KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,789
- 4,951
Kwako Rais wa JMT Mhe.Samia Suluhu Hassan, ninakusalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mhe.Rais, kwa namna ya pekee pekee ninapenda kuchukua nafasi kukupongeza kwa kuwa kielelezo Cha safari ya mabadiliko makubwa kwenye nyanja mbalimbali katika Taifa letu na kubwa zaidi litakalokumbukwa ni kuingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa 2025 kukiwa na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Mhe.Rais, siku ya Jana katika Baraza la Eid ulitukumbusha wajibu wa wafanyabiashara kulipa Kodi Kwa Serikali inayostahili na sio kuidhulumu Serikali. Ni kweli Mhe.Rais suala Hilo la wafanyabiashara kuidhulumu mapato ya Kodi Serikali lipo sana na zaidi wanunuaji hawalipi umuhimu mkubwa. Kivipi?
Mnunuaji ndio alitakiwa kuwa mtu wa kwanza na WA mwisho kubanana na huyu mfanyabiashara kumpatia risiti hali ya mzigo alioununua lakini wanunuaji hawafanyi hivyo na ninaamini Serikali ikianza na wanunuaji , wafanyabiashara watatoa risiti halali Kwa kiasi Fulani itapunguza tatizo.
Kwenye suala la kupewa risiti Kuna mambo matatu:
Kwanza, Kuna wafanyabiashara wanatoa risiti pungufu au hawatoi kabisa Kwa kigezo Cha punguzo la Bei. Mnunuaji anapewa punguzo la Bei ili akubali kuandikiwa risiti pungufu au asipewe kabisa.
Pili, Kuna wafanyabiashara wanatoa risiti za kutembelea njiani Kwa wateja. Hapa mteja anapewa risiti hata ya wiki iliyopita ya mzigo tofauti ili tu atumie kutembelea njiani. Wanaotumia mbinu hii wakikutana na ukaguzi wanasema mzigo nilinunua wiki iliyopita lakini sikuuchukua ndio nimeuchuka Leo.
Tatu, Kuna wafanyabiashara wanatoa Bado risiti za mkono. Mashine ya EFD anakuwa nayo kama dharula ya ukaguzi ikiwepo lakini wateja anawaandikia risiti za mkono na ukiuliza juu ya risiti ya EFD anakuambia mashine ni mbovu , Kwa kuwa mteja anakuwa amekipenda hiko kitu na Bei ni nzuri anachukua tu risiti ya mkono.
Haya ndio makundi ya wafanyabiashara na risiti wanazotoa, hapa sijazungumzia wanaotoa risiti kamili na halali Kwa sababu kundi hili ni wazalendo.
Mhe. Rais ,wakati ukiwaapisha viongozi uliowateua karibuni ulitilia mkazo suala la namba moja ya utambulisho Kwa Kila mtu.
Nafikiri suala Hilo la namba moja ya utambulisho linaweza kutumika kudhibiti dhuluma ya mapato inayofanywa na wafanyabiashara kwenye suala la risiti za EFD.
Hivyo Mhe.Rais nashauri suala hili la risiti za EFD kutoka Kwa wafanyabiashara liachwe Kwa wanunuaji walishughulikie ila Serikali iwahamasishe wanunuaji Kwa gawio kidogo kutokana na manunuzi.
Kwa kuwa Leo hii mteja anayepewa punguzo la Bei na mfanyabiashara hatoona umuhimu wa kudai risiti kutokana na punguzo basi ninaamini gawio la Serikali litamchochea kudai risiti. Kwa kuwa itakuwa ngumu Serikali kujua Bei halisi mzigo wa mteja basi huyu mteja adai risiti hata ya punguzo ili apate gawio.
