabambikia kesi na wengine kufungwa bila sababu, yote chini ya huyu mwehu, sasa hana sponsor wenzake wamemgeuka mirija ya vyeo na pesa imekatwa hana tofauti na wahuni kama Sabaya na Makonda, roho mbaya inalipa
SIO kweli mkuu.

Kumbuka Mapolisi na usalama Wa Taifa wengi WALIKUA wanapigania maslahi na kuhongwa vyeo na madaraka. Bashiru asingekua na nguvu peke yake wakati Wabunge Wengi WALIKUA hawaoni pa kutokea na Kwa wazi wote walitegemea nguvu ya Dola.

Ingekua ni ngumu sana KUFANYA mabadiliko ya kikatiba Kabla ya awamu ya Pili ambapo walipanga kulitumia Bunge lile dhaifu kupitisha katiba ya Warioba. Hapo ndio malengo ya serikali Ile yalpokuwa. Pangekua na Katiba Nzuri na uongozi Bora sana Baadae. Mitandao ya wizi na kupeana madaraka kifamilia ilikua imesambaratishwa kabisa.

Hapo tungeweza Kukaa mezani na kulinda Taifa Bora.
Kwa Sasa Ndugu yangu hakuna Jambo la kizalendo linaloweza kufanyika Tena . Hata Katiba mpya haitawezekana mana imelenga kuwanufaisha Wanasiasa zaidi kimaslahi. Ni masuala ya utawala Tuu zaidi . Hakuna Welfare ya wananchi kuishi Maisha Bora kwenye nchi Yao.

Makazi Bora,Maji, chakula Bei nafuu n.k. hakuna. Katiba itawanufaisha Bado watawala na wamasiasa. Ni majina tu ya vyama yatabadilika lakini watu watakua ni hawa Hawa Akina Makamba ,Nape,Mwigulu, Ridhiwani,Mwinyi, Bashe, Musukuma n.k.

Awamu ya mabadiliko ya Katiba ilikua ni hii ya Pili ya JPM AMBAYO ilidondoka na kuokotwa na awamu iliyojipa Jina la awamu ya Sita Ili isogeze Mbele maazimio MENGI ikiwemo ya Katiba.

Kwa hiyo katiba inapaswa kuletwa awamu hii. Anayedhani kuwa anakubalika 2025 basi aingie kwenye uchaguzi chini ya Katiba mpya na si Vinginevyo.
 
Ndugu yangu ipo hivi.
Bashiru ameweka hoja mezani na kinachoendelea sasa ni CCM kudhihirisha udhaifu wake na ninavyomjua malkia alivyo na hasira za ndani kwa ndani muda huu Bashiru atakuwa under home arrest. Hatoonekana hadharani kwa muda hadi anyooke.

CCM ni zimwi ambalo lazima ulikubalie kila kitu hata kama gharama yake ni kuua nusu ya Watanzania.

Kataa CCM liokoe Taifa
 
KWAKO MH LUSINDE NA MH KENANI;DK BASHIRU ALIWAHI KUSEMA MANENO HAYA AKIWA KATIBU MKUU WA CCM,JE HAMKUMUELEWA ENZI ZILE!??

Leo 17:50hrs 20/11/2022

1. "Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu cha CCM na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi,mijizi,wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje".

2. "Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike".

3. "Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho";

4. "Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani".

5. "Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa,akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura".

6. "Napenda kuwafahamisha kwamba Hussein Bashe sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi,kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi,Bashe na Nape Nnauye ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. Nape kidogo ana joto zaidi kuliko Bashe. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa Nape na Bashe ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya Bashe bungeni inafikirisha".

7. "Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu".

8. "Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi".

9. "Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya Makonda" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya Makonda" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Makonda". Kuna wakati huwa namsikia Makonda akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako,hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu" .

10. "Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania,nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno".

Kwa hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh Daktari Bashiru alikuwa ni mwanadamu wa aina gani,na alidhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani,"Nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko" tulifundishwa hivyo na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

-Hofu yenu iko hapa.

Mnasema huenda he is ready for the worse !! Come what may ! Che guevara alisema “ its better to die standing than to live kneeling “. !!

Shida nyingine ndani ya chama,Vigogo ndani ya chama wanajua kabla haujaanzisha vita na kamati kuu ya chama,hakikisha kwanza una back-up ya kutosha kupitia wenyeviti wa mikoa na wilaya,ukiisha kusanya hiyo support ndio twende sasa na ‘twanga, nikutwange’ mpaka ndani ya vikao vya ndani,mifano ni minyukano ya Chama tola ile dhana ya kuvua gamba hadi uchaguzi wa 2015.

