Kwakuwa kizazi chetu kimeshindwa... Tuwekeze katika kizazi kijacho!

Kwakuwa kizazi chetu kimeshindwa... Tuwekeze katika kizazi kijacho!

Uko Sahihi Mkubwa Aweda
Pengine tuna Tatizo la Kimsingi zaidi kuliko Mfumo wa Elimu. Hata kama tukiubadili Mfumo leo hatutapata mafanikio kwa kuwa hata kama tkiubadili mfumo na wahitimu wanaenda kufanya kazi katika mfumo uliocollapse ni lazima nia zao njema zitakuwa Transformed kuwa za Kifisadi. Ni vigumu kuwa mwadili wakati mfumo wetu wa kimamlaka unakusukuma upokee au kutoa Rushwa ili ufanikiwe.
Thats why nikasema thinking yetu ina matatizo lakini pia mfumo wetu wa kiutawala una Matatizo. Tanzania hii tunaishi kitumwa pasipo kujijua. Tunahitaji Kuibatiza nchi hii, tena ubatizo wa kuzamishwa katika maji izaliwe upya. Izaliwe upya katika kwa kubadili system ya Utawala, Kustructure upya kila kitu, sera za uchumi, afya, elimu, mahakama, ulinzi..kila kitu. Vitu vyote hivi vinategemeana na kila kimoja kinaathiri kingine. Iwapo tunahitaji mabadiliko ya kweli lazima tukae chini na kuisuka upya system ya nchi hii from zero. Ili kumwezesha daktari atibu kwa uhakika, engineer ajenge kwa moyo na akili thabiti, hakimu ahukumu kwa haki, polisi alinde usalama na haki mkulima alime kwa bidii, mfanyakazi afanye kazi kwa uhakika............. Kwa sababu hata tukibadili katika lakini mfumo wa utekelezaji wake ukawa ni huu huu wa sasa....Tunaendelea hivi hivi!

Ntulutumbi nimekupata,
Nakubaliana na wewe kuwa kila sehemu imeoza, serikali na sekta binafsi kote kunanuka rushwa na kuna kila aina ya matatizo. Kauli ya mbiu ya tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele ni aibu ya miaka 50.
Hoja yangu ni kuwa, kwa kuwa mahakama ni matatizo matupu, serikalini ( Ikulu, CAG, Takukuru, polisi nk) ni matatizo matupu, Bunge ndo usanii mtupu, tunahitaji kuanza mahali ktk kubadili au kubatiza ( as you said) nchi yetu. Hatuwezi kutangaza kwamba kuanzia tarehe 10/12/2011(mwaka wa 51 wa uhuru wetu) nchi yetu imebadilika. Hilo haliwezekani. Kwa kuwa mabadiliko (mabatizo ) haya tunayozungumzia siyo tukio la siku moja, ni mchakato wa zaidi ya miaka 5.
Kwa hiyo basi, kwa mapendekezo yangu, tunahitaji kuanza kwenye elimu. Hii ni kwa sababu elimu inafundishwa kwa watoto kuanzia miaka 3 au 5 chekechea hadi 21/25 - chuo kikuu ambao hawajachafuliwa nafsi zao kifisadi. Tukiwa na silabasi nzuri, siyo hii ya sasa ( silabasi inayozungumzia uzalendo, ubaya wa Rushwa, ubaya wa Uvivu, faida ya ufahamu mzuri wa ujasiriamali kukabiliana na umaskini), watoto ambao ni matunda ya mfumo huu mpya wa elimu, watakataa Rushwa, watakuwa wazalendo wakiwa mahakamani, serikalini, na Bungeni watatenda haki. Mashujaa wa kutaja orodha ya mafisadi bila woga kama Dr Slaa wataongezeka. Huu ndio utakuwa mwanzo mpya.
Hata hivyo, Serikali itakayosimamia mchakato huu wa kubadili nchi yetu lazima itangaze tarehe ya kuanza mchakato huo kama Nyerere alivyotangaza azimio la Arusha. Ijulikane tarehe x ( mf 10/12/2011) ni mwanzo wa kubadili nchi yetu kimfumo na kimaaadili japokuwa hatuwezi kusema itachukua muda gani. Vyombo vya habari vitangaze.
Pili, Lazima tukubaliane kuhusu mafisadi na wabadhirifu kabla hatujaanza mchakato huo. Kuna namna mbili. Kwanza ni kuwasamehe wote waliohusika kabla ya tarehe ya kubatiza nchi yetu ila warejeshe fedha zote walizoiba (Reconciliation).
Pili, ni kusema kwamba, wote waliofisadi nchi yetu huko nyuma tutawawajibisha kisheria kwa kuwapeleka ktk mahakama maalumu ya kubadili nchi yetu - ugumu wa hili la pili ni kuwa hakuna mbunge, mahakimu au viongozi wa serikali yetu watakaopona - kama wapo ni wachache sana. Majaji watakaosimamia mahakama hii ni wale wastaafu au walioopo wasiotiliwa shaka na majaji wenzao ktk utoaji wa hukumu - majaji wa namna hii wapo.
Tatu, hili litafanyika baada ya kupatikana kwa katiba mpya itakayokuwa imeondoa madhaifu yote yaliyojaa ktk katiba ya sasa inayompa rais madaraka makubwa sana - Rais mfalme. Na Rais atakayeongoza mabadiliko mabadiliko haya hawezi kuwa kikwete lazima awe mwingine ambaye hajahusishwa na kashfa ya aina yoyote - Rais mwenye Moral authority.
Thx
 
