Kwanini Abiria wengi wa Mabasi ya Mikoani wakifika maeneo ya Mto Wami na Milima ya Kitonga Nyuso zao huwa ni za Huruma sana?

Kwanini Abiria wengi wa Mabasi ya Mikoani wakifika maeneo ya Mto Wami na Milima ya Kitonga Nyuso zao huwa ni za Huruma sana?

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Na kama haitoshi kuna Abiria wengine mkiwa mnayakaribia tu hayo Maeneo tajwa Mawili Maandiko ya Vitabu vya Dini vya Biblia Takatifu na Quran Tukufu huwa wanayakumbuka na pia wanajua mno Kuyadadavua kwa mapana yake.

Na kinachonishangaza sana mkiyapita tu hayo Maeneo utaona Abiria wote ndani ya Mabasi Nyuso zao zinaanza kurejea katika Ujeuri ule wa Mwanadamu halisi.
 
Wami kuna lori lilipiga mbizi pale juzi mamba wakafanya yao.

Pale kwa dereva mzoefu wa njia hakuna changamoto sana. Kikubwa ni ku-control speed. Na miguu ya gari iwe vizuri.
 
ndio hivyo.
Hakuna changamoto kubwa wami.
Maybe kidogo Kitonga.

Tema Mate chini Ndugu kwani unaonekana hupajui Mto Wami na kama ni kupajua Kwako basi ni hii hii Miaka ya hivi karibuni tu. Hapo ni balaa!!!!!!
 
Inategemea na saikolojia ya mtu.

Kuna wengine wanapofika katika hali ama sehemu hatarishi ndiyo "ujeuri" huongezeka mara dufu.
 
Back
Top Bottom