Niseme tu kama mwanazuoni,maneno ya Daktari Bashiru ni Phd in delivery,Daktari Bashiru ni freemind, hategemei hisani kama ninyi, ndio maana pamoja na kupewa ukatibu mkuu wa CCM na Rais Magufuli ila bado alikuwa anaongea maneno yenye ukakasi mno dhidi ya CCM na Rais Magufuli aliyachukua hayo kama feedback na kuyatafutia solution.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854.

-Bachelor of Business Administration in International Business

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Nimekuelewa
 
Ndugu yangu ipo hivi.
Bashiru ameweka hoja mezani na kinachoendelea sasa ni CCM kudhihirisha udhaifu wake na ninavyomjua malkia alivyo na hasira za ndani kwa ndani muda huu Bashiru atakuwa under home arrest. Hatoonekana hadharani kwa muda hadi anyooke.

CCM ni zimwi ambalo lazima ulikubalie kila kitu hata kama gharama yake ni kuua nusu ya Watanzania.

Kataa CCM liokoe Taifa
CCM ni kundi la fisi, mwenzao akichafuka na damu wanamtafuna mzima-mzima.
 
Bashiru sichoki kumsikiliza anaongea kwa mamlaka sana na ni vile hana mamlaka akiwa na hayo mamlaka watanzania mtalimia meno
Hahah.. jamaa Yuko vizuri sana. Anaongea kama mtu mwenye mamlaka. Anatufaa sana huyu mwamba. Tuondokane na Hawa lonyalonya
 
Umesahau na ile kauli aliyosema CCM lazima itumie dola kubaki madarakani.
Chama dola kwa maana chama kilicho madarakani kina advantage ya kutumia yale waliyoyafanya ili kupewa ridhaa ya kuendelea kubaki madarakani.
 
KWAKO MH LUSINDE NA MH KENANI;DK BASHIRU ALIWAHI KUSEMA MANENO HAYA AKIWA KATIBU MKUU WA CCM,JE HAMKUMUELEWA ENZI ZILE!??

Leo 17:50hrs 20/11/2022

1. "Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu cha CCM na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi,mijizi,wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje".

2. "Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike".

3. "Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho";

4. "Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani".

5. "Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa,akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura".

6. "Napenda kuwafahamisha kwamba Hussein Bashe sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi,kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi,Bashe na Nape Nnauye ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. Nape kidogo ana joto zaidi kuliko Bashe. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa Nape na Bashe ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya Bashe bungeni inafikirisha".

7. "Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu".

8. "Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi".

9. "Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya Makonda" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya Makonda" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Makonda". Kuna wakati huwa namsikia Makonda akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako,hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu" .

10. "Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania,nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno".

Kwa hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh Daktari Bashiru alikuwa ni mwanadamu wa aina gani,na alidhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani,"Nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko" tulifundishwa hivyo na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

-Hofu yenu iko hapa.

Mnasema huenda he is ready for the worse !! Come what may ! Che guevara alisema “ its better to die standing than to live kneeling “. !!

Shida nyingine ndani ya chama,Vigogo ndani ya chama wanajua kabla haujaanzisha vita na kamati kuu ya chama,hakikisha kwanza una back-up ya kutosha kupitia wenyeviti wa mikoa na wilaya,ukiisha kusanya hiyo support ndio twende sasa na ‘twanga, nikutwange’ mpaka ndani ya vikao vya ndani,mifano ni minyukano ya Chama tola ile dhana ya kuvua gamba hadi uchaguzi wa 2015.

Niseme tu kama mwanazuoni,maneno ya Daktari Bashiru ni Phd in delivery,Daktari Bashiru ni freemind, hategemei hisani kama ninyi, ndio maana pamoja na kupewa ukatibu mkuu wa CCM na Rais Magufuli ila bado alikuwa anaongea maneno yenye ukakasi mno dhidi ya CCM na Rais Magufuli aliyachukua hayo kama feedback na kuyatafutia solution.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854.

-Bachelor of Business Administration in International Business

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Vyema, ila sijaona alipokemea kusifia na kuwapigia mapambio watawala wakati akiwa madhabahuni. Kwenye Ukatibu Mkuu wake ndio mambo ya Mh Rais tunakushukuru kwa kutuletea Milion 500 kwa ajili ya kituo cha afya, nk yalianza na kushamiri! Sikusikia akisema Mh Rais hana pesa za kugawa kwa wananchi, pesa zote hupitishwa na Bunge. Leo ndio anakumbuka kwamba kusifia si sahihi?
 
Back
Top Bottom