Kwanini benki hutoza wateja ada kwa kutoa pesa zao wenyewe?

Kwanini benki hutoza wateja ada kwa kutoa pesa zao wenyewe?

Ogopa sana kuona Biashara ambayo wanakodi jengo kuubwa, wanaajiri watu na elimu zao za juu, wana ajiri kampuni za ulinzi, wanatoa tenda za internet, kuweka ATM mashine ili tu kukutunzia wewe elfu kumi (10,000) yako.
 
Me huwa sielewagi hata kwanini kutoa hela yako mwenyewe kuwe na charges (simu na benki)

Hiyo sasa cha mtoto... kubwa kuliko ni hii ya kukatwa hela unapoangalia salio sijui hata ni nani alianzishaga huu wizi na upumbavu

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Mada ya Mtoa hoja ni fikirishi na inahitaji exposure kidogo kwenye masuala ya monetary na banking system hasa katika nchi zilizopiga hatua kubwa kiuchumi.

Ukizitazama nchi zenye uchumi mzuri kifedha mathalani China kwa mfano, wao huamini benki ndizo zilipaswa kuwalipa wateja wao kwa kutunza fedha kwao (japo sina hakika kama linafanyika hilo) ila jambo nililolithibitisha ni kwamba HAKUNA CHARGES ZOZOTE ANAZOTOZWA MTEJA AFANYAPO MUAMALA WOWOTE WA KIFEDHA. Kwa maana nyingine ni kwamba kuna zero charges katika mifumo yao ya kawaida ya kibenki mathalani ATM n.k na kama ulikuwa na 100k kwenye akaunti yako haijalishi utatazama salio mara ngapi salio lako litabaki kuwa 100k na siku ukienda kutoa unaweza ukitoa 100k yote.

Jambo hilo linawezekana kufanyika hata hapa kwetu ikiwa serikali yetu kupitia kupitia Wizara ya fedha itaamua kuyaelekeza mabenki (kupitia BOT) kuondoa tozo za miamala yote ya kifedha katika benki zao.

Tatizo tulilo nalo sisi Tanzania ni kuwa serikali ndiyo inayoyahimiza mabenki kuweka tozo kama kodi ya serikali katika miamala inayofanyika. Kwa maana nyingine serikali ndiyo inayotubebesha mzigo huu.

AMANI IWE NANYI

Kweli yako mkuu
Naona hili lipo Tz tu na huo ni wizi kama wizi mwingine tu
Mbona Ulaya hawana mambo haya
Naweka hela Bank zinaongezeka ingawa ni % ndogo ila makato hakuna ya kutolea wala ya kuangalia salio wala ya kuweka
Nashangaa sana kwa hili
 
Benki siyo kama parishi ya kanisa inayofanya mambo kwa bila faida. Kwa mfano benki moja niliyokuwa na na account, hata kama hakuna fedha kama hujaifunga utachajiwa fee kila mwezi.

Parishi ya wapi inayofanya mambo yake bila faida?
 
Vishingi vyako laki tano unavyoweka leo asubuhi na kuvichukuwa kwesho jioni ndiyo benki wafanyie biashara ya kukopesha watu? Hivi unadhani gharama za kuendesha benki 7/24, infrastructure zake zote siyo gharama? Anzisha yako au tafuta watu mfanye ushirika muanzishe ya kwenu na muwape wateja huduma kama unavyosema. Bila shaka wateja wengi watahamia kwenu kwani gharama zenu zitakuwa ndogo sana.

Duuh, jamaa umetoa makavuu! [emoji3525][emoji3525]
 
Zile karatasi na uchapishaji siyo bure...

Huduma za kutunza na kuendesha ATM siyo bure...
 
Ni vema umekiri huna ufahamu, basi jifunze kusikiliza wakubwa wakiongea.

🤣 🤣 🤣 🤣 🤣Mtanzania kwa ''utaalam'' tu. Akisoma kidogo nadharia utadhani yeye ndiye mwanzilishi wake. Haya mnayolalamika hapa yote ni upuuzi wa hali ya juu, na yanatokana na kukosa exposure. Mtu kama wewe unaonekana umeenda hivi vyuo vya kata basi umekuwa kama yule kipofu aliyeona mwezi. Kukaa kwangu nje kumenifanya niwe na account kwenye benki mbalimbali. Hizi fees mnazolalamikia haziepukiki kwani ndiyo zinafanya benki ziwepo. Benki siyo kama parishi ya kanisa inayofanya mambo kwa bila faida. Kwa mfano benki moja niliyokuwa na na account, hata kama hakuna fedha kama hujaifunga utachajiwa fee kila mwezi. Vile vile mwenye fedha naye anachajiwa fee kila mwezi.
Mimi nimewaambia hawana hoja wakanishukia Kama mwewe.

Wao wanadhan hizo ATM machine bank inapewa na serikali? Walinzi n.k
 
Bank haifanyii biashara pesa ya mtu bila mkataba unaweka leo keshokutwa umechukua hata usipochukua keshokutwa hawajui utaibeba lini so zile nigharama za kukuhifadhia cash yako hutaki nunua kibubu
 
Umesoma na ukaelewa mada?
Point yangu ni mm bank inakupa namna mbali mbali za ww kuipata hela yako kwa urahis ndio maana kuna Atm, mawakala na njia nyengine so.hzo njia zitafanikiwaje.kama.hakuna pesa?
 
