Kwani mngegomea, mngepungukiwa na nini?

Kwani mngegomea, mngepungukiwa na nini?

Ndio na hao viongozi sio lazima wawe viongozi/wagombea wa upinzani.

Hapa hadi maisha yatupige vizuri ndio tutaelewa.Leo viongozi waupinzani wakigoma watu watapiga kura kama kawaida.
Haya.
 
Hapana!

Hakuna kilicho kipya!

Mazingira ya uchaguzi wa 2020 ndo yale yale ya 2015, 2010, 2005!

Tatizo ni usahaulifu wenu tu.
Kama ndio hivyo basi wapinzani wajitathimi upya, sio kwa sababu ya tume kutokuwa huru bali kwa anguko kubwa la kukataliwa na wapiga kura.
 
Haondoki huyu. Katiba inakwenda badilishwa. Kisingizio ni ili amalizie miradi yake.

Na pia atawaambia vibaraka wake kuwa usalama wake uko hatarini, so ni vyema aendelee kupata kinga ya uRais ili asidhuriwe.. Hatoki huyu madarakani ng’o. Na ikifika hapo, wote wanaomshabikia sasa ni bora waufyate, kila mtu aenjoy show.
 
Kweli kabisa, lakini sometimes we have to learn in hard way. Mashabiki maandazi labda watapungua turudi kujadili mustakabali wa Taifa letu bila mihemuko.

Upinzani hadi sasa wanashindwa kusimamisha wagombea majimbo yote, hili nani alaumiwe? Just a simple case, lazima tufahamu haitokuja siku CCM watawapa fair platform.

Kelele za JF na Tweeter huwadanganya sana kama vile zitageuka kura. Baada ya uchaguzi huu, kama wataingia tena awamu ijayo na mguu ule ule kama walivyopuuza maoni yetu baada ya zile blunders za 2015 watakula kisago kile kile.

Sasa ndugu unaamini kuwa kura hazikupigwa? Hujashuhudia wizi wa kura wa kutisha?? Mbona hao unaowakejeli wamepiga kura sana tu. Tatizo hulioni?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kwani kura za mbunge lazima ziwe sawa na kura za Rais?

Naweza kuwa mwana ACT, kura ya ubunge nikampigia mgombea wa CHADEMA, ya urais nikampa wa CCM.

Nyie watu mmechanganyikiwa!
Acha kutetea. Ukienda kupiga kura unapewa karatasi zote. Unless usipige huko basi zingehesabika zimeharibika. Haihitaji elimu kujua huo mchezo hapo.
 
Acha kutetea. Ukienda kupiga kura unapewa karatasi zote. Unless usipige huko basi zingehesabika zimeharibika. Haihitaji elimu kujua huo mchezo hapo.
Sasa hoja yako hapa ni nini?

Kwani ukipewa karatasi zote unalazimishwa kuzitumia zote?

Huna akili kabisa wewe!
 
Swali kwa wapinzani.

Kwani mngegomea kushiriki haya maigizo ya uchaguzi wa 2020, mngepungukiwa na nini?

Na hivi mlivyoshiriki, mme-gain nini?

Mimi msimamo wangu uko wazi. Unajulikana.

Hakuna kushiriki chaguzi za maigizo ambazo mtu hauhitaji hata uwe genius kujua matokeo yake yatakuwaje.

Kushiriki chaguzi za hivyo, chaguzi za kutimiza wajibu tu, ni umajinuni.

Baadhi yenu mmetaja chaguzi za serikali za mitaa mwaka jana ambapo wapinzani walizisusia.

Kwanza, chaguzi za serikali za mitaa si sawa na uchaguzi mkuu.

Pili, migomo ya kushiriki chaguzi za maigizo ni lazima iwe endelevu.

Kama mwaka jana mligoma na CCM wakajipa ushindi wote, mwaka huu mmeshiriki na mmeambulia nini zaidi ya kipigo cha mbwa?

Zigomeeni hizo chaguzi. Wekeni mashinikizo mpaka zipatikane taasisi zilizo huru za kusimamia na kuendesha chaguzi.

La sivyo, mtaendelea kutegemea hisani ya CCM kupata ushindi.

Na siku mkikutana na jitu lenye roho mbaya, hata hizo nafasi chache mnazoshindaga, mtanyimwa.

Na jinsi mlivyo na vichwa vigumu, si ajabu mkaanza ule upuuzi wenu wa twende na Shangazi 2025.

Bure kabisa.
Je watakubaliana wapinzani wa vyama vyote ?

