Kwanini Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu hakuvaa sare za Jeshi wakati akiwatunuku kamisheni wanajeshi?

Kwanini Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu hakuvaa sare za Jeshi wakati akiwatunuku kamisheni wanajeshi?

Rais gani mwingine aliwahi kuvaa uniform za jeshi kwenye shughuli kama ile zaidi ya yule aliyekuwa anajifanya mjuaji wa kila kitu kwahiyo mnataka aige kila kilichofanywa na huyo mtu wenu , mkae mkijua mtu wenu alikuwa mshamba na asiyejiamini yaani ni limbukeni.
Ww kapuku una nini cha maana zaidi ya kushinda mitandaoni kuwanga na kalio!!???
unamuita mwenzio mshamba mtu aluyekuwa president.......
duniani kuna maajabu
 
Karibu Marais wote ambao ni maamri Jeshi Wakuu kwa nchi zao huvaa kijeshi ikiwapendeza, sio Africa tuu, hata kwingine.
Marais wote waliopita hawakuwahi kuvaa magwanda kwenye shughuli kama hizo, ina maana hawakuwahi kuwa amiri jeshi mkuu? Kwani magwanda ndio yanakufanya kuwa amiri jeshi mkuu?
 
Uchafu ni lile lililofukiwa, sasa hivi wafuasi wake wamebaki kulia kama mbwa jike linalohitaji mbwa dume lishughulikiwe.
siajabu wazazi wako walishafukiwa au wapo mbioni kufukiwa vile vile.....
swala la kufukiwa kila mtu atalipitia kwa wakati wake...
 
Hapo umeongea mkuu,mwinyi,mkapa ,kanali kikwete Hawa wote walikuwa Amiri mkuu kwa kipindi Cha miaka kumi na hawakuwahi kuonekana na combat hata siku moja,hata Mwalimu JKN ukiachilia kipindi kile Cha Vita ya kagera ambapo occasionally alipiga combat hakuwa anaendekeza kuvaa combat.
Kabisa mkuu
 
Sasa huyu mwendazake kafanya vip??

Kila siku kutuongopea kuwa nchi hii ni tajir na tunajiendesha KWA pesa zetu za ndani kumbe anakopa kopa huko nje,deni la Taifa limeongezeka Mara dufu katika kipind chake kifupi alichokaa mwendazake
Alikuongopea wewe na wenzako wa aina yako.
 
Swala la kutembeza bakuli ni jambo lisiloepukika kwa uchumi wa nchi yetu hata huyo Magufuli aliyekuwa anaongopa kutekeleza miradi mikubwa kwa fedha za ndani ndiye amekopa fedha nyingi katika kipindi kifupi cha utawala wake kuliko rais yeyote aliyepita,mradi pekee uliotumia fedha za ndani kwa 100% ni ununuzi wa ndege tu lakini maeneo mengine kwa sehemu kubwa ama tumekopa ama tumepokea asilimia fulani ya ufadhili sema yeye tofauti yake na wenzake ilikuwa ni kujikweza ndio maana hata serikali ikipeleka fedha sehemu alikuwa akijinadi ni fedha zake yaani kama yeye ndiye alikuwa akiifadhili serikali.
Huoni hata aibu kusema eti kutembeza bakuli ni suala lisiloepukika. JPM hakutembeza bakuli, alikopa, na hivyo ni vitu viwili tofauti. Kwa nchi ilipokuwa imefikia hadi kutegemea msaada ili kufanya uchaguzi mkuu ilikuwa ni kuuza utu wetu.

Mwalimu Nyerere ashawahi kuandika kwamba hata kama tunaweza kupata msaada wa fedha kutoka nchi rafiki lakini sivyo tunavyotaka na haipaswi kuwa hivyo. Kiongozi wa nchi hapaswi kuonyesha attitude ya kujiuza uza eti upate fedha za bure. Ni utoto, ni undazi na hakuna vitu vya bure duniani.
 
Sasa umesikia nimeomba chochote kwake! Najimudu kwa kiasi nilichaajiriwa mimi siwezi mapambano aliyoyafanya yeye(kuuwa watu na kudhulumu haki za wengine) eti ili tu nipate mapesa mengi yatakayokuja kutumiwa hadi ma vitukuu vyangu.
Ukiambiwa utoe ushahidi he killed unao mkuu?na alidhulumu unao? + kazi ya hukumu ni ya Mungu Wewe u msafi?uko msafi kiasi cha kunyooshea wenzako tena wendazao vidole?
 
Leo ukisema fulani anatetea mabeberu na hivyo mtu kama huyo ni msaliti hivyo hastahili kuendelea kuishi halafu hata wiki haiishi kuna mtu anashambuliwa kwa risasi hapo unataka tuwe na ushahidi gani? Au mtu tu anahoji uhalali wa Phd yako halafu siku chache baadaye anapotea mazima unataka watu wamnyooshee kidole nani!
Tupe ushahidi wa watu waliowahi kufanyiwa hivyo na mazingira yake.Maelezo yako hayajitoshelezi.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Kwa nchi yenye demokrasia sio vizuri kwa kiongozi wa nchi kuvaa magwanda ya moja kati ya vyombo vyake vya ulinzi, kwanza haileti picha nzuri na vile vile inatoa taswira kuwa kiongozi huyo anakaupendeleo au amebase zaidi au ana imani zaidi na chombo flani cha ulinzi na vile vile inatoa ujumbe kuwa chombo hicho ni bora kuliko vyombo vingine.
Umeshawahi kujiuliza kwanini hata hao viongozi wanaovaa magwanda kwanini wasivae na magwanda ya vyombo vingine vya ulinzi na usalama?
Kiongozi ambae haijui /haelewi political science ndio atakaevaa magwanda lakini kwa mweledi hawezi vaa.
 
Nilikaa kusubiri juzi nilitarajia Rais Samia atavalia mavazi rasmi ya Kijeshi nilisubiri alipotokeza nikazani ni yule Rais nunda wa Korea ,kumbe ni yeyye,nikajisemea leo ni mambo ya Kijeshi na yeye sasa sikujua anahudhuria ile kama Rais au Amiri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,kwanini hakuvaa magwanda?
Kwani ile kofia na lile joho hukuliona?
 
Back
Top Bottom