Sijui kwanini kila nkipitia post zote kwenye mind yangu nasikia mwangwi unavuma UONGOZI UONGOZI!
Nijaribu kuweka msawazo wa mambo hapa.
Kwenye post ya kufungulia mjadala huu, umezitaja nchi kadhaa duniani ikiwamo Japan...
Lakini nadhani tunaweza tukaongeza mifano zaidi ya nchi ambazo tukazitumia kama mifano bora, lakini kwa kupanua mjadala tusiishie tu kuzitaja hzo nchi. Tunahitaji kudadavua zaidi juu ya hizo nchi, zilitokaje, waliwezaje??
Ni kweli kuwa kila nchi hyo imepata kuwa na uongozi uliosimika namna bora ya kusimamia mustakabali wao, kwa mfano mdogo maarufu ninaoufahamu ni china na Mao.
Hivyo ukienda au tukichukua mfano wowote wa taifa lolote lazima kuna UONGOZI uliowezesha mabadiliko ya msingi ya jamii husika kujitambua na kuelekea kwenye muafaka wa taifa husika,
hata kama pale ambapo tutataja wanafalsafa kama Plato au wanasayansi kama Newton bado ulihitajika UONGOZI kuziwezesha falsafa hizo na kusuka mifumo yakinifu katika kupokea na kuendeleza sayansi!
UONGOZI ndio kila kitu katika jamii yoyote, sababu mpaka sasa hamna ushahidi wowote pale duniani kuwa kuna jamii iliwahi kusonga kwa juhudi binafsi za mtu mmoja mmoja, kwamba kila mtu anafanya lwake!
Tukiwa tunaangalia UONGOZI katika jamii husika hapo ndio tunaongelea SIASA kama ni shughuli nzima inayohusu uendeshaji wa utawala wa jamii, ikiwa ni pamoja na mipangilio ya utawala, umiliki na uendeshaji wa nguvu za umma (kwa uelewangu mdogo toka kwenye makala ya J. Ulimwengu).
Ninachotaka kusema hapa ni kwamba wakati tunajadili mustakabali wa kizazi kijacho ni lazima tuweke wazi kuwa kosa letu kizazi hichi limekuwa wapi? Na pia hamna jinsi tunakwepa kuwa sehemu ya kurekebisha makosa hayo kwani tukiyaacha hcho kizazi kijacho kitayachukulia kama utamaduni wao.
Baba wa Taifa alikuwa na ndoto yake juu ya hii nchi, bahati mbaya ndoto hyo haikupata kuwa ndoto ya watanganyika wote!
Jamii yetu kama jamii iliyojiviringisha kwenye mgogoro wa kiuongozi wa kisiasa na hii imekwamisha kila kitu.
Matatizo yote hayo tumeorodhesha ni matokeo ya kuanguka kwa UONGOZI katika SIASA ya nchi yetu.
Siamini kama kizazi kijacho kinaweza kuwa kizuri kama kinatoka kwa wazazi walio vurugika!
 
Nionavyo mie
Kwenye science kuna mambo ya mabadiliko yanayotokea na kuitwa 'reversible or irrevesible change'. Nadhani hili linahusika hata katika reality life, kama mtu akiharibikiwa ubongo ni lazima atakufa 'revesible death.
Sioni mahali ambapo kama taifa au jamii tunaweza tukaanzia na tukabadili historia kwa sasa, tuko kwenye irrevesible state.
Mfumo wa jamii hauwezi kusaidia watoto kujenga fikra tofauti na tulizonazo sasa. Watoto hujifunza zaidi kwa kuona vile vinavyofanyika na wazazi wao. Watoto wako wanaona nini sasa? Walimu wao wakoje? Wewe ukoje? Majirani wakoje? Mpaka hapo kutegemea kizazi kijacho ni vigumu.
Ukitafakari uongozi na penyewe unaona kuna changamoto kubwa. Sawa tutajitahidi tumweke kiongozi mzuri. Lakini watendaji ni wa aina gani? Ni wale wale walio na sura ya rushwa, uvivu, wasiokuwa na mawazo mapya. Anyway, anaweza akawatoa hao watendaji, wengine walio kama yeye atawatoa wapi?
Akifanikiwa hilo juu, je wazungu ambao mpaka sasa wana nguvu na wanatunyonya watakubali kuona soko lao linaharibiwa? Sasa si wazungu peke yao hata bara la asia ambao wanatuibia, je watakubali? Watamuua tu.
Tafakari wanafunzi wa vyuo vikuu ambao jamii inawatazama kama wasomi na sehemu ya mabadiliko ya mfumo wetu hakuna jipya zaidi ya ubinafsi na wangine kuishia kuwa vibaraka wa viongozi wa vyama na ushabiki usiokuwa na mantiki. Hata mahali walipo na kwa nafasi zao wameshindwa kuwa na faida kwa jamii inayowazunguka, tuwategemee wakianza kazi? (personal benefit)
Tafakari viongozi wa dini ambao jamii inawatazama kama watu wenye maadili, leo wana vituko vya kila aina. Wao ndio wauzaji wa madawa, wao ndo wezi, wabakaji, walawiti na la maana sana wanaleta migogoro ya kisiasa na kidini. Huko nako hakuna tumaini.
Tafakari familia zetu, huko ndio mwanzo wa haya yote. Iko wapi heshima ya familia, wapi upendo, wapi ushirikiano, wapi uzalendo?
Nyumbani kumejaa ubinafsi, ugomvi, maovu na vituko vya kila aina.
Kila mleta mabadiliko iwe ya kisiasa, ya kiuchumi, ya kisayansi alikuwa na strong will from his or her education, family or religion. Walilewa hawa kwenye hiyo hali na baadaye mfumo ukawasaidia wao kutimiza ndoto zao.
Now we have collapsed system na collapsed basis of will power, watoke wapi wakutukomboa. Hata wakiwa na good morals, system will fail them.
Hapa msemo wa jiokoe nafsi yako mwenyewe unatumika. Unaweza ukawagusa wachache wengine lakini changamoto kubwa ipo katika kuyatekeleza mawazo hayo. It needs more than personal sacrifice
 