Kukiwa na gawio ,mnunuaji hatoridhishwa na jibu la mashine ya EFD ni mbovu hivyo inawezekana akaondoka bila kununua Kwa huyo mfanyabiashara na atafanya hima kumtafuta mfanyabiashara anayetoa risiti za EFD na pia suala la kupewa risiti za mkono litapungua kama sio kuisha kabisa maana risiti ya mkono Haina gawio mnunuaji akihamasika na gawio itamchochea zaidi na zaidi.
Kuhusu kupewa risiti za kutembelea njiani kukwepa ukaguzi basi nalo litakwisha kabisa ,mnunuaji atataka risiti halali ya mzigo alionao ili naye gawio lisimpite.
Kwa kuwa gawio hili litahusu manunuzi yote yanayofanywa ninaamini wanunuaji watahamasika bila kujalisha ukubwa au gharama za mzigo na hili litawakumbusha wanunuaji Kila mara kudai risiti za EFD.
THE WAY FORWARD: NINI KIFANYIKE?
Kwanza, namba ya utambulisho ambayo Mhe.Rais umekuwa ukisisitiza itumike. Kwa kuwa itakuwa ni namba maalumu Kwa Kila mtu hivyo Kila mtanzania atakuwa na usajili maalumu. Mashine za EFD ziwezeshwe sehemu ya kuweka hiyo namba ya utambulisho na kwenye Kila risiti hiyo namba ionekane.
Namba hiyo ndio itumike kama jina lako kuingia kwenye mfumo unapotaka kulitoa gawio lako.
Pili, elimu itolewe Kwa wingi juu ya gawio Hilo la Serikali katika manunuzi. Uelewa unapokuwa mkubwa unafanya utekelezaji uwe wa juu zaidi.
Tatu, utaratibu huo unaweza kuitwa GAWIO LA SERIKALI KWA WANUNUAJI/ KATIKA MANUNUZI.
Mwisho, ninaamini wanunuaji wakitumika vizuri Kwa kuwapa gawio kutokana na manunuzi wanayofanya watasaidia kudhibiti suala la ukwepaji Kodi kutoka Kwa wafanyabiashara.
Wako katika ujenzi wa Taifa,
Mhe.Rais, kwa namna ya pekee pekee ninapenda kuchukua nafasi kukupongeza kwa kuwa kielelezo Cha safari ya mabadiliko makubwa kwenye nyanja mbalimbali katika Taifa letu na kubwa zaidi litakalokumbukwa ni kuingia kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa 2025 kukiwa na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Mhe.Rais, siku ya Jana katika Baraza la Eid ulitukumbusha wajibu wa wafanyabiashara kulipa Kodi Kwa Serikali inayostahili na sio kuidhulumu Serikali. Ni kweli Mhe.Rais suala Hilo la wafanyabiashara kuidhulumu mapato ya Kodi Serikali lipo sana na zaidi wanunuaji hawalipi umuhimu mkubwa. Kivipi?
Mnunuaji ndio alitakiwa kuwa mtu wa kwanza na WA mwisho kubanana na huyu mfanyabiashara kumpatia risiti hali ya mzigo alioununua lakini wanunuaji hawafanyi hivyo na ninaamini Serikali ikianza na wanunuaji , wafanyabiashara watatoa risiti halali Kwa kiasi Fulani itapunguza tatizo.
Kwenye suala la kupewa risiti Kuna mambo matatu:
Kwanza, Kuna wafanyabiashara wanatoa risiti pungufu au hawatoi kabisa Kwa kigezo Cha punguzo la Bei. Mnunuaji anapewa punguzo la Bei ili akubali kuandikiwa risiti pungufu au asipewe kabisa.
Pili, Kuna wafanyabiashara wanatoa risiti za kutembelea njiani Kwa wateja. Hapa mteja anapewa risiti hata ya wiki iliyopita ya mzigo tofauti ili tu atumie kutembelea njiani. Wanaotumia mbinu hii wakikutana na ukaguzi wanasema mzigo nilinunua wiki iliyopita lakini sikuuchukua ndio nimeuchuka Leo.