Kuangalia salio wapo right kukata. Kwa mfano una milioni ishirini na nne laki tatu na sabini na saba elfu na mia mbili hamsini, ukisema uhesabie mwenyewe utatumia muda gani? Sasa wewe unakuwa umeipa kazi mashine ikuhesabilie pesa yako kwa muda mfupi kwa TZS 350 TU.
 
Una hoja nzuri sana. Zaidi naongezea gharama za kuangalia salio. Nataka kuangalia kujua kiasi gani cha pesa nilichonacho, sasa kwanini unitoze kuangalia pesa zangu mwenyewe? Huduma za kutuma pesa ni sawa kwasababu mnanisaidia kifikisha pesa kwa mwingine.

Naung mkono hoja,na serikali imefumbia macho swala hilo miaka yote,its doesn’t make sense,pesa ya mtu kaiweka na bank inanufaika nayo ila unakatwa makato ya kuangalia salio lako,,tozo za withdraw pesa,tozo za mwezi du,mabank ya kiafrica balaa sana,mi naishi baraa la europe,nchi niliyopo unakatwa pesa ya insuarance tu,na hapo mnalijadili wakati wa kufungua account ,hakuna makato mengine,hiyo insurance ni kwa manufaaa yako mfano ukifariki au kupata ajali kazini ikakufanya uwe kilema au usiweze kufanya kazi ,unapewa zaidi ya euro 60k zaidi ya milioni 160 za bongo,hapo mnajadili ukatwe kila mwisho
Wa mwezi au kila baada ya miezi 6 na ni hela mbuzi,wao wanathamini wewe kuweka pesa katika bank yao na wao wanaifanyia biashara sio kama bongo umeweka wanakata hadi kuangalia salio aisee
 
Ukitaka kujua ni wizi ambao Benki Kuu imeunyamazia, tembelea nchi nyingine. Nimekaa Ulaya, Asia na America. Na kote nilikuwa na akaunti. Sikuwahi kukatwa pesa kwa kutoa kwenye akaunti yangu! Huu ni wizi tu ila wezi wanatumia kalamu na wamekaa kwenye ofisi nzuri na AC juu.
Habari za leo wakuu,

Leo tujadili hizi tozo za mabenki [withdrawal charges] kwa wateja ambao kimsingi ndio wamiliki wa fedha hizo.

Mteja anatunza pesa yake benki, na benki zinaifanyia biashara [kukopesha] kwa faida. Kisha mmiliki akihitaji kutoa kiasi chochote kwa matumizi yake hutozwa 'ada' kiasi fulani.

Hii imekaaje?

Ni afadhali wangeishia kuchaji zile ada za kuhifadhi tu, kama ni kwa mwezi au vyovyote.

Angalau tungejua ni gharama ya kutunza fedha, lakini hii ya kila unapotoa wanakata ni WIZI tu kama WIZI mwingine.

Kama kuna sababu zenye mashiko hebu tuzijadili hapa.

Nawasilisha.
 
Gharama ya kuangalia salio nao ni wizi mwingine. Hebu fikiria Vodacom, Airtel, Halotel, Tigo... nao wangemua kukata muda wa maongezi kila unapoangalia salio! Benki zenyewe zingelalamika. Na ukitaka kujua ni wizi, kwa nini Japan, Ulaya... hakuna makato ya kuangalia salio? Eti hata ukiangalia kwa ATM, wanakata pesa yako!!
Una hoja nzuri sana. Zaidi naongezea gharama za kuangalia salio. Nataka kuangalia kujua kiasi gani cha pesa nilichonacho, sasa kwanini unitoze kuangalia pesa zangu mwenyewe? Huduma za kutuma pesa ni sawa kwasababu mnanisaidia kifikisha pesa kwa mwingine.
 
Umeona eh? Huu wizi hauko nchi zilizoendelea. Ni wizi wa mchana kweupe na serikali imeufumbia macho.
baraa la europe,nchi niliyopo unakatwa pesa ya insuarance tu,na hapo mnalijadili wakati wa kufungua account ,hakuna makato mengine,hiyo insurance ni kwa manufaaa yako mfano ukifariki au kupata ajali kazini ikakufanya uwe kilema au usiweze kufanya kazi ,unapewa zaidi ya euro 60k zaidi ya milioni 160 za bongo,hapo mnajadili ukatwe kila mwisho
 
Kwa nini Ulaya hawatukati kuangalia salio? Usitetee wizi. Nyie watu wa benki tafuteni njia nyingine ya kupata faidia siyo kuibia watu pesa zao. Acheni unyang'anyi.
Kuangalia salio wapo right kukata. Kwa mfano una milioni ishirini na nne laki tatu na sabini na saba elfu na mia mbili hamsini, ukisema uhesabie mwenyewe utatumia muda gani? Sasa wewe unakuwa umeipa kazi mashine ikuhesabilie pesa yako kwa muda mfupi kwa TZS 350 TU.
 
Back
Top Bottom