Labda kuna jambo la kujiuliza.

Kauli mbiu ya kiongozi muasisi wa uhuru wa Tanganyika aliweka wazi. Ili Tanganyika iendelee ilikuwa inahitaji mambo manne.
1. Watu
2. Ardhwi
3. Siasa safi
4. Uongozi bora.

Sasa ni nini kilichokosokana mpaka nchi kadri siku zinavyokwenda inazidi kuwa masikini?
 
Kwa muda mrefu mimi nimekuwa nawaambia watu, kuwa sisi Waafrika tuna matatizo mengi ya kufikiria na kuthubutu,mtoa mada ametuambia tatizo hilo halipo Afrika kwa Waafrika bali lipo mpaka Marekani kwa Waafrika wa kule pamoja na kupata fusa zote.
Kwangu hii naiona kuwa ni changamoto na tufanye yafuatayo.
1-Tumeshajua matatizo yetu tufanyaje sasa?
2-Fikra zetu ziendane na hali ya sasa.
3-Tusidhani hatuna vitu vizuri vya kuanzia.
 
Nionavyo mie
Kwenye science kuna mambo ya mabadiliko yanayotokea na kuitwa 'reversible or irrevesible change'. Nadhani hili linahusika hata katika reality life, kama mtu akiharibikiwa ubongo ni lazima atakufa 'revesible death.
Sioni mahali ambapo kama taifa au jamii tunaweza tukaanzia na tukabadili historia kwa sasa, tuko kwenye irrevesible state.
Mfumo wa jamii hauwezi kusaidia watoto kujenga fikra tofauti na tulizonazo sasa. Watoto hujifunza zaidi kwa kuona vile vinavyofanyika na wazazi wao. Watoto wako wanaona nini sasa? Walimu wao wakoje? Wewe ukoje? Majirani wakoje? Mpaka hapo kutegemea kizazi kijacho ni vigumu.
Ukitafakari uongozi na penyewe unaona kuna changamoto kubwa.
1Sawa tutajitahidi tumweke kiongozi mzuri. Lakini watendaji ni wa aina gani? Ni wale wale walio na sura ya rushwa, uvivu, wasiokuwa na mawazo mapya. Anyway, anaweza akawatoa hao watendaji, wengine walio kama yeye atawatoa wapi?
Akifanikiwa hilo juu, je wazungu ambao mpaka sasa wana nguvu na wanatunyonya watakubali kuona soko lao linaharibiwa?
2 Sasa si wazungu peke yao hata bara la asia ambao wanatuibia, je watakubali? Watamuua tu.

3 Tafakari wanafunzi wa vyuo vikuu ambao jamii inawatazama kama wasomi na sehemu ya mabadiliko ya mfumo wetu hakuna jipya zaidi ya ubinafsi na wangine kuishia kuwa vibaraka wa viongozi wa vyama na ushabiki usiokuwa na mantiki
. Hata mahali walipo na kwa nafasi zao wameshindwa kuwa na faida kwa jamii inayowazunguka, tuwategemee wakianza kazi? (personal benefit)
Tafakari viongozi wa dini ambao jamii inawatazama kama watu wenye maadili, leo wana vituko vya kila aina. Wao ndio wauzaji wa madawa, wao ndo wezi, wabakaji, walawiti na la maana sana wanaleta migogoro ya kisiasa na kidini. Huko nako hakuna tumaini.
Tafakari familia zetu, huko ndio mwanzo wa haya yote. Iko wapi heshima ya familia, wapi upendo, wapi ushirikiano, wapi uzalendo?
Nyumbani kumejaa ubinafsi, ugomvi, maovu na vituko vya kila aina.
Kila mleta mabadiliko iwe ya kisiasa, ya kiuchumi, ya kisayansi alikuwa na strong will from his or her education, family or religion. Walilewa hawa kwenye hiyo hali na baadaye mfumo ukawasaidia wao kutimiza ndoto zao.
Now we have collapsed system na collapsed basis of will power, watoke wapi wakutukomboa. Hata wakiwa na good morals, system will fail them.
Hapa msemo wa jiokoe nafsi yako mwenyewe unatumika. Unaweza ukawagusa wachache wengine lakini changamoto kubwa ipo katika kuyatekeleza mawazo hayo. It needs more than personal sacrifice