Tatu, Kuna wafanyabiashara wanatoa Bado risiti za mkono. Mashine ya EFD anakuwa nayo kama dharula ya ukaguzi ikiwepo lakini wateja anawaandikia risiti za mkono na ukiuliza juu ya risiti ya EFD anakuambia mashine ni mbovu , Kwa kuwa mteja anakuwa amekipenda hiko kitu na Bei ni nzuri anachukua tu risiti ya mkono.
Haya ndio makundi ya wafanyabiashara na risiti wanazotoa, hapa sijazungumzia wanaotoa risiti kamili na halali Kwa sababu kundi hili ni wazalendo.
Mhe. Rais ,wakati ukiwaapisha viongozi uliowateua karibuni ulitilia mkazo suala la namba moja ya utambulisho Kwa Kila mtu.
Nafikiri suala Hilo la namba moja ya utambulisho linaweza kutumika kudhibiti dhuluma ya mapato inayofanywa na wafanyabiashara kwenye suala la risiti za EFD.
Hivyo Mhe.Rais nashauri suala hili la risiti za EFD kutoka Kwa wafanyabiashara liachwe Kwa wanunuaji walishughulikie ila Serikali iwahamasishe wanunuaji Kwa gawio kidogo kutokana na manunuzi.
Kwa kuwa Leo hii mteja anayepewa punguzo la Bei na mfanyabiashara hatoona umuhimu wa kudai risiti kutokana na punguzo basi ninaamini gawio la Serikali litamchochea kudai risiti. Kwa kuwa itakuwa ngumu Serikali kujua Bei halisi mzigo wa mteja basi huyu mteja adai risiti hata ya punguzo ili apate gawio.
Kukiwa na gawio ,mnunuaji hatoridhishwa na jibu la mashine ya EFD ni mbovu hivyo inawezekana akaondoka bila kununua Kwa huyo mfanyabiashara na atafanya hima kumtafuta mfanyabiashara anayetoa risiti za EFD na pia suala la kupewa risiti za mkono litapungua kama sio kuisha kabisa maana risiti ya mkono Haina gawio mnunuaji akihamasika na gawio itamchochea zaidi na zaidi.
Kuhusu kupewa risiti za kutembelea njiani kukwepa ukaguzi basi nalo litakwisha kabisa ,mnunuaji atataka risiti halali ya mzigo alionao ili naye gawio lisimpite.
Kwa kuwa gawio hili litahusu manunuzi yote yanayofanywa ninaamini wanunuaji watahamasika bila kujalisha ukubwa au gharama za mzigo na hili litawakumbusha wanunuaji Kila mara kudai risiti za EFD.
THE WAY FORWARD: NINI KIFANYIKE?
Kwanza, namba ya utambulisho ambayo Mhe.Rais umekuwa ukisisitiza itumike. Kwa kuwa itakuwa ni namba maalumu Kwa Kila mtu hivyo Kila mtanzania atakuwa na usajili maalumu. Mashine za EFD ziwezeshwe sehemu ya kuweka hiyo namba ya utambulisho na kwenye Kila risiti hiyo namba ionekane.
Namba hiyo ndio itumike kama jina lako kuingia kwenye mfumo unapotaka kulitoa gawio lako.
Pili, elimu itolewe Kwa wingi juu ya gawio Hilo la Serikali katika manunuzi. Uelewa unapokuwa mkubwa unafanya utekelezaji uwe wa juu zaidi.
Tatu, utaratibu huo unaweza kuitwa GAWIO LA SERIKALI KWA WANUNUAJI/ KATIKA MANUNUZI.
Mwisho, ninaamini wanunuaji wakitumika vizuri Kwa kuwapa gawio kutokana na manunuzi wanayofanya watasaidia kudhibiti suala la ukwepaji Kodi kutoka Kwa wafanyabiashara.
Wako katika ujenzi wa Taifa,