Je ikiwa hawatokubaliana wapinzani wa vuama vyote alafu ikawa vyama viwili vya upinzani vimegoma na vyama vitatu vya upinzani vimekubali je unadhani mgomo huu utasaidia kitu wakati kuna wapinzani tayari wameshakubali ?
 
Je watakubaliana wapinzani wa vyama vyote ?

Je ikiwa hawatokubaliana wapinzani wa vuama vyote alafu ikawa vyama viwili vya upinzani vimegoma na vyama vitatu vya upinzani vimekubali je unadhani mgomo huu utasaidia kitu wakati kuna wapinzani tayari wameshakubali ?
Basi acha waendelee kushiriki...

Who the hell cares?
 
Yaani katika siku zote na mada zako zote hii ndio nimeikubali , Mimi niliandika nyuzi zisizopungua nne humu kupinga upinzani kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana lakini bado hawakujifunza tu .
 
Wewe ndiye utakuwa msahaukifu. Yakiyitokea 2010 na 2015 ni wizi wa kura.

Safari hii kura hazijaibiwa Bali wamejitangazia matokeo kama wanavyotaka.

Kwa hiyo raisi ni nani? Una akili wewe?
 
Basi acha waendelee kushiriki...

Who the hell cares?
Me naona wakigoma alafu wengine wanafanya ni kazi bure tu.

Kuwepo kwa vyama vingi vya upinzani hiyo ni kuunda upinzani ndani ya upinzani,jambo ambalo linazidi kudhoofisha upinzani tu.
 
Yaani katika siku zote na mada zako zote hii ndio nimeikubali , Mimi niliandika nyuzi zisizopungua nne humu kupinga upinzani kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana lakini bado hawakujifunza tu .
Duh!

Yaani baada ya miaka 14 hapa JF na mabandiko zaidi ya 80K, ni mada yangu moja tu ndo umeikubali?

Ina maana huwa naandika pumba nyingi sana? 🤣🤣

Anywho, utani pembeni, hili suala nimeanza kulizungumzia kwa muda mrefu sana.

Bahati mbaya wahusika wenyewe ni watu wenye vichwa vigumu sana.

Waache tu waendelee kujipotezea muda, la, watakuwa ni wamendea ruzuku na si watu wa kusimamia kanuni.
 
Me naona wakigoma alafu wengine wanafanya ni kazi bure tu.

Kuwepo kwa vyama vingi vya upinzani hiyo ni kuunda upinzani ndani ya upinzani,jambo ambalo linazidi kudhoofisha upinzani tu.
Sawa.

Wafanye wanavyotaka basi.

Mimi kamwe sitojihangaisha na kupiga kura chini ya haya mazingira. Kamwe daima!

Nyie anzeni kujipanga kwa ajili ya 2025 🤣🤣.
 
Wapinzani Kuna wakati tunakwamishwa na viongozi wetu,dalili zote toka uchaguzi wa Serikali za Mitaa zilikuwa zinaonyesha bila katiba mpya bila tume huru ya uchaguzi Basi hakuna uchaguzi huru na wa haki ungefanyika.Sasa Kwanini viongozi walijitoa uchaguzi serikali za Mitaa lkn uchaguzi mkuu hawakujitoa?Viongozi wetu Ni wabinafsi.
 
Kwani kuna nini jipya ambalo lilikuwa halijulikani?

Tatizo lenu nyie ni we peso was kusahau!

2010 Slaa alilalamika kuibiwa kura.

2015 Lowassa naye hivyo hivyo.

Mlivyo wepesi kusahau, ikifika 2025 mtakuwa mshasahau haya ya 2020, mtaingia kwenye uchaguzi na mtaishia kupigwa tena na mtalia kama mliavyo hivi sasa!
Japo unatumia maneno makali lkn Kuna ukweli ndani yake.Viongozi wetu Ni wabinafsi. Uchaguzi wa mwaka huu umekuja na Neema ndani yake, nadhani Sasa hivi watapigania kile walichotakiwa kupigania Sasa. Haiwezekani kushiriki uchaguzi utakaoshindwa,Ila unashiriki tu kwa vile unahisi unaweza pitishwa. Sasa hivi wote wamekatwa nadhani SoMo litaeleweka
 
Wewe ndiye utakuwa msahaukifu. Yakiyitokea 2010 na 2015 ni wizi wa kura.

Safari hii kura hazijaibiwa Bali wamejitangazia matokeo kama wanavyotaka.
Dalili zilionekana toka serikali za Mitaa pia kwenye uchukuaji fomu.Kwanini hawakujitoa?
 
Back
Top Bottom