Double R,
Sehemu kubwa nakubaliana na wewe, Lakini ninataka niongezee kidogo penye Red hapo juu.
pamoja na hoja yangu kuwa lazima tuanzie na mabadiliko ktk mfumo na maudhui ya elimu vile vile nakubaliana na wewe kuwa mabadiliko hayo ya elimu lazima yaongozwe na viongozi makini. Hata hivyo, viongozi makini kukosa watu wa kuwasaidia kwa kuwa wote wameoza, mimi ninawaza tofauti. Kwa kawaida Watu walioko chini ya kiongozi hawapaswi kumbadilisha kiongozi aliyeko juu yao ( Rais) kama ni kiongozi mzuri. Badala yake, wale walioko chini ya kiongozi ndo wanapaswa kubadilika ili wafanane na Kiogozi aliyeko juu yao. Kwa hiyo, nchi kama ya kwetu ikipata kiongozi mwenye maono kama haya tunayoyajadili hapa, anaweza akawafanya wafuasi wake wamfuate. Nchini Rwanda Paul Kagame pamoja na madhaifu yake yote, alipopiga marufuku rushwa leo hii hakuna rushwa. Uchumi wa nchi yake unakwenda, moyo wa uzalendo wa wana Rwanda uko juu kuliko nchi nyingine yo yote ktk afrika ya Mashariki.

Nakubaliana na wewe pia kwamba, wasomi wa vyuo vikuu kuwa wapiga debe na washabiki wa sera wasizoziamini badala ya kuwa chachu ya maendeleo ni tatizo lilijijenga ktk mfumo wa elimu. Hatufundishwi kujiamini mashuleni. Mtu anahitimu chuo kikuu hawezi hata kujieleza mbele ya watu 20, anaona aibu. Je, mtu wa namna hii atawezaje kusimamia mawazo yake. Sitaki kuleta siasa ktk jambo hili, lakini nadhani vijana wengi wanaoshabikia ccm siyo kwa sababu hawaoni tatiza la ccm, wengi wao hawana uwezo wa kujenga hoja na kusimamia yale wanayoamini. Pili, hawana ujasiri. Hii ni kwa sababu kujiunga na vyama vya upinzani inahitaji kujiamini na kuwa tayari kwa lo lote.

Tatu, hili la Rais anayesimamia haki kuuawa na wazungu inawezekana, lakini haliwezi kufanyika bila kuwashirikisha watanzania kuwasaidi wazungu hao. Hivyo, nchi isipokuwa na viongozi wanafiki, wafitini na wasiohongeka wa kushirikiana na wazungu hao, bado Rais huyo pamoja na kuathiri maslahi ya wazungu anaweza asiuawe na wazungu hata wakitaka. Wamerekani hawakumpenda Hugo Shavez na Fidel Castro miaka nenda rudi lakini mpaka leo ni wazima.

Kwa hiyo, kwa kuhitimisha, nchi yetu inahitaji mabadiliko, bila kujali tunaanza na elimu au la, mabidiliko hayo lazima yaongozwe na kiongozi mkuu wa nchi aliye makini. tiger Countries kama korea kusini ambazo walikuwa sawa na sisi miaka ya 60 zilibadiliswa na viogozi wao. Siyo kwa kauli mbiu tupu kama ya ari, nguvu na kasi mpya bila vitendo, bali kwa kauli mbiu nzuri zilizofanyiwa kazi kwa vitendo na wakafanikiwa. Na sisi tunaweza kufanikiwa tukipata viongozi wazuri.
 
Hapa nadhani Tunahitaji Azimio jipya la kitaifa, Azimio la kubadili mfumo wa kisiasa, kuchochea uwajibikaji,kujenda Uzalendo na litekelezwe kwa Vitendo!Lakini ili hilo Azimio lifanye kazi lazima uongozi na mifumo mingine yoote iwe elimu, kilimo,usalama n.k ifumuliwe na ijengwe upya.Japo sisi tulio wakubwa twaweza kufa wakati mabadiliko hayajaleta matunda but angalau kizazi kijacho kitatambua harakati zetu na hopefully kuziendeleza. But we need significant Changes katika sera zetu, uongozi wetu , mioyo yetu ,fikra zetu....Everything!
 
Hongera kwa makala nzuri. Kwa historia ndogo ninayofahamu, sisi weusi tulikuwa mbele kimaendeleo dhidi ya mataifa ya weupe kabla ya Biashara ya pembe tatu ya antlatika(Trans Atlantic Slave/Triangular Trade) tangu biashara hii ilipoanza tumerudi nyuma sana kimaendeleo kulinganisha na nchi nyingine, kwa sababu tumeshindwa kubadilika kulingana na sayansi na teknolojia.

Hii biashara ya atlantiki ilianza muda ambao kulikuwa na vuguvugu la mapinduzi ya kiviwanda huko ulaya lakini sisi hatukubadilika tukabaki na teknolojia ileile ya kizamani hivyo pindi ilipoharibiwa na wazungu tukabaki hatuna chetu.

Pia naona Hali ya tabia nchi ya Afrika imetufanya tukkose changamoto mbalimbali za kimaisha ambazo watu wa ulaya walizipata hivyo ikabidi kupambana nazo waweze kustahimili maisha yao.

Kwa upande mwingine bado tunasumbuliwa na unafiki, uroho, upumbavu, ujinga, uoga na kutopenda kufikiri kwa kina. Nadhani mpaka hapo tutakapoadibishwa kutokana na tabia zetu ndipo tutabadilika

Hii Historia ya kwamba waafrika tulikuwa na maendeleo kuliko waarabu na wazungu inalazimika
tutafute credibility yake, nadhani ni historia ya uongo sana hii. Nina wasi wasi mkubwa sana historia
imepindishwa kwa makusudi sana ili kutupumbaza au kwa msingi ambao sijauelewa mpaka sasa.

Sababu ni kama vile inamaanisha kwamba baada ya wakoroni kuingia Africa walizibadilisha akili
za waafrica wa bara lote hili zikaanza kufikiria kwa kuridi nyuma. Aje mtu hapa aniaonyeshe
masalia yoyote yale ya ufahamu wa Muafrika kabla ya wakoroni kuja hapa alafu tuanzie hapo.
 
Hii Historia ya kwamba waafrika tulikuwa na maendeleo kuliko waarabu na wazungu inalazimika
tutafute credibility yake, nadhani ni historia ya uongo sana hii. Nina wasi wasi mkubwa sana historia
imepindishwa kwa makusudi sana ili kutupumbaza au kwa msingi ambao sijauelewa mpaka sasa.

Sababu ni kama vile inamaanisha kwamba baada ya wakoroni kuingia Africa walizibadilisha akili
za waafrica wa bara lote hili zikaanza kufikiria kwa kuridi nyuma. Aje mtu hapa aniaonyeshe
masalia yoyote yale ya ufahamu wa Muafrika kabla ya wakoroni kuja hapa alafu tuanzie hapo.
mkuu fuatilia hii link https://www.jamiiforums.com/interna...can-history-minus-the-eurocentric-filter.html
 
Hii Historia ya kwamba waafrika tulikuwa na maendeleo kuliko waarabu na wazungu inalazimika
tutafute credibility yake, nadhani ni historia ya uongo sana hii. Nina wasi wasi mkubwa sana historia
imepindishwa kwa makusudi sana ili kutupumbaza au kwa msingi ambao sijauelewa mpaka sasa.

Sababu ni kama vile inamaanisha kwamba baada ya wakoroni kuingia Africa walizibadilisha akili
za waafrica wa bara lote hili zikaanza kufikiria kwa kuridi nyuma.
Aje mtu hapa aniaonyeshe
masalia yoyote yale ya ufahamu wa Muafrika kabla ya wakoroni kuja hapa alafu tuanzie hapo.
Tazama miji kama Sofala na Kilwa, na fuatilia historia yake utapata majawabu. Pia usikomee hapo kiongozi fuatilia historia ya maKabaka wa Baganda tawala zao zilikuwaje. (Tatizo kubwa la Waafrika wa leo ni kukata tamaa na uongozi usiowajibika) sihitaji kukuambia ufuatilie Historia za Mali na Misri.
 

Nimepasoma, lakini na yenyewe ni muendelezo wa upotoshoshaji ule ule. Sababu sijaona ni wapi inaelezea
nini kilitokea mpaka vizazi hivyo vikashindwa kuturithisha ufahamu wao uliotukuka.

Haya mambo yanavyoelezewa ni sawa sawa kabisa na kusema kwamba, hata baada ya mtoto kukulia
nyumbani na kufundishwa na hatimae yeye mwenye kupractice uchungaji na ufugaji wa ngomb'e kwa
muda mrefu tu lakini bado uwezekano wa mtu huyu kusahau kabisa kabisa uchungaji na ufugaji wa
ng'ombe au hata kusahau jina la mnyama huyo.

Yaani ni sawa sawa na kulazimisha kwamba inawezekana kabisa na wala sio jambo la kustaajabu kwamba
hata mimi ghafla tu leo naweza nikashindwa kurudi nyumbani, nikapasahau kabisa na nikaanza kutanga tanga
mitaani kama hayawani.

Ninahoji ukweli wa hizi historia kwa machungu sana, wale wanaoandika historia hizi ndio wale wale walioandika
mambo ambayo yaliingizwa kwenye mtaala wa mtoto wa kitanzania akiwa bado mdogo kabisa, darasa la tatu,
kwamba hapo Mwanzo binaadamu alikuwa Sokwe, tena naanza kusahau nadhani!!! sijui wanasema binaadamu alikuwa
sokwe au Muafrica ndio alikuwa sokwe?
 
Nimepasoma, lakini na yenyewe ni muendelezo wa upotoshoshaji ule ule...........................


Ninahoji ukweli wa hizi historia kwa machungu sana, wale wanaoandika historia hizi ndio wale wale walioandika
mambo ambayo yaliingizwa kwenye mtaala wa mtoto wa kitanzania akiwa bado mdogo kabisa, darasa la tatu,
kwamba hapo Mwanzo binaadamu alikuwa Sokwe, tena naanza kusahau nadhani!!! sijui wanasema binaadamu alikuwa
sokwe au Muafrica ndio alikuwa sokwe?

