Kwanini ajali nyingi zinazotokea mataa Mbezi Beach huwa zinaua tu Vijana walioanza kufanikiwa kimaisha na kiutajiri?

Mshana Jr pandisha ule uzi wako wa 2014 wa Jems mtoto wa Dando.

The same area more and more wasanii na vijana wengi wameishia pale.

Ni eneo korofi, au halipendi pombe au pana yao waliyoweka

James alivuta pale Makumbusho maeneo ilipo TISS/Merry Water...
 
Njia panda za kutoka kwenye starehe zina masheitwaNi watoa roho, likewise penye barabara zilizonyooka.
Niwaibie Siri vijana wapenda kula Bata,waache kutumia magarinya AC ziraili mtoa roho anatumiaga AC kuwamaliza kupitia usingizi na kutokujali alama za barabarani....
Ni mara mia mbili kufungua vioo vya gari lako kama uwezi kodi bajaji au tumia trekta.
 
Daaaah mwamba umeua aisee
 
Ushauri mzuri sana

Ova
 
Binafsi mara nyingi miaka ya nyuma nilikuwa nikipita sana hiyo barabara jioni na kurudi usiku wa manane katika kufanikisha issues zangu.

Na issues nyingi zilizokuwa zinanifanya nifike huko zilikuwa zinahusisha matumizi kilaji kwa sehemu kubwa, na muda wangu wa kurudi home ulikuwa ni around saa 6-9 usiku.

Mambo niliyo-notice-

*Barabara ya Bagamoyo watu wengi hawana utaratibu wa kufuata taa na sheria za barabarani hasa usiku.

*Ni aina ya barabara isiyo na vizuizi vingi kama matuta, natural barriers nk. hivyo watu kwenda mwendokasi sana. Binafsi mwendo ulikuwa 80-160 km/hr

*Wengi wanaotembea usiku ni walevi.

*Junction mara nyingi zinasongwa na giza, na hakuna mwanga wa kutosha.

* Kwa aina ya mwendo niliokua napita nao na bado wengine wana-overtake au tuko sambamba ni kiashiria tosha cha uendeshaji hapo. Reckless driving imeshamiri sana.

- Kuna siku nilipark gari nyumbani halafu sikujua hata getini kwangu nimepitaje-pitaje, na hasahasa ile kona kwenye daraja la kimara, nikarudi nje kukagua gari halina alama hata ya mkwaruzo- Nilijiuliza sana maswali mengi nikasema inawezekana huko mabarabarani kuna viumbe wengine wanawasaidia binadamu kuendesha magari.

Baada ya hapo, siwezi kunywa sana beer nikiwa na endesha- 4 Beers Maximum, na nikipita junction usiku nakuwa makini sana sana.

* Siku nikiwa naendesha gari sijanywa huwa nakuwa disappointed sana huko barabarani sababu ya pattern mbovu ya uendeshaji wa madereva wengine. Tanzania mtu inabd uwe defensive kwelikweli, hata ikibd vaa element manake kugongwa ni nje-nje.
 
Hapa naomba niulize,kwani umezungumzia ajali kwa walioanza kuyaona mafanikio,ila hujafafanua ni ajali za aina gani,waendesha Mikoko,wakitembea kwa miguu,ama hujazungumzia mwonekano au giografia ya eneo la ajali hizo,kumbuka sio wote tunafahamu watu hao na mafanikio yao au eneo la ajali
 
Nilitarajia muuliza swali atoe giografia ya eneo tajwa kabla ya kuanza fikra za vichaa wa kitanzania 🥱
 
Nilitarajia muuliza swali atoe giografia ya eneo tajwa kabla ya kuanza fikra za vichaa wa kitanzania 🥱
Kipande kingine watu wanakimbia usiku dar ni kipande cha Sam Nujoma. Hapo weka mbali na watoto - Yan taa zikiwa zinaruhusu kuingia barabara kuu jiulize mara mbili, swala la haki achana nalo kabisa manake mtu unaweza kugeuzwa kitoweo.

* Usiku watu hawaoni vizuri kwa kutumia macho, ila miguu inaona accelerator pedal balaa.
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] Uzuri mie sio kijawa niliefanikiwa siogopi hayo mataa nakuja tu
He he he..Hii Comment yangu hata sijui imefikaje huku....Nimekosea.[emoji1787]

Nilidhani naandika kule kwenye uzi wa Simba..
 
Hasa kwa mtu ya Gilasi🏆
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…