Kama umesoma mtaala ambapo somo la historia linafundushwa darasa la tatu naanza kupata shaka na umri na elimu yako. Umezungumzia upotoshaji wa historia, kumbuka historia sio kitu cha kubuni, bali hupatikana kutoka katika vyanzo mbalimbali ambavyo vinaweza kuthibitishwa kitafiti. Nenda kasome kitabu cha Historia kinachotumika kidato cha kwanza na cha pili sura ya kwanza.
 
Kama umesoma mtaala ambapo somo la historia linafundushwa darasa la tatu naanza kupata shaka na umri na elimu yako. Umezungumzia upotoshaji wa historia, kumbuka historia sio kitu cha kubuni, bali hupatikana kutoka katika vyanzo mbalimbali ambavyo vinaweza kuthibitishwa kitafiti. Nenda kasome kitabu cha Historia kinachotumika kidato cha kwanza na cha pili sura ya kwanza.

Wasiwasi niwe nao kwako ambaye mpaka leo bado uko tayari kuamini kila kitu unachoambiwa au unachosoma,
Hata hivyo vitabu unavyonielekeza kwenda kuvisoma bado vinakilema kile kile, ni bora badala ya kunielekeza vitabu
vya kusoma, wewe ujustify hapa kwamba ni kweli, huko zamani Waafrica walikuwa very bright na sasa wamekuwa
vichwa maji kabisa, ukiweza kutumia scientific proofs sawa, ukiweza kutumia nguvu za giza sawa.

Namna Mwenyezi Mungu ameziumba Bongo zetu (Binaadamu) ni progressively, Binaadamu anaendelea jinsi muda
unavyokwenda, anakuwa na ufahamu wa mambo mengi zaidi, hata juu yake mwenyewe, yes, Binaadamu bado hatujafikia
hatua ya kujifahamu asilimia mia moja,anayafahamu mazingira yake vizuri zaidi, na kama leo wote tungekuwa tunaongea
lugha moja, bila shaka tungekuwa mbali sana kimaendeleo.

Wamekuja hapa wazungu wamechukua babu zetu na kuwapeleka kwao kuwa watumwa, historia haisemi kwamba waliwapeleka
huko ili hao mababu zetu wakawafundishe tamaduni bora na ufahamu wa kiafrica ambao wazungu walizitolea denda.

Historia inasema wakati wazungu walikuwa tayari wanatumia siraha za moto, mababu zetu walikuwa wanatumia maji maji sijui,
alafu mnakaa kwenye computer na kuandika kwamba africa was developed than the rest of the world zamani nyingi sana.

Hii inashangaza sana kama vile Tundu Lisu anavyoshangazwa na taifa kubwa kama Tanganyika, Kuongozwa na kataifa kadogo
kama Zanzibar.

Nataka aje mtu hapa aniambie what happened? Mutation ya namna gani ilitokea kwetu?
 
Ntulutumbi nimekupata,
Nakubaliana na wewe kuwa kila sehemu imeoza, serikali na sekta binafsi kote kunanuka rushwa na kuna kila aina ya matatizo. Kauli ya mbiu ya tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele ni aibu ya miaka 50.
Hoja yangu ni kuwa, kwa kuwa mahakama ni matatizo matupu, serikalini ( Ikulu, CAG, Takukuru, polisi nk) ni matatizo matupu, Bunge ndo usanii mtupu, tunahitaji kuanza mahali ktk kubadili au kubatiza ( as you said) nchi yetu. Hatuwezi kutangaza kwamba kuanzia tarehe 10/12/2011(mwaka wa 51 wa uhuru wetu) nchi yetu imebadilika. Hilo haliwezekani. Kwa kuwa mabadiliko (mabatizo ) haya tunayozungumzia siyo tukio la siku moja, ni mchakato wa zaidi ya miaka 5.
Kwa hiyo basi, kwa mapendekezo yangu, tunahitaji kuanza kwenye elimu. Hii ni kwa sababu elimu inafundishwa kwa watoto kuanzia miaka 3 au 5 chekechea hadi 21/25 - chuo kikuu ambao hawajachafuliwa nafsi zao kifisadi. Tukiwa na silabasi nzuri, siyo hii ya sasa ( silabasi inayozungumzia uzalendo, ubaya wa Rushwa, ubaya wa Uvivu, faida ya ufahamu mzuri wa ujasiriamali kukabiliana na umaskini), watoto ambao ni matunda ya mfumo huu mpya wa elimu, watakataa Rushwa, watakuwa wazalendo wakiwa mahakamani, serikalini, na Bungeni watatenda haki. Mashujaa wa kutaja orodha ya mafisadi bila woga kama Dr Slaa wataongezeka. Huu ndio utakuwa mwanzo mpya.
Hata hivyo, Serikali itakayosimamia mchakato huu wa kubadili nchi yetu lazima itangaze tarehe ya kuanza mchakato huo kama Nyerere alivyotangaza azimio la Arusha. Ijulikane tarehe x ( mf 10/12/2011) ni mwanzo wa kubadili nchi yetu kimfumo na kimaaadili japokuwa hatuwezi kusema itachukua muda gani. Vyombo vya habari vitangaze.
Pili, Lazima tukubaliane kuhusu mafisadi na wabadhirifu kabla hatujaanza mchakato huo. Kuna namna mbili. Kwanza ni kuwasamehe wote waliohusika kabla ya tarehe ya kubatiza nchi yetu ila warejeshe fedha zote walizoiba (Reconciliation).
Pili, ni kusema kwamba, wote waliofisadi nchi yetu huko nyuma tutawawajibisha kisheria kwa kuwapeleka ktk mahakama maalumu ya kubadili nchi yetu - ugumu wa hili la pili ni kuwa hakuna mbunge, mahakimu au viongozi wa serikali yetu watakaopona - kama wapo ni wachache sana. Majaji watakaosimamia mahakama hii ni wale wastaafu au walioopo wasiotiliwa shaka na majaji wenzao ktk utoaji wa hukumu - majaji wa namna hii wapo.
Tatu, hili litafanyika baada ya kupatikana kwa katiba mpya itakayokuwa imeondoa madhaifu yote yaliyojaa ktk katiba ya sasa inayompa rais madaraka makubwa sana - Rais mfalme. Na Rais atakayeongoza mabadiliko mabadiliko haya hawezi kuwa kikwete lazima awe mwingine ambaye hajahusishwa na kashfa ya aina yoyote - Rais mwenye Moral authority.
Thx

Najua wewe ni Mwanachama wa CHADEMA, Je, haya ni maoni binafsi au pia iko kwenye mikakati ya Chama, kwamba
kitakapopata ridhaa ya wananchi kuongoza serikali yetu kutakuwa na cut of date ya namna hii unayoelezea?

Alafu, hilo neno kubatiza ulivyolitumia ni katika misingi ya kubeba maana yake kweli kweli au vipi?
 
Nionavyo mie
Kwenye science kuna mambo ya mabadiliko yanayotokea na kuitwa 'reversible or irrevesible change'. Nadhani hili linahusika hata katika reality life, kama mtu akiharibikiwa ubongo ni lazima atakufa 'revesible death.
Sioni mahali ambapo kama taifa au jamii tunaweza tukaanzia na tukabadili historia kwa sasa, tuko kwenye irrevesible state.
Mfumo wa jamii hauwezi kusaidia watoto kujenga fikra tofauti na tulizonazo sasa. Watoto hujifunza zaidi kwa kuona vile vinavyofanyika na wazazi wao. Watoto wako wanaona nini sasa? Walimu wao wakoje? Wewe ukoje? Majirani wakoje? Mpaka hapo kutegemea kizazi kijacho ni vigumu.
Ukitafakari uongozi na penyewe unaona kuna changamoto kubwa. Sawa tutajitahidi tumweke kiongozi mzuri. Lakini watendaji ni wa aina gani? Ni wale wale walio na sura ya rushwa, uvivu, wasiokuwa na mawazo mapya. Anyway, anaweza akawatoa hao watendaji, wengine walio kama yeye atawatoa wapi?
Akifanikiwa hilo juu, je wazungu ambao mpaka sasa wana nguvu na wanatunyonya watakubali kuona soko lao linaharibiwa? Sasa si wazungu peke yao hata bara la asia ambao wanatuibia, je watakubali? Watamuua tu.
Tafakari wanafunzi wa vyuo vikuu ambao jamii inawatazama kama wasomi na sehemu ya mabadiliko ya mfumo wetu hakuna jipya zaidi ya ubinafsi na wangine kuishia kuwa vibaraka wa viongozi wa vyama na ushabiki usiokuwa na mantiki. Hata mahali walipo na kwa nafasi zao wameshindwa kuwa na faida kwa jamii inayowazunguka, tuwategemee wakianza kazi? (personal benefit)
Tafakari viongozi wa dini ambao jamii inawatazama kama watu wenye maadili, leo wana vituko vya kila aina. Wao ndio wauzaji wa madawa, wao ndo wezi, wabakaji, walawiti na la maana sana wanaleta migogoro ya kisiasa na kidini. Huko nako hakuna tumaini.
Tafakari familia zetu, huko ndio mwanzo wa haya yote. Iko wapi heshima ya familia, wapi upendo, wapi ushirikiano, wapi uzalendo?
Nyumbani kumejaa ubinafsi, ugomvi, maovu na vituko vya kila aina.
Kila mleta mabadiliko iwe ya kisiasa, ya kiuchumi, ya kisayansi alikuwa na strong will from his or her education, family or religion. Walilewa hawa kwenye hiyo hali na baadaye mfumo ukawasaidia wao kutimiza ndoto zao.
Now we have collapsed system na collapsed basis of will power, watoke wapi wakutukomboa. Hata wakiwa na good morals, system will fail them.
Hapa msemo wa jiokoe nafsi yako mwenyewe unatumika. Unaweza ukawagusa wachache wengine lakini changamoto kubwa ipo katika kuyatekeleza mawazo hayo. It needs more than personal sacrifice

Ndio Maana tunatakiwa kuomba Ufalme wa Mbinguni uje hapa Duniani.
 
Ndio Maana tunatakiwa kuomba Ufalme wa Mbinguni uje hapa Duniani.

Ufalme wa Mwenyezi Mungu uko Mbinguni, Duniani ni nafasi ya wanadamu kuweka Mambo sawa uko Mungu akitoa Ulinzi kutokea Mbinguni. Huwezi kukaa na 'kusubiri' Mungu aje akuletee Demokrasia, au aje akuondolee rushwa na Ufisadi, wadhani Nchi zilizo na Machafuko Hakuna Mungu? Acha kuconfuse nafasi ya Mungu na Nafasi ya mwanadamu!N a Usimjaribu Mungu wako.
 
Ufalme wa Mwenyezi Mungu uko Mbinguni, Duniani ni nafasi ya wanadamu kuweka Mambo sawa uko Mungu akitoa Ulinzi kutokea Mbinguni. Huwezi kukaa na 'kusubiri' Mungu aje akuletee Demokrasia, au aje akuondolee rushwa na Ufisadi, wadhani Nchi zilizo na Machafuko Hakuna Mungu? Acha kuconfuse nafasi ya Mungu na Nafasi ya mwanadamu!N a Usimjaribu Mungu wako.

Mimi utanionea Bure, Mambo ya kuomba Ufalme wa Mbinguni uje duniani sio yangu, na mimi
nimesoma kwenye Biblia tena aliyetoa maelekezo ya kuomba ufalme huo uje hapa duniani ni
Yesu Mwenyewe ambaye ameandikwa kwamba ndiye atakayekuwa kiongozi wa ufalme huo
hapa duniani.

Kwa hiyo kama kwenye kauli yangu kuna chembe ya kuconfuse nafasi ya Mungu na Mwanadamu,
ama kumjaribu Mungu wangu, anayestahili kulaumiwa ni Yesu Mwenyewe wala sio mimi.

Na nikukumbushe leo kama sio kukufunza kwamba Democrasia sio Mpango wa Mungu, Democrasia
ni Mpango na harakati kinyume na taratibu za Mungu. Tafakali!!!!
 
Mimi utanionea Bure, Mambo ya kuomba Ufalme wa Mbinguni uje duniani sio yangu, na mimi
nimesoma kwenye Biblia tena aliyetoa maelekezo ya kuomba ufalme huo uje hapa duniani ni
Yesu Mwenyewe ambaye ameandikwa kwamba ndiye atakayekuwa kiongozi wa ufalme huo
hapa duniani.

Kwa hiyo kama kwenye kauli yangu kuna chembe ya kuconfuse nafasi ya Mungu na Mwanadamu,
ama kumjaribu Mungu wangu, anayestahili kulaumiwa ni Yesu Mwenyewe wala sio mimi.

Na nikukumbushe leo kama sio kukufunza kwamba Democrasia sio Mpango wa Mungu, Democrasia
ni Mpango na harakati kinyume na taratibu za Mungu. Tafakali!!!!

Nakubaliana na wewe but do you think kama mtu ameingia Madarakani kwa kuiba kura, i mean ni MWIZI hapo kuna Ufalme wa Mungu? Wa kusubiri ufalme uje kumbadili mwizi (Japo hukumu ni siku ya mwisho katika maisha mengine kabisa) basi endeleeni Kusubiri..Wakati sisi tunaoamini Twaweza kubadili Mambo tuendelee na harakati wkt huyu Mungu akitupa Ulinzi wa Kutokamatwa kamatwa na Polisi!
 
Nakubaliana na wewe but do you think kama mtu ameingia Madarakani kwa kuiba kura, i mean ni MWIZI hapo kuna Ufalme wa Mungu? Wa kusubiri ufalme uje kumbadili mwizi (Japo hukumu ni siku ya mwisho katika maisha mengine kabisa) basi endeleeni Kusubiri..Wakati sisi tunaoamini Twaweza kubadili Mambo tuendelee na harakati wkt huyu Mungu akitupa Ulinzi wa Kutokamatwa kamatwa na Polisi!

Mtulumbi, nakubaliana na wewe kwamba Utawala wa democrasia wa kweli kabisa kabisa ni solution ya matatizo yetu, lakini
naomba kuweka wazi kwamba solution hiyo ni kwa ajili ya kupunguza speed ya matatizo kutujia mapema, lakini sio solution
ya matatizo yetu yote kama tunavyotegemea, Kuna mtu kaweka comment ya msingi sana kwenye thread hii, akimaanisha
kwamba kwa hapa tulipofikia hakuna namna tunaweza kupata njia sahihi kama taifa ya kutufikisha kwenye point yoyote ile
ya heri.

Ukiangalia kila kitu kinachoendelea duniani kinatusukuma kwenye destruction kila kukicha, Hata hiyo tunayoita democrasia,
sidhani kama is something we need, tunataka, lakini ni wapi duniani democrasia imewapa amani ya milele, tunataka kuwa na
uhakika wa chakula, wapi duniani democrasia imewapa chakula cha uhakika, elimu, wapi democrasia imepeleka amani kwa
watu wote.

Mungu yuko wapi kusupport democrasis iuokoe Ulimwengu, By the way nashindwa kuelewa tunapoanza kutoa kauli za
kumshirikisha Mungu kwenye issues ambazo hajawahi kupromise kutusupport, Kwenye Biblia hakuna sehemu nimepata
kuona neno democrasia
 
Back
